Wasia

Egypt's Dar Al-Ifta

Wasia

Question

 Sisi ni Jumuiya ya Kiheri, inafanya kazi katika uwanja wa kuzitoa misaada, na matendo ya malezi na wema kwa wazee na mayatima, na matukio ya uboreshaji wa elimu na utamaduni na Dini, na wenye pupa ya kudumu ni kwamba rasilimali za Jumuiya ziwe za halali na zitumike katika halali.
Kwa sababu hiyo tunaomba fatwa yenu katika msimamo wa (oni la) kisheria kwa zawadi kutoka mwanamke mwema anataka kuipa kwa Jumuiya yetu, Na zawadi ni aina ya upande mmoja wa nyumba unaoufanyia kazi na kuingiza kipato kila mwaka na hili halina ubaya wowote, na idadi kubwa ya wafanyakazi hunufaika na pato hilo ambapo mmiliki wa nyumba hiyo huwa anajihimiza na kuongeza idadi ya watu wanaonufaika pamoja na kuongeza mishahara yao kwa wingi, na pawepo na ongezeko la faida lililo safi baada ya hapo, na umiliki wa nyumba hurejea kwa jumuiya kama zawadi baada ya maisha yake.
Na ulizo uwe juu ya uhalali wa jambo hilo, kwa kujua kwamba yeye ana upande wengine wa nyumba kwa kiasi chenyewe cha pesa, zaidi ya anachokimiliki katika vito vya dhahabu na mali zinazoingia ambazo zinapaswa kuachwa kama urithi kwa ndugu wahusika, kwa kujua kwamba hakuna uhusiano wowote wa kiundugu kwa daraja la kwanza.
Naye anautashi wa kuusia mali alizoziacha kinyume na upande wa nyumba ya zawadi kwa kiwango cha theluthi moja kwa baadhi ya wafanya kazi wanaomtumikia pamoja na kuwalea wanyama wa kufugwa ni halali ya kufugwa kwao.
Na kwamba jumuiya inatashia kuikubalia zawadi njema hiyo, lakini baada ya kulielezea oni lako tukufu katika jambo hilo kwa ujumla, na kujua usahihi wake katika sheria.

Answer

 Kwa jina la Mwenyezi Mungu, na sifa njema ni zake, na rehema na amani zimshukie Bwana wetu Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, na Aali zake na Masahaba wake na wafuasi wake, na baada ya hayo:
Zawadi: ni miliki inayopatikana papo hapo. Na inahusu kila kitu maishani bila ya kuwa na sifa ya kukirejesha kilichotolewa. Na mfungamano wa zawadi ni kwa kauli yetu: wakati wa uhai, itatoa wasia; kwani wasia ni miliki inayohamishwa baada ya kifo kwa njia ya kujitolea, iwe imeusiwa kama kitu au kama manufaa. Na kanuni ya biladia ya Kimisri iliujulishia wasia basi ikasema: Wasia: ni tendo au hatua inayochukuliwa katika mali iliyoachwa baada ya kifo.
Na umilikishi katika wasia hautimizi ila kwa ukubaliano ambao hauwi ila baada ya mauti, hata kama ikiwa kukubali kwake ni katika wakati wa uhai, lakini uhakika wake wa kumiliki haukamili.
Wanazuoni wamejuzisha wasia kwa jumuia (au nyingine) ya kuhudumu watu kwa ujumla na kwa sharti isiwe ni katika upande wa maasi, wakasema katika kitabu cha: [Al-Menhaaj 67/4, Ch. Dar Al-Kutub Al- Elmiyah] na maelezo yake kwa mwanazuoni mkubwa Asherbiniy: "Ikiusiwa kwa jumuia (au nyingine) ya kuhudumu watu kwa ujumla, basi (sharti ya usahihi wake) ni isiwe katika upande wa maasi. Na kanuni ya wasia ya Kimisri nambari ya 71 kwa mwaka wa 1946 ilitaja katika mada ya saba kuwa: "Wasia unafaa kwa ajili ya maeneo ya ibada na taasisi za kujitolea na nyingine nyingi miongoni mwa pande mbali mbali za wema pamoja na taasisi za kisayansi na vile vile masilani."
Ama kuhusu kiwango kinachousiwa nacho; basi wasia Ima iwe kwa theluthi moja au chini yake, na ikawa zawadi inatekelezeka bila ya kuwepo haja ya idhini ya warithi, au ima iwe Zaidi ya theluthi moja, ikatekelezwa katika theluthi moja tu na kusitishwa kutolewa kilichozidi theluthi moja hata kwa idhini ya warithi, na ikiwa wataidhinisha itajuzu na kama hawakuidhinisha haitatekelezwa kwa kiwango hicho kilichozidi. Na Ibn Qudamah akasimulizi Ijmai juu ya hayo katika kitabu chake: [Al-Mughniy 62/6, Ch. Dar Ihiyaa Aturath Al-Arabiy].
Imamu Al-Bukhariy na Muslim walipokelea –na kitamko kwa Al-Bukhariy- kutoka kwa Saad Bin Abi Waqaasw, R.A. akasema: nimesema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Je, niusie kwa mali yangu yote? Akasema: "Hapana". Nikasema: Nusu ya mali yangu? Akasema: "Hapana". Nikasema: Thuluthi ya Mali yangu? Akasema: Basi thuluthi na theluthi moja ni nyingi; hakika wewe unapowaacha warithi wako wakiwa na utajiri ni bora zaidi kuliko kuwaacha wakiwa masikini wanaowaomba watu wengine wawasaidie"
Na imetajwa katika kanuni ya wasia ya Kimisri inayoiashiria nayo katika mada yake ya thelathini na saba; Wasia unasihi kwa theluthi moja kwa mrithi na mwengineo, na hutekelezwa bila ya kuruhusiwa na warithi, na unaswihi kwa ongezeko la theluthi moja, lakini hautekelezwi kwa nyongeza isipokuwa kwa kuruhusiwa na warithi baada ya kufariki kwa muusiaji, na wakawa ni watu wa kujitolea kwa wengine na wanajua kwa waliyoiruhusia.
Na kutokana na hayo; Basi hakika akitakacho mwanamke mwema ni kupelekwa katika jumuiya yenu kipato safi cha faida na umiliki wa nyumba ya waliotajwa hauzingatiwi kuwa ni zawadi bali ni wasia; kwani mwenye kumiliki mali ataongeza umiliki wake baada ya kifo chake, na hii inakwenda kinyume na zawadi ambayo hupatikana kwa umiliki wake hapo hapo.
Na wasia wake wa nyumba iliyotajwa na faida kamili inayopatikana kwa ajili ya jumuiya hiyo ya kujitolea ni sahihi kuitekeleza ikiwa kiwango chake hakivuki theluthi moja ya miliki zake, na hakuna ubaya wowote kwao kuzikubali mali hizo pale zinapotolewa.
Ama wasia wake wa pili kwa baadhi ya wafanyakazi katika huduma yake, au kwa ulezi wa wanyama wake wafungwao, basi haina ubaya yoyote pia, na utakuwa umejuzu na unatekelezwa bila ya haja kwa kuruhusia warithi kama haikuzidi jumla ya aliyoyausia nayo kwa jumuiya yenu na wafanyikazi hao kiwango cha thuluthi moja. Na iwapo itaongezeka zaidi ya theluthi moja, basi ikiwa inajuzu nyongeza hiyo basi itakuwa ni yenye kusitishwa kwa idhini ya warithi, na yanayo bora zaidi -ni kutoka katika tofauti ya anayezuia wasia kwa kilichozidi theluthi moja, miongoni mwa wanazuoni ni kuwa mwema aliyetajwa arejeshe ugawi wa theluthi hiyo kwa wote waliotajwa katika nyasia mbili, au achague baadhi yao au mmoja wao na akamtengea wasia wake, na yote haya ikiwa mtu huyu mwema ana warithi.
Ama ikiwa hana mrithi yeyote basi atalazimika kuusia amtakae katika mali zake, na wasia wake utatekelezwa hata kama utaitumia mali yake yote, kwani kizuizi cha nyongeza katika theluthi moja huwepo kwa ajili ya kuwapo haki ya warithi, na hupotea kwa kutokuwapo kwao.
Al-Haswkafiy alisema katika kitabu cha: [Aduru Al-Mukhtaar 652/6, pamoja na kitabu cha: Hashiyat Ibn Abdiin, Ch. Dar Al-Kutub Al-Elmiyah]; "Na ulisahihika (yaani wasia) kwa mali yote kama hakuwa na warithi wake yaani mwenye wasia.
Na Al-Bahutiy akasema katika kitabu cha: [Sharhu Muntaha Al-Iradat 445/2, Ch. Aalam Al-Kutub] Na unasahihiwa wasia kutoka watu hawana mrithi daima, kwa mali yake yote, inapokelewa na Ibn Masu'ud; kwani uzuio kutoka uongezeko wa thuluthi ni kwa haki ya mrithi na huyo hayupo.
Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ni Mjuzi zaidi.

 

 

Share this:

Related Fatwas