Uamuzi wa Sharia juu ya “kukubalika...

Egypt's Dar Al-Ifta

Uamuzi wa Sharia juu ya “kukubalika kwa fidia”

Question

Muislamu akiharibu kitu kutoka katika mali ya wengine, je anawajibika kulipa fidia yake, na ni ipi hukumu ya kukubali fidia hii?

Answer

Kuchukua fidia ambayo baadhi ya watu wanaiita "Iwadh", ikiwa inahukumiwa na watu wenye uwezo kama vile wenye mamlaka ya mahakama au wasuluhishi katika mizozo na kunufaika nayo inajuzu kisheria, na hakuna katazo ndani yake. Hakuna tofauti kati ya kosa na nia katika dhamana, na hakuna tofauti kati ya mtu kuwa mtoto, mwendawazimu, amelala, au mjinga, kwa sababu hiyo haina athari kwa dhamana. Ambapo Wanachuoni wa Fiqhi walikubaliana juu ya uhalali wa dhamana, kuhifadhi haki, na kupunguza uvamizi wa mali ambazo zina msingi maisha. Pia walikubaliana kuwa uharibifu ni moja ya sababu za dhamana. Kama mtu akiharibu mali za mtu mwingine kwa makusudi au kwa makosa, ni lazima awe na dhamana, na dhamana ya mali ni sawa na mali hizo. Kwa mujibu wa kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na mkilipiza basi lipizeni sawa na vile mlivyo adhibiwa. } [Al-Nahl: 126], Vile vile dhamana inakuwa kwa kukadiriwa kwa thamani ya siku ya uharibifu, na jambo hilo ni juu ya uamuzi wa hakimu au yeyote anayechukua nafasi yake.

Share this:

Related Fatwas