Kuingilia faragha ya watu

Egypt's Dar Al-Ifta

Kuingilia faragha ya watu

Question

Ni nini hukumu ya kuingilia faragha za watu?

Answer

Kuheshimu faragha za wengine ni wajibu wa kidini na wa maadili; kwa hivyo Uislamu umekataza dhihaka na kufunja heshima; Mwenyezi Mungu amesema: {Enyi mlio amini! Wanaume wasiwadharau wanaume wenzao, wala wanawake wasiwadharau wanawake wenzao. Huenda hao wakawa bora kuliko wao. Wala msivunjiane hishima, wala msiitane kwa majina ya kejeli. Ni uovu kutumia jina baya baada ya kwisha amini. Na wasio tubu, hao ndio wenye kudhulumu} [Al-Hujurat: 11], na Mwenyezi Mungu amesema: {wala msianze uadui. Kwani Mwenyezi Mungu hawapendi waanzao uadui.} [Al-Baqarah: 190], na Mtume (S.A.W) amesema: "Kitu kizito kabisa katika mizani ya muumini siku ya Kiyama ni tabia njema, na hakika Mwenyezi Mungu hakubaliani na mwenye kufanya mambo machafu na mabaya" (Imepokelewa na Al-Bukhari katika Al-Adabu Al-Mufrad), na Mtume (S.A.W) amesema: "Katika ukamilifu wa Uislamu wa mtu ni kuyaacha yasiyomuhusu" (Imepokelewa na At-Tirmidhi); kwa hivyo kushambulia au kuumiza wengine - hata kwa neno au jicho - ni kulaaniwa kisheria.

Share this:

Related Fatwas