Kulawiti

Egypt's Dar Al-Ifta

Kulawiti

Question

“Nilisoma kwenye mtandao mhadhara wa Mwislamu ambaye ni Mjerumani anazungumzia kulawiti kwa mtazamo wa Uislamu. Hapa kuna baadhi ya dondoo:
Amezungumzia Hadithi ya Luti na watu wake ilisimuliwa ndani ya Qur'ani kwa namna tofauti kidogo. Wafasiri waliona katika kisa cha Luti kilichotajwa ndani ya Qur’ani ushahidi kwamba kulawiti, au kwa hakika zaidi kujamiiana kati ya wanaume, ni dhambi na kwamba huleta ghadhabu ya Mwenyezi Mungu.
Ufafanuzi huu unasababisha matatizo kadhaa: moja wapo ni kwamba matini ya Qur-ani haizungumzi kwa uwazi juu ya ngono, na wala haitaji kulawiti, kutamani wavulana au kujamiiana kinyume na maumbile (maneno haya hayakutajwa ndani ya Qur-ani). Mengi ya yale ambayo yamejulikana kama ngono katika Kiarabu ni maneno “Nyinyi mnawaingilia wanaume kwa matamanio”. Hii haimaanishi kufanya ngono.
Kujua kwamba marejeo ya hamu ya kulawiti na kutenda kitendo cha watu wa Luti ni suala la balagha na kwamba kuwalaumu wanaume katika watu wake, ambaye aliamrishwa kuwaonya, kulikuwa ni makatazo tu.
Pili: Suala hapa linahusu wanaume waliooa - wake wanatajwa waziwazi.
Tatu: Wanafanya jambo ambalo linaonekana kuwa la kisasa “hajakutangulieni yeyote kwa uchafu huo katika viumbe vyote” (Al-A’raf aya 80, Al-Ankabut aya 29).
Hii haikubaliani kabisa na kile tunachojua leo juu ya ulawiti. Mwanamume wa kawaida ambaye ni Shoga katika zama za kisasa haoi mwanamke, licha ya kujua kwamba ulawiti umekuwepo kati ya wanadamu katika kila mahali na kwa njia tofauti sana.
Hivyo mtu anapaswa kuuliza: Je, ni kosa gani hasa la watu wa Luti?
Jambo jingine ambalo lazima lizingatiwe ni kwamba baadhi ya hadithi za Luti katika Qur'ani zinaonya kwamba uhalifu wa watu wa Luti hapo mwanzo ulikuwa ni jaribio lao la kuwabaka Malaika waliokuja kama mitume kwa Luti (katika sura ya wanadamu. ) (Surat Hud: Aya 78-81, Surat Al-Hijr: aya 68 -71, Surat Al-Qamar: Aya 37).
Hivyo, jambo linahusu ukiukwaji, ubakaji, dhuluma, mateso na unyanyasaji wa haki za wageni. Hadithi ya Luti haina uhusiano wowote na upendo, uhusiano na urafiki. Kutokana na hadithi hiyo haiwezekani kufahamu hukumu ya ushoga kati ya wanaume wanaopendana na, vile vile, kati ya wanawake.
Chanzo cha pili ambacho ni muhimu pia ni “Sunna.” Idadi kubwa ya Hadithi hizi zinanasibishwa kwa Mtume, na kwa mujibu wake, Mtume (S.A.W.) anawalaani wale wanaofanya vitendo vya watu wa Luti kwa kiwango ambacho kinahitaji kuuawa na kupigwa mawe mashoga. Inastahiki kuona kwamba vitabu viwili ambavyo ni muhimu zaidi katika Hadith sahihi, yaani Sahih Al-Bukhari na Sahih Imam Muslim, havina Hadithi hizi, na kwamba wanavyuoni wakubwa hawakusema kwamba Hadithi hizi ni sahihi na kuzihukumu kuwa ni batili, Tunamtaja hapa, kwa mfano, Ibn Hazm Al-Andalusi maarufu, ambaye alipingana naye katika kitabu chake kirefu cha fiqh “Al-Muhalla” (karibu mwaka 1030 AD). Hadithi zote zilizotajwa na wengi wa wanavyuoni wa Fiqhi wa kale kwa ajili ya kutoa dalili ya adhabu ya kifo kwa ushoga. (Kwa mnasaba huu, Ibn Hazm ndiye mwandishi wa kitabu maarufu zaidi cha Kiarabu juu ya mapenzi [Tawq Al-Hamamah], ambamo alishughulikia suala la mapenzi kati ya wanaume, ambalo katika kesi hii, kulingana na mtazamo wa mwandishi, linapaswa kubaki safi.)
Hatimaye, sheria ya Kiislamu, iliyoibuka katika karne za kwanza baada ya Mtume Muhammad, ilitumia Hadithi hizi kuweka adhabu kali kwa kosa la kulawiti.
Kwa hiyo, wakafasiri, kwa kuzingatia rai iliyoenea kuhusu yale yaliyotajwa ndani ya Qur’ani kuhusu kisa cha Luti, kwamba kosa la watu wa Luti ni kuingiliana kinyume na maumbile kati ya wanaume, na adhabu ya uhalifu huu lazima iwe kali sana: kwa kupigwa mawe au kutupwa kutoka mlimani au kuchomwa mwili ukiwa hai, na adhabu hii mwisho inafanana na matokeo ya uharibifu wa kijiji cha watu wa Luti, lakini hii inawezekana kuwa imechukuliwa kutoka katika sheria ya Kikristo ya Kirumi. Kama mtu akiangalia historia ya Kiislamu, atagundua kwamba adhabu hizi za kutisha, ambazo zimetajwa hapo juu, hazikutumika kwa ujumla.
Kinyume chake kabisa: ulawiti, haswa katika mfumo wa kutamani kufanya ngono pamoja na watoto, ulikuwa wa kawaida, na utafutaji wa mashoga haukuwahi kukuzwa kama ilivyokuwa katika Ulaya enzi za kati.
Kuna swali muhimu ambalo halijaulizwa katika eneo hili kuhusu upendo na urafiki. Imetajwa ndani ya Qur’ani (Surat Al-Roum, Aya 21) kwamba Mwenyezi Mungu aliwaumbia watu wanandoa ili waishi nao, na wapate kwao mapenzi na rehema, kwa sababu katika hayo zimo ishara kwa wanaotafakari miongoni mwa watu.
Na usemi katika Aya unawajumuisha watu wote, wawe wanamume au wanawake. Neno la Kiarabu “Mume” linaweza kutumika kwa mwanaume na mwanamke, na si lazima liwe na maana ya mke, kama lilivyoelezwa na wafasiri wengi wa Qur’ani.
Kila binadamu - akiwa ni shoga Muislamu mwanamume au mwanamke anaruhusiwa katika hili kukiri hasa kwa upendo na urafiki. Hii ina maana kwamba uhusiano wa mwanamume na mwanamume au mwanamke kwa mwanamke pia unapaswa kuwa na nafasi katika Uislamu.
Swali:
Ninakuomba utoe maoni yako juu ya maelezo haya yenye mantiki ya kusisimua, vile vile ninakuomba utoe ufafanuzi wa neno “Kulawiti” kwa mtazamo wa Kiislamu?
Je, hali ya kukumbatia, kumbusu na kuweka mkono wa mtu mkononi wakati wa kutembea ni kulawiti? Je, ulawiti kwa wanaume wawili ni kuchezea kwao uume na korodani zao?
Au ulawiti unatazamwa katika Uislamu kuwa ni kuingilia kunyume cha maumbile baina ya wanaume tu?
Na naomba udhuru wa kukuletea mada hii, lakini mada hii inajadiliwa sana Ujerumani na Magharibi, kwa kweli ndoa kati ya mashoga imekuwa halali katika baadhi ya nchi, pia kuna baadhi ya habari katika Kanisa la Kiinjili ambazo hazikatai
 

Answer

 Shukrani zote ni za Mwenyezi Mungu peke yake, rehema na amani zimwendee Mtume wa mwisho naye ni Mtume Muhammad S.A.W pamoja na watu wa nyumbani kwake na Masahaba zake na mwenye kumfuata kwa wema mpaka Siku ya Malipo.
Mungu amekataza kulawiti, kitendo hiki kibaya ambacho kinajumuisha maovu makubwa
Na zikaja Aya zenye kubainisha uharamu huu, Mwenyezi Mungu Akasema: {Na tulimtuma Lut', alipo waambia watu wake: Je, mnafanya uchafu ambao hajakutangulieni yeyote kwa uchafu huo katika viumbe vyote! (80) Hivyo nyinyi mnawaingilia wanaume kwa matamanio mkawaacha wanawake? Kumbe nyinyi ni watu wafujaji! (81) Na haikuwa jawabu ya kaumu yake isipo kuwa kuambizana: Wafukuzeni katika mji wenu, maana hao ni watu wanao jitakasa. (82) Basi tukamwokoa yeye na watu wake, isipo kuwa mkewe, alikuwa miongoni mwa walio bakia nyuma. (83) Na tukawamiminia mvua. Basi tazama jinsi ulivyo kuwa mwisho wa wakosefu (84).} [Al-A’raf:80-84]
-Lakini Qur’ani Tukufu inatumia kutoka katika lugha maneno ya juu kabisa yenye kuleta maana bila ya kuumiza hisia za mwanadamu kwa kutumia maneno ambayo hayafai.
-Mwenye kuangalia Sheria tukufu hapati tofauti katika kitendo hiki baina ya wanaume waliooa na wasiooa kwa upande wa uharamu wake.
-Ama kauli yake Mola Mtukufu: “Hajakutangulieni yeyote kwa uchafu huo katika viumbe vyote.” Maana yake ni kuzidisha hatia, na wala haikusudiwi kukataza kitendo hicho kwa sababu ni uzushi, na ikiwa haikuwa uzushi, kwa mfano, bali ni cha zamani, basi kingeruhusiwa.
Ama kilichotajwa na muulizaji juu ya kukosekana uwazi wa kosa la watu wa Nabii wa Mwenyezi Mungu Luti, (A.S.), jambo hilo halikutajwa hivyo, dhambi ya kweli ya watu wa Nabii Luti ni kuingiliana wanaume kinyume na maumbile.
Ama yale waliyojaribu kufanya watu wa Mtume wa Mwenyezi Mungu Luti pamoja na Malaika ni dhambi nyingine.
Kutoa dalili kutoka katika Hadithi tukufu sio kwa ajili ya kuthibitisha asili ya hukumu, lakini kwa ajili ya kuthibitisha uharamu wa kulawiti kwa mujibu wa Aya za Qur’ani. Ukweli kwamba Imamu Al-Bukhari na Imamu Muslim hawakuitaja hukumu hii haioneshi kwamba haijathibitika kwa jumla, Imamu Al-Bukhari alitaja katika tafsiri ya Aya tukufu za Surat Al-Naml (Na Lut'i alipo waambia watu wake: Je! Mnafanya uchafu nanyi mnaona?...). [An-Naml: 54] Amesema: “Uchafu ni kitendo kibaya na cha kuchukiza, nacho ni ulawiti.
Majibu ya Imamu Ibn Hazm kuhusu hukumu ya kifo kwa ushoga hayamaanishi kwamba hakukataza kitendo hiki kiovu, na kitabu cha “Tawq Al-Hamamah” hakina uhusiano wowote na kitendo hiki kiovu.
{Na tulimtuma Lut', alipo waambia watu wake: Je, mnafanya uchafu ambao hajakutangulieni yeyote kwa uchafu huo katika viumbe vyote! (80) Hivyo nyinyi mnawaingilia wanaume kwa matamanio mkwaacha wanawake? Kumbe nyinyi ni watu wafujaji! (81) Na haikuwa jawabu ya kaumu yake isipo kuwa kuambizana: Wafukuzeni katika mji wenu, maana hao ni watu wanao jitakasa. (82) Basi tukamwokoa yeye na watu wake, isipo kuwa mkewe, alikuwa miongoni mwa walio bakia nyuma. (83) Na tukawamiminia mvua. Basi tazama jinsi ulivyo kuwa mwisho wa wakosefu (84).} [Al-A’raf:80-84]
Al-Qurtubi amesema katika tafsiri yake Aya za Surat Al-A’raf 80: “Wanachuoni wameafikiana kwa kauli moja kwamba kulawiti ni haramu.
Aya zilizotajwa katika usemi wenu {Na katika Ishara zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao. Naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. Hakika katika haya bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanao fikiri} [Ar-Rum: 21] haihusiani na ndoa kati ya wanaume wawili na wanawake wawili. Ufahamu huu ni kosa tu, sio kutoka katika lugha, na ni kutojali misingi ya sheria tukufu.
Tunawashauri wale ambao wamezoea kitendo hiki cha kinyama watafute daktari mwadilifu na kujaribu kutibu ugonjwa huu mbaya.
Ama kilichotajwa na muulizaji kuhusiana na hukumu ya kukumbatiana, kumbusu na kuweka mkono wake mkononi wakati wa kutembea, hii sio kulawiti, lakini ni miongoni mwa tangulizi za kitendo hiki kiovu.
Ama swali lake kuhusu wanaume wawili kuchezea kwao uume na korodani, kitendo hicho ni haramu kabisa.

Share this:

Related Fatwas