Kufurahia ugonjwa
Question
Je, ni ipi hukumu ya mtu anayefurahia ugonjwa wa mtu mwingine?
Answer
Kufurahi juu ya masaibu na mitihani inayowapata wengine - ikiwa ni pamoja na kifo - sio maadili mema, na mwenye kufurahia kifo atakufa kama wengine wamekufa? Je, mtu angefurahi akiambiwa: Fulani anafurahia kufa kwako?! Mtume (S.A.W) amesema: “Usioneshe kumchekelee ndugu yako kwa bezo, basi Mwenyezi Mungu asije kumsamehe yeye na akakujaribu wewe”. Hadithi hii imepokelewa kutoka kwa At-Tirmidhi. Kufurahi na kustarehesha katika mateso yanayompata mtu - vyovyote iwavyo - ni kinyume na maadili ya kinabii yenye kuheshimika na utu wema wa mwanadamu, na misiba inapotokea, ni lazima kuzingatia na mawaidha, bila kufurahishwa na mateso ya watu.
Arabic
Englsh
French
Deutsch
Urdu
Pashto
Hausa
