Kukutana mwanamke na mwanamume chum...

Egypt's Dar Al-Ifta

Kukutana mwanamke na mwanamume chumba kimoja kazini

Question

Ni ipi hukumu ya kukutana mwanamke na mwanamume katika chumba kimoja kazini?

Answer

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na rehma na amani zimwendee bwana wetu Mtume wa Mwenyezi Mungu, jamaa zake, Maswahaba wake na wanaomfuata. Na baada ya hayo:

Hakuna kizuizi kisharia kuwepo mfanya kazi wa kiume na mwenzake wa kike kazini katika chumba kimoja, ikiwa chumba hakikufungwa au katika hukumu ya faragha, kwa kauli ya Mtume S.A.W.: “Asikae faragha mwanamume na mwanamke isipokuwa pamoja Mahrim” imepokelewa na Bukhari.

Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ni Mjuzi Zaidi

Share this:

Related Fatwas