Mwanaume kudai kurudushiwa zawadi ya uchumba "Shabka" kutoka kwa mwanamke
Question
Nini hukumu ya zawadi ya uchumba Shabka[1] mwanaume anapotaka irejeshwe?
[1] Shabka Ni vito ambavyo mwanamume humpa mwanamke anayetaka kumuoa. Pete ya uchumba mara nyingi hutengenezwa kwa dhahabu, na inaweza kutengenezwa kwa vito vya thamani, kama vile almasi na kadhalika.
Answer
Shabka ni vito anavyotoa mwanamume kwa mwanamke anayetaka kumuoa. Mara nyingi huwa ni dhahabu au vito vya thamani kama almasi na mfano wake. Kimila imekuwa ikichukuliwa kama sehemu ya mahari, na hivi ndivyo Fatwa na Mahakama za Misri zinavyofanya kazi.
Ikitokea hitilafu kati ya pande mbili kuhusu urejeshaji wa Shabka, jambo hilo huachiwa hakimu kulingana na ushahidi na hoja zinazopelekea uamuzi; ikithibitika kwake kuwa Shabka yote au sehemu yake ni mahari, huamuru irejeshwe kwa mwanamume kwa namna ifuatayo:
Wakati wa kuvunja uchumba: Ana haki ya kurejeshewa Shabka.
Wakati wa talaka kabla ya kuingiliana (ndoa kutimizwa): Ana haki ya kurejeshewa Shabka au sehemu yake, isiyozidi nusu ya thamani ya mahari.
Wakati wa talaka baada ya kuingiliana: Hana haki ya kurejeshewa Shabka.
Wakati wa Khulu' (mwanamke kujivua ndoa): Ana haki ya kurejeshewa Shabka.
Maelezo
Mwanaume anapomdai mwanamke amrejeshee Shabka, hali haiwezi kuwa nje ya mambo yafuatayo:
Kwanza: Katika hali ya kuvunja uchumba, mwanaume ana haki ya kudai irejeshwe, na mwanamke lazima amrudishie; kwa sababu ni sehemu ya mahari ambayo mwanamke anastahiki baada ya ndoa tu, na uchumba si ndoa bali ni ahadi ya ndoa.
Pili: Katika hali ya talaka kabla ya kuingiliana, mwanamke anastahiki nusu ya mahari. Wakati huo, inaruhusiwa mwanaume kuchukua kutoka kwenye Shabka kile chenye thamani ya nusu ya mahari na si zaidi ya hapo.
Tatu: Katika hali ya talaka baada ya kuingiliana, mwanaume hana haki ya kudai irejeshwe; kwani ni sehemu ya mahari, na mahari yote ni haki ya mwanamke ikiwa talaka imetokea baada ya kuingiliana.
Nne: Katika hali ya Khulu', mwanaume ana haki ya kudai irejeshwe, na mwanamke anayejitoa kwenye ndoa lazima amrudishie; kwa sababu ni sehemu ya mahari, na Khulu' inamlazimu mwanamke kurejesha mahari yote kwa mwanaume.
Tunapata faida kutokana na yaliyotangulia:
Kwamba Shabka anayotoa mwanaume kwa mwanamke anayetaka kumuoa, kimila imekuwa ikichukuliwa kama sehemu ya mahari, na hivi ndivyo Fatwa na utaratibu wa Mahakama ya Misri unavyoelekeza. Ikitokea hitilafu kati ya pande mbili kuhusu kurejesha Shabka, jambo hilo huachiwa hakimu kulingana na ushahidi na bayana zinazopelekea uamuzi kwake; ikiwa itathibitika kwake kuwa Shabka yote au sehemu yake ni mahari au ni sehemu ya mahari, basi ataamuru irejeshwe kwa mwanaume kwa namna ifuatayo:
Wakati wa kuvunja uchumba: Ana haki ya kurejeshewa Shabka.
Wakati wa talaka kabla ya kuingiliana: Ana haki ya kurejeshewa Shabka au sehemu yake, kwa kiasi kisichozidi nusu ya thamani ya mahari.
Wakati wa talaka baada ya kuingiliana: Hana haki ya kurejeshewa Shabka.
Wakati wa Khulu' (mwanamke kujivua ndoa): Ana haki ya kurejeshewa Shabka.
Arabic
Englsh
French
Deutsch
Urdu
Pashto
Hausa
