Ndoa ya Urfi (Ndoa Isiyosajiliwa) ...

Egypt's Dar Al-Ifta

Ndoa ya Urfi (Ndoa Isiyosajiliwa)

Question

Nini hukumu ya ndoa ya Urfi?

Answer

Ndoa ya Urfi ni halali kisharia ikiwa itatimiza nguzo na sharti za ndoa sahihi, nazo ni: Ijab na Qabul (Nimekuozesha binti yangu – Nimekubali kumuoa), mashahidi wawili na mahari, na mkataba wa ndoa uwe hauna vizuizi vya kisharia; mfano wa kizuizi cha kisharia: Kuoa dada wa kunyonya, au kuoa shangazi au dada wa mama.

Ama kwa binti mdogo (chini ya umri wa kisharia) kujiozesha mwenyewe kwa njia ya Urfi; hilo halijuzu; kwa sababu Jamhuri ya Wanazuoni wameshurutisha uwepo wa walii wa mwanamke katika mkataba wa ndoa. Ama maoni ya baadhi ya Wanazuoni katika kutoshurutisha walii; yanahusu mwanamke aliyebaleghe na mwenye utambuzi (rashida) ambaye anajiozesha mwenyewe kwa mwanaume anayelingana naye.

Maelezo

Mkataba wa ndoa sahihi ni ule uliotimiza sharti na nguzo za kisharia zifuatazo:

1- Kutoa na kukubali (Ijab na Qabul).

2- Mashahidi wawili.

3- Mahari.

4- Kuhudhuria kwa walii wa mke kwa Jamhuri ya Wanachuoni wa Fiqhi, na Madhehebu ya Imamu Abu Hanifa — ambayo ndiyo yanayotolewa Fatwa na kufanyiwa kazi katika mahakama za Misri — ni kutoshurutisha walii kwa mwanamke mwenye akili aliyefikia umri wa kuwajibika [1].

5- Mkataba wa ndoa uwe hauna vizuizi vya kisharia, kama mwanamke kuwa haramu kwake; kama dada wa kunyonya, shangazi, au dada wa mama.

Wakati wowote nguzo na sharti hizi zinapopatikana katika mkataba wa ndoa, unakuwa ni sahihi iwe ni ndoa rasmi[2] au ndoa ya Urfi, na unazalisha athari zake za kisharia, ambazo ni pamoja na:

Kuthibitika kwa matumizi (nafaka) ya mume kwa mkewe.

Kuruhusiwa kwa muingiliano (tendo la ndoa) kati ya wanandoa.

Mwanamke kustahili nusu ya mahari kabla ya kuingiliana, na mahari yote baada ya kuingiliana.

Watoto kunasibishwa na mume ikiwa mwanamke atazaa naye.

Kuthibitika kwa urithi kati yao.

Kutoruhusiwa kuoa wake wanne wengine zaidi yake.

Kutoruhusiwa kumkusanya yeye na mwanamke ambaye ni haramu kukusanywa naye; kama dada yake wakati wa ndoa.

Mwanamke kutoruhusiwa kuolewa na mwingine isipokuwa baada ya kupewa talaka na kumaliza eda yake.

Tunapata faida kutokana na yaliyotangulia:

Kwamba mkataba wa ndoa ikiwa umetimiza nguzo na sharti na ukawa hauna vizuizi vya kisharia, unakuwa mkataba sahihi, na unazalisha athari zake za kisharia, iwe ni ndoa rasmi au ndoa ya Urfi.

 

[1] «(Rashida)»: Mwanamke mwenye akili aliyefikia umri wa kuwajibika.

[2] «Ndoa rasmi»: Mkataba wa ndoa uliosajiliwa kiserikali..

Share this:

Related Fatwas