Tofauti kati ya Udini na Ujuzi wa D...

Egypt's Dar Al-Ifta

Tofauti kati ya Udini na Ujuzi wa Dini.

Question

Je! Kuna tofauti kati ya ujuzi wa dini na udini? 

Answer

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na rehma na amani zimwendee bwana wetu Mtume wa Mwenyezi Mungu, jamaa zake, masahaba wake na wanaomfuata, na baada ya hayo:
Miongoni mwa misemo ya kawaida katika vitabu vya Fatwa ni usemi wao: (Chukua Fatwa yake na usizingatie uchamungu wake), ambayo ni kanuni nzuri inayoonesha tofauti kati ya taaluma ya dini na udini wa vitendo, na kwamba taaluma ya dini ni taaluma kama taaluma zingine zote, kanuni, misingi, istilahi, mbinu, vitabu, mpangilio, shule, misingi, historia ... na kadhalika.
Inahitajika pia nguzo za mchakato wa kielimu, ambayo maarifa hayatimizwi isipokuwa kwazo, nayo ni: mwanafunzi, mwalimu, kitabu, mtaala, na mazingira ya kielimu. Na kwamba njia ya kujifunza ina daraja tofauti, kama daraja za elimu ya umma, kisha elimu ya Chuo Kikuu, kisha masomo ya juu kwa daraja zake tofauti, na pia ina njia zake ambazo ni tofauti za kuweza kuisimamia, baadhi yake ni ya kinadharia, na nyingine ni ya vitendo, na nyingine ni ya kimaisha na ya vitendo pia, na utendaji wake unatofautiana kutokana na utafiti wa kinadharia hadi kitabu cha masomo, kutafiti katika jarida linalopitiwa na wataalamu, hadi utafiti wa kujadiliwa au kama mhimili katika kongamano la jamii ya kielimu ambalo mwasilishaji anajulisha watafiti wengine kwa matokeo ya utafiti wake.
Na suala la jamii ya kielimu litakuwa tofauti kila wakati kulingana na vipawa vya kimungu, zawadi za milele, na Vipaji ambazo Mwenyezi Mungu humpa kila mtu ambaye hujulikana navyo zaidi kuliko wengine, na suala la utaalamu wa umma litaendelea kuzingatiwa na utaalamu maalumu unahitajika, na kutabaki tofauti kati ya wale ambao watafaulu kusoma masomo lakini hawafaulu maishani, na wale ambao watafaulu katika hilo. Na yeyote anayefikia kiwango cha hoja na rejeleo, na hashughulikii vizuri maisha au anayashughulikia vizuri, kama Shawqi alivyosema mwishoni mwa shairi lake (Kitabi):
Wangapi wanafaulu katika kupokea masomo
Lakini katika maisha yake hakufaulu
Tunaona maana hizi zote katika kila uwanja, na labda uwanja wa karibu zaidi ambao unatumika kama taaluma ya dini ni uwanja wa tiba na taaluma ya tiba. Tazama yote ambayo tumeyataja kama tukizungumza juu ya taaluma ya tiba ya mwili, wakati nilikuwa nikisisitiza kuhifadhi dini zote, na yote hayo yanatofautiana kuhusu haki ya watu katika kutunza afya zao, kuzuia magonjwa na kuyatibu, na misingi ya maisha yenye afya na afya ambayo kila mtu anatamani, bali ni haki yake, kama kwamba taaluma ya dini inatofautiana na udini, ambayo ni muhimu kwa kila mtu na inahitajika na kila mtu, lakini watu wanaihitaji kwa kiwango cha mtu binafsi na kikundi, na umma.
1- Ingawa kuna uwazi wa tofauti kati ya elimu ya dini na udini, au taaluma ya tiba na ulinzi wa afya ya umma, tofauti hii haitambuliwi mara nyingi katika tamaduni zetu, na tunaona machafuko mabaya ambayo yana sura zilizoenea katika sekta zote, na hakuna anayeokoa isipokuwa aliyepata rehema za Mwenyezi Mungu – nao ni wachache katika utamaduni wetu uliopo - na namwomba Mwenyezi Mungu Afungue ufahamu juu ya madai haya kwa ajili ya mapitio muhimu sana ya misimamo ya wanavyuoni wetu na wanafikra kuhusu msimamo wao juu ya hali hii.
2- Tunaona kinachothibitisha kwamba hakuna utambuzi wa tofauti kati ya elimu ya dini na udini, pamoja na kwamba Profesa wa sayansi, au kilimo, au uandishi wa habari, au uhandisi au tiba ameanza kuzungumzia Fiqhi, na kujadili Fatwa iliyotolewa na wale ambao wamebobea na kutumia maisha yake katika vyanzo na ufahamu wa ukweli, na hii ni kwa sababu yeye ni msomi wa dini, au kwa sababu hajui, au hajasadiki tofauti kati ya elimu ya dini na udini, na anaamini kuwa jambo hilo linaruhusiwa na linapatikana kwa wote.
3- Pia tunaona ukosefu wa ufahamu wa maana ya Fatwa. Ambapo imechanganyika na swali au maoni, ambayo ni swali na jibu, na maoni yanaonekana kutolewa kisha kujadiliwa, kwa hivyo Fatwa ni kama hukumu ya Jaji, na Jaji haufuati uamuzi huu baada ya kutolewa kwake na hajadiliwi, lakini inastahili kukata rufaa katika mahakama ya juu au kwa hitimisho katika mahakama Kuu. Hali ya kutoridhika na Fatwa inahitaji Fatwa kutoka kwa mamlaka ya juu, na haihitaji pingamizi kutoka hapa au kutoka huko, na hali ya kutoridhika na agizo la daktari haimaanishi kupuuza jambo hilo, lakini badala yake inahitaji ushauri kutoka kwa wale ambao ni wenye maarifa zaidi au uzoefu, na hakuna mtu yeyote aliye na haki ya kujadili daktari kwa maoni yake, na inatosha kukataa dawa na kukaa bila ya matibabu.
Watu wengi wangeogopa ikiwa tukiwatahadharisha kwa mfano huu na kuannza kukataliwa kwake na kudai kuwa hiki ni kuzuia cha maoni au cha uhuru wao, na jambo hilo halihusiani na maoni au uhuru kadiri linavyohusiana na njia ya mawazo yaliyonyooka ambayo lazima yafuatwe badala ya upuzi huu wa ujinga ambao kila mtu anazungumzia jambo ambalo halijui.
4- Vivyo hivyo, tunaona kwamba wakati swali linapoulizwa kwa kutaka taarifa, muulizaji na msikilizaji wanaamini kuwa jibu ni Fatwa, na mara moja muulizaji aliuliza juu ya habari za wake zake Mtume S.A.W. na tukamjibu na akaziingatia kuwa Fatwa kutoka kwetu, na tusipomjibu, hufahamu kwamba hali hii ni kama kukataa kutimiza wajibu wa Fatwa, na kuna maswali juu ya hali ya kisiasa ambayo maoni yanaweza kuelezewa, na hukumu ya kisheria kuhusu vitendo vya kibinadamu vya kawaida, kwa hivyo rafiki yetu hatofautishi kati ya hili na lile, na huzungumzia hata kwenye kurasa za magazeti na husababisha kuchanganyikiwa kwa mpokeaji. Ninamwoma Mwenyezi Mungu kwamba haikukusudiwa hivyo, na kwamba mbinu hii haikusudiwi kuhamisha elimu ya Fatwa kwa maoni ambayo yanaweza kujadiliwa bila ya kufuata mpangilio unaohitajika na hali hii, mfumo unaohitaji, na ujuzi unaofanya.
Ama sehemu ya pili ya msemo: (na usizingatie uchamungu wake), sio tu kwa kuhifadhi afya ya mtu anakuwa daktari, wala mara tu mtu anaposhika dini yake kuwa mwanachuoni, lakini suala hilo linahitaji Chuo Kikuu ambacho tunaomba kila mtu katika nyanja zote arudi kwenye Chuo ili umalizike mfumo wa wasiokuwa na ujuzi wowote, na ibaki elimu - na elimu peke yake - ni msingi wa utaalamu maridadi, na kumwondoa (ambaye hajui) anayeishi pamoja nasi, na kati ya methali za watu wa kawaida ambazo zinawakilisha Historia ya hekima na uzoefu wa wanadamu ni methali inayosema (mpe mkate mwokaji wake hata kama akila nusu yake).
Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ni Mjuzi zaidi.

 

Share this:

Related Fatwas