Kumsumbua mwenye kuswali

Egypt's Dar Al-Ifta

Kumsumbua mwenye kuswali

Question

Nini hukumu ya kumsumbua mwenye kuswali wakati wa kusimamisha Swala yake, kama vile kumchekesha, kwa mfano, na mengineyo?

Answer

Kumsumbua mwenye kuswali wakati wa Swala yake kwa kumchekesha na mfano wa hayo ni haramu kwa mujibu wa Sharia. Mwenye kufanya hivyo ni mwenye dhambi.

Swala ndio nguzo ya dini, na Swala ina utakatifu wake. Nayo ni mazungumzo yanayofanyika baina ya mja na Mola wake Mtukufu, na mja lazima afikie unyenyekevu ambao kwa mazungumzo hayo awe;  miongoni mwa wale ambao Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema: {HAKIKA wamefanikiwa Waumini (1) Ambao ni wanyenyekevu katika Swala zao(2)} [Al-Mu’minun: 1, 2]. Kwa hivyo, Uislamu unaharamisha kila kitu kinachopelekea usumbufu kwa mwenye kuswali, jambo ambalo linaathiri unyenyekevu wake, iwe kutoka ndani ya Swala au nje yake. Haifai kwa Muislamu kuingia katika utakatifu na utukufu wa Swala kwa kumfanya mwenye kuswali acheke au mfano wa hayo. Kwa sababu hiyo ni dhambi kubwa. Wanachuoni wa Fikhi hawakutofautisha kati ya kuwa kumsumbua mwenye kuswali ni kwa utiifu au kwa uasi, hivyo wakaweka sharti kuwa ni haramu na ni marufuku ikiwa ni kwa utiifu, hivyo kwa kumfanya mwenye kuswali acheke ni haramu zaidi.

Share this:

Related Fatwas