Zaka ya Hisa katika Makampuni Uwasi...

Egypt's Dar Al-Ifta

Zaka ya Hisa katika Makampuni Uwasilishaji wa Uchambuzi

Question

Zaka ya Hisa katika Makampuni Uwasilishaji wa Uchambuzi

Answer

Na

Hisham Rabih Ibrahim

Mtafiti wa Uzamili, Kitivo cha Sharia na Kanuni Cairo

Ufafanuzi wa Zaka

Ufafanuzi wa Zaka kwa mujibu wa lugha:

Zaka  katika lugha inaitwa kwa pamoja na maana kadhaa, ikiwa ni pamoja na:

* Ukuaji na kuongezeka, Ibn Faris amesema: “Za-Ka, ni herufi zinazoashiria kukua na kuongezeka.”.

* Kutakasa, ikiwa ni pamoja na kauli yake Mola Mtukufu: {Hakika amefanikiwa aliye itakasa} [AL-SHAMS: 9], maana yake: Ameitakasa na uchafu, Mola Mtukufu akasema: {Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.} [AL-A’LA : 14], na inasemekana kuwa zaka ni utakaso wa pesa; Inaitwa hivyo kwa sababu inatumainiwa kwake utakaso wa fedha, ambayo ni ongezeko na ukuaji wake. Al-Hafidh Al-Fath amesema: “Kwa sababu ni utakaso wa nafsi kutokana na uovu na utakaso wa dhambi. Mwenyezi Mungu anasema: {Chukua sadaka katika mali zao, uwasafishe na uwatakase kwazo} [AT TAWBAH: 103]

*Kusifu, ikiwa ni pamoja na kauli yake Mola Mtukufu: {Basi msijisifu usafi.} [AN-NAJM: 32], Na kutoka humo pia hali ya kuwasifu mashahidi, basi kinachokusudiwa ni kuirekebisha nafsi na kuieleza na kuisafisha, na mwanamume anajisifu ikiwa anaielezea na kusifu nafsi yake.

*Wema, imesemwa: mtu mchamungu na mwema, na wachamungu  watu wema.

Zaka  ya kawaida katika Sharia inaitwa kwa jina hili kwa sababu inategemea zaidi kutolewa kwa zaka ya pesa. Yaani kuongezeka na kukua kwake.” Imesemwa katika kitabu cha (Al-Maghrib): “Nayo maana hiyo ni dhahiri”.

Kwa juu juu, inaweza kuonekana kuwa zaka ni kupungua kwa pesa na hakuna kuongezeka kwake, basi hii inawezaje kuunganishwa na usemi wao kwamba moja ya maana zake ni ukuaji na kuongezeka?

Jibu la hilo: Zaka hupata ongezeko na kukua kwa kiasi kinacholipwa na Mwenyezi Mungu,, dalili ya hilo ni kauli yake Mtume wa Mwenyezi Mungu (S.A.W): “Hakuna yoyote yule atakayetoa sadaka isipokuwa Allah Mwingi wa rehema anaichukua (sadaka hiyo) kwa (mkono wake wa) kuliabasi anailea (sadaka hiyo) kama mmoja wenu anavyomlea mtoto wa farasi wake aundama wa ngamia wake. Basi (sadaka hiyo) inakua katika kiganja cha Allah Mwingi wa rehema mpaka inakuwa kubwa kuliko mlima, kama mmoja wenu anavyomlea mtoto wa punda wake au wa ngamia wake.” .

Pia huingia kwenye pesa kwa baraka na ukuaji kwa kuzingatia faida; Hayo ni kwa sababu fedha zinazochukuliwa humo zimebarikiwa na Mwenyezi Mungu na kukua, na zinarudi kwa wingi zaidi kuliko zilivyokuwa, na katika hilo Mtume (S.A.W) anasema: “Fedha hazipungui kwa sababu ya kutoa sadaka”.

Al-Hafidh Ibn Hajar amesema: “Zaka ni ukuaji. Kwa sababu kuitoa ni sababu ya kukua kwa pesa, au kwa maana ya kwamba malipo yanayotokana nayo yanaongezeka, au kwa maana ya kwamba zaka inaambatanishwa na pesa ambayo ina ukuaji wa biashara na kilimo, na ikasemwa: kwa sababu mmiliki hulipa ushuru kwa kulipa; Mwenyezi Mungu Mtukufu Amesema: {Chukua sadaka katika mali zao, uwasafishe na uwatakase kwazo} [AT TAWBAH: 103].

Al-Nawawiy amesema: “Wametaja mambo mawili katika Hadithi: moja wapo: maana yake ni kwamba Yeye humbariki na kuondosha madhara kutoka kwake, kwa hivyo upungufu wa sura unafidiwa na baraka iliyojificha, na hili linaelewela kwa kuhisi na ada. Na ya pili: kwamba hata ikiwa sura yake itapungua, malipo yaliyo juu yake ni fidia  ya upungufu wake na ongezeko kwa mara nyingi zaidi”.

     Na ikatajwa katika maelezo ya Al-Zarqaniy: “Fedha hazipungui kwa sababu ya kutoa sadaka, yaani Mwenyezi Mungu huzimdishia iliyopungua, na inawezekana kuwa zikipungua (mtoaji wa sadaka) atapata katika Akhera kinachofidia upungufu huo, na inawezekana kwamba kauli hii ina maana hizi mbili”.

Ufafanuzi wa zaka  kwa mujibu wa istilahi:

Ni vigumu kupata tofauti kubwa katika ufafanuzi wa zaka  miongoni mwa Wanachuoni wa Fiqhi wa Madhehebu, hata hivyo - zaka  - inaweza kuitwa makadirio ya fungu la pesa ambalo Mwenyezi Mungu aliwalazimishia watu kwa ajili ya wale wanaostahiki, kama ilivyoitwa pato la hisa hii yenyewe.

Kwa mujibu wa Hanafi, zaka ni: “Umiliki wa mali kutoka kwa Muislamu maskini ambaye si miongoni mwa Bani Hashim au mtumwa wao, isipokuwa manufaa hayo yatakatwa kutoka kwa mmiliki wa pesa kutoka kwa kila upande kwa ajili ya Mwenyezi Mungu”.

Na ikasemwa: "Umiliki wa pesa maalumu kwa mtu maalumu".

Wanazuoni wa madhehebu ya Imamu Malik wamesema: Zaka ni: “Kutoa mali maalumu kutoka katika mali maalumu inayofikia kiwango kwa anayestahiki, ikitimia kwa mmiliki na kupita mwaka”.

Na ikasemwa: “Zaka ni jina la sehemu ya mali, sharti la uwajibu wake kwa mnufaika ni kufikia kiwango cha mali, na chanzo cha kutoa kwa sehemu ya mali…” ( ).

Wanazuoni wa madhehebu ya Imamu Shafiy wameifasiri zaka kuwa: “Jina la kiasi malumu cha mali maalumu ambacho lazima kitumike kwa vitu maalumu kwa masharti” ().

Wanazuoni wa madhehebu ya Imamu Hanbali walisema: Ni: “Haki ya faradhi katika mali maalumu kwa ajili ya kundi maalumu na katika wakati maalumu”

Tofauti kati ya zaka  na ushuru:

Ushuru katika istilahi ya wanauchumi dhana yake inatofautiana kwa kuzingatia maendeleo yake ya kihistoria, lakini kile ambacho wanauchumi wamekizingatia katika enzi ya sasa ni kwamba ushuru ni: “Makato ya lazima anayobeba mfadhili na kulipa  bila malipo kulingana na uwezo wake wa kugharimia kama mchango kutoka kwake kwa matatizo ya umma, au ili kuziingiza katika mamlaka kwa ajili ya kufikia malengo fulani”.

Na ingawa zote mbili ushuru na zaka  zimeunganishwa na ukweli kwamba ni wajibu kimsingi, ambapo hakuna uchaguzi wa kulipa au kutolipa, lakini zaka ni wajibu kwa mujibu wa Sharia, na ushuru ni wajibu kwa mujibu wa kanuni, basi zinatofautiana katika masuala kadhaa, miongoni mwa masuala hayo ni pamoja na:

* Zaka hiyo ni wajibu kutokana na amri ya Mwenyezi Mungu Mtukufu na Mtume wake, yaani chanzo chake ni Sharia, na ushuru umewekwa na serikali, na kuanzia hapa hakuna yeyote ana haki ya kubadilisha hukumu ya sheria katika zaka na nyinginezo, jinsi hali zinavyobadilika, tofauti na ushuru ambapo dhima yake ni kutokana na mamlaka ya kutunga sheria, ambayo serikali ina haki ya kuulazimisha, au kuurekebisha uwajibu wake na kuufanya uwe wa hiari.

* Ushuru kwa mujibu wa ufafanuzi wake wa kisasa ni: "Makato ya mali...", wakati zaka  inajumuisha pesa taslimu na mali pia. Bali zaka ya mali inalipwa moja kwa moja kutoka humo, bali hairuhusiwi kuibadilisha kuwa kitu kingine kwa mujibu wa rai ya wanazuoni wengi, na hata wale waliosema kuwa inajuzu kulipa fedha badala ya mali hiyo walisema hivyo kwa makusudi ya thamani, kwa hivyo walizingatia mali hiyo kuwa ni asili kisha wameitathmini kwa thamani.

 *Kulipa ushuru hakuna malipo kwake wala thawabu isipokuwa ni kufikia maslahi ya Waislamu na mlipaji anakusudia kumridhisha Mwenyezi Mungu, wakati Zaka ina malipo makubwa kwa Mwenyezi Mungu katika malipo, thawabu na ukaribu na Mwenyezi Mungu.

* Zaka ni ibada ya kimali ya kidini, na ni nguzo moja miongoni mwa nguzo tano za Uislamu, na imelazimishwa kwa Waislamu tu, kwa ajili ya kukubaliwa kwake inahitaji nia, wakati ushuru hauhitajiki nia.

*Zaka inaweza kukusanywa au isikusanywe na serikali, na pesa inayoonekana inaweza kukusanywa bila ya zile zilizofichwa, na ikitokea kwamba serikali haifanyi kazi hii au serikali haipo, basi Zaka hiyo haiondoki watu binafsi, lakini badala yake ni lazima walipe Zaka  ya mali zao na kuzitumia katika benki zake halali, wakati ushuru unahusishwa na serikali tu.

Pili, Hukumu ya Zaka

Zaka ni nguzo moja miongoni mwa nguzo za Uislamu, na hakuna tofauti baina ya Wanachuoni wa Fiqhi kwamba zaka ni wajibu. Qura’ni, Sunna, Wanachuoni wa Fiqhi wote, na dalili za kiakili zimethibitisha hivyo:

Kwanza: Dalili katika Qura’ni Tukufu:

Zipo Aya nyingi ndani ya Qur’ani Tukufu zinazozungumzia Zaka na fadhila zake, na yale ambayo Mwenyezi Mungu amewaandalia wenye kuilipa Zaka, pia kuna Aya nyingine zinazoeleza kuwa ni wajibu katika mfumo wa faradhi zinazoashiria kuiomba bila ya kuiacha, zikiwemo dalili hizo:

Kauli yake Mwenyezi Mungu: {Na shikeni Swala, na toeni Zaka}[ AL BAQARAH: 43]. Vile vile kauli yake Mwenyezi Mungu: {Chukua sadaka katika mali zao, uwasafishe na uwatakase kwazo} [AT TAWBAH: 103]. Na kauli yake Mwenyezi Mungu: {Na Waumini wanaume na Waumini wanawake wao kwa wao ni marafiki walinzi. Huamrisha mema na hukataza maovu, na hushika Swala, na hutoa Zaka, na humt'ii Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Hao Mwenyezi Mungu atawarehemu.} [AT TAWBAH: 71]. Na kauli yake Mwenyezi Mungu pia: {Wale ambao tukiwapa madaraka katika nchi husimamisha Swala, na wakatoa Zaka, na wakaamrisha mema, na wakakataza mabaya} [AL-HAJ:41]. Na kauli yake Mwenyezi Mungu: {HAKIKA wamefanikiwa Waumini (1) Ambao ni wanyenyekevu katika Swala zao (2) Na ambao hujiepusha na mambo ya upuuzi (3) Na ambao wanatoa Zaka (4)} [AL-MU'MINUN:1-4] Na kauli yake Mwenyezi Mungu: {Enyi mlio amini! Toeni katika vile vizuri mlivyo vichuma}[ AL BAQARAH: 267]

Ushahidi wa Aya juu ya uwajibu wa Zaka, ukubwa wa fadhila yake, na kwamba ni sifa za waumini ambazo ni dhahiri, na kinachobainishwa katika mifumo ya Qur-ani ni kuunganishwa kwa Swala na Zaka pamoja. Aya zote za Qura’ni Tukufu - wengine walizihesabu Aya hizi ni themanini na mbili - ambamo Swala ilitajwa pamoja na Zaka.

Qur’ani Tukufu haikutosheka na haya tu. Pia katika Qur`ani Tukufu mwenye kukataa kutoa Zaka anatishiwa adhabu kali huko Akhera, Mwenyezi Mungu anasema: {Wala wasidhani wale ambao wanafanya ubakhili katika aliyo wapa Mwenyezi Mungu katika fadhila zake kuwa ni kheri yao. Bali hiyo ni shari kwao. Watafungwa kongwa za yale waliyo yafanyia ubakhili Siku ya Kiyama.} [AAL IMRAAN: 180]. Mwenyezi Mungu anasema pia: {Na wanao kusanya dhahabu na fedha, wala hawazitumii katika Njia ya Mwenyezi Mungu, wabashirie khabari ya adhabu iliyo chungu} [AT TAWBAH. 34].

Na katika hili ni onyo kwa nyoyo zilizoghafilika na kuzihamasisha nafsi kutoa Zaka, na kwa njia hii nafsi inaendeshwa kwa fimbo ya vitisho ili kutekeleza wajibu huo kwa hiari yake, vinginevyo itasukumwa kwake kwa fimbo ya kanuni na upanga wa Sultani kwa nguvu.

Pili: Dalili kutoka kwa Sunna:

Na tukiangalia Sunna ya Mtume (S.A.W.) tukaona kuwa Mtume (S.A.W.) akiunganisha Zaka na Swala kwa pamoja, basi huenda Jibril amezitaja nguzo za Uislamu kwa ukamilifu kama katika Hadithi ifuatayo: “Uislamu umejengwa juu ya ...”, na pengine alizitaja baadhi ya nguzo zale tu, lakini Zaka  na Swala vilikuwa daima zikiunganishwa pamoja mbele ya yale anayoamuru nayo.

Na Hadithi zinazohusu faradhi ya zaka kwa Waislamu, na onyo kali dhidi ya kuizuia ni nyingi, ikiwa ni pamoja na Hadithi ya Jibril, isemayo: “Uislamu umejengwa juu ya nguzo tano…” Hadithi hiyo ikiwa ni pamoja na:

*Imepokelewa kutoka kwa Mtume (S.A.W.) kwamba yeye alisema katika mwaka wa Hija ya kuaga: “Mwabudini Mola wenu, na Swalini Swala tano zenu, na fungeni mwezi wenu na toeni zaka ya mali yenu, na watiini wale wenye mamlaka juu yenu, ili kuingia Peponi mwa Mola wenu.”.

* Imepokelewa kutoka kwa Asma binti Abi Bakr amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (S.A.W.) aliniambia: “Toa sadaka kwa mali yako wala usizuie mali yako kwa kuhesabu (kwa kuhofia itapungua), Allah asije akakunyima rehma zake na wala usiwanyime watu kwa ile fadhila uliyopatiwa na hivyo Allah akakunyima”. Katika Hadithi nyingine: “Usikusanye Allah akakukatia riziki”

* Mtume, (S.A.W.), anasema katika Hadithi iliyopokelewa kutoka kwa Anas, (R.A): “Mtu mmoja alikuja kutoka kwa Tamim kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, (S.A.W.), na akasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, mimi nina pesa nyingi, na nina familia, watoto, na mwanamke wa sasa, basi niambie jinsi ninavyotumia pesa hizi na jinsi ninavyofanya? Mtume wa Mwenyezi Mungu (S.A.W.), akasema: Toa zaka katika fedha zako, kwani zaka ni utakaso unaokutoharisha, na unaungana na jamaa zako, na unajua haki za muombaji na jirani ambaye ni masikini”

*Katika Hadithi nyingine iliyopokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah-(R.A) kwamba: “Mtu mmoja alikuja kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (S.A.W.), akasema, Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu: Akasema Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu ni sadaka ipi ina malipo makubwa zaidi? Mtume akasema,: Ni utoe sadaka nawe umzima, na unahitajia mali bado, unahofia ufukara na unatarajia utajiri. Wala usichelewe mpaka roho ikafika kwenye koo, ukaanza kusema: fulani ana haki kadhaa na fulani ana haki kadhaa na fulani alikuwa ana haki kadhaa”.

* Mtume, (S.A.W.), anasema katika Hadithi iliyopokelewa kutoka kwa Abu Huraira-(R.A) kwamba: “Hakuna siku ambayo wanaamka asubuhi waja isipokuwa Malaika wawili huteremka mmoja wao husema Ewe ALLAH mpe badala mwenye kutoa na mwingine husema Ewe ALLAH mpe kuharibikiwa mwenye kuzuia”.

Na Hadithi nyingine zinazobainisha kwa uwazi kuwa Zaka ni moja ya nguzo za Uislamu, na nguzo mojawapo ya dini, sawa na Swala na saumu n.k, na hakuna maana ya uwajibu isipokuwa hiyo.

Tatu: Ushahidi katika makubaliano (Ijmaa):

Wanazuoni wamekubaliana kwa kauli moja juu ya dhana ya

 Zaka , na kwamba ni moja ya nguzo za Uislamu.

Nne: Ushahidi unaokubalika kiakili:

*Kutoa zaka kwa ajili ya kumsaidia mnyonge, kusaidia masikini, kuwezesha wasiojiweza, na kumtia nguvu katika kutekeleza yale aliyomuamrisha Mwenyezi Mungu Mtukufu ya tauhidi, ibada, na njia za kutimiza wajibu ni wajibu.

*Zaka inaitakasa nafsi ya mtoaji kuondosha uchafu wa madhambi, na kuitakasa maadili yake kwa tabia ya ukarimu na kuacha ubahili na dhiki, kama vile nafsi zilivyo na dhiki kwa kuhangaika na pesa, hivyo huzoea kusamehewa, na kukubali utendaji wa amana na utoaji wa haki kwa wale wanaostahiki, na yote hayo yalijumuishwa katika kauli yake Mola Mtukufu: {Chukua sadaka katika mali zao, uwasafishe na uwatakase kwazo} [AT TAWBAH: 103].

*Vile vile Mwenyezi Mungu Mtukufu alivyowaneemesha matajiri, na akawafadhilisha kwa aina za fadhila na mali zaidi ya mahitaji ya asili, na akawateua nazo ili wafurahie na maisha, na kulazimishwa kushukuru neema. Kiakili, kisheria, na kutoa Zaka kwa masikini ni jambo la kushukuru neema, hivyo ilikuwa ni wajibu.

Hukumu ya kuzuia zaka :

Wanachuoni wa Fiqhi wameafikiana kuwa mwenye kuikataa Zaka ni kafiri, na mwenye kukataa kuitoa anapigwa vita juu yake, na inachukuliwa kutoka kwake kwa nguvu, kama alivyofanya Bw. Abu Bakr As-Siddiq, na kusema juu ya Zaka ni kwa kauli moja. Ama tofauti ndani yake, kama vile Zaka ya biashara, Zaka ya matunda na mazao katika ardhi ya Kharajji, na Zaka ya fedha za wasiotozwa ushuru, mwenye kuikanusha si kafiri; kwa sababu wanachuoni wanatofautiana kuhusu ikiwa ni wajibu au la.

Matokeo ni kwamba watu katika kutoa Zaka na kuamini kuwa ni wajibu ni wa aina tatu:

* Watu wanaoamini kuwa hali ya kutoa Zaka ni wajibu na inastahiki sifa kwa Mwenyezi Mungu, nayo kauli yake Mwenyezi Mungu kuhusu hilo ni: {HAKIKA wamefanikiwa Waumini (1) Ambao ni wanyenyekevu katika Sala zao (2) Na ambao hujiepusha na mambo ya upuuzi (3) Na ambao wanatoa Zaka (4)} [AL MU'MINUN: 1-4]

*Watu wengine wanaamini kuwa hali ya kutoa Zaka ni wajibu lakini wanakataa kuilipa. Iwapo mmoja wao ni katika miliki ya mtawala, angeichukua Zaka kutoka katika mali yake kwa nguvu, au angepigana naye kama walivyofanya Maswahaba (R.A) kwa wanakataa kutoa Zaka.

* Wengine hawaamini kuwa kutoa zaka ni wajibu, Ikiwa mtu huyo ni miongoni mwa wasiojua hivyo kwa sababu ya kusilimu kwake hivi karibuni, basi afahamishwe - yaani ni wajibu, na ni haramu kurudia hali hiyo ya kukataa kutoa zaka, vinginevyo atahukumiwa kuwa ni kafiri.

Dakta Yusuf Al-Qaradhawi anasema katika kitabu chake “Fiqhi Az-Zaka”: “Jambo muhimu baada ya hapo ni kujua kwamba zaka ni miongoni mwa mambo yanayojulikana katika dini kwa ulazima, nayo ni moja ya nguzo za Uislamu, hupitishwa hivyo kwa watu wote, uwajibu wake unathibitishwa na Aya za Qur'ani Tukufu zilizo wazi na zinazojirudiarudia, na kwa Sunna ya Mtume iliyopokelewa na wengi isiyo na shaka, na Makubaliano ya umma mzima, kizazi baada ya kizazi... Wanachuoni waliamua kwamba anayeikanusha ufaradhi wake amekufuru na ametoka katika Uislamu, na kwa hukumu hii ya kisheria iliyo wazi na yenye kauli moja, tunaujua msimamo wa wale wanaoudharau uzito wa zaka, na kutangaza waziwazi kuwa haifai zama hizi, na wao ni Waislamu waliokulia katika nchi za Uislamu”

Tatu, Zaka  kwenye hisa

Kwanza: ufafanuzi wa hisa:

Ufafanuzi wa hisa katika lugha:

Hisa: ni sehemu ya pesa au mali

Ufafanuzi wa hisa katika istilahi:

Hisa ni aina mojawapo ya dhamana ambamo shughuli za kibiashara hufanyika, na mgawanyiko wake ni ule unaojulikana kama “dhamana.” Hisa hufafanuliwa kama: “Hati Fungani ya thamani sawa, inayoweza kujadiliwa kwa njia za kibiashara, ambapo haki ya mwenyehisa katika kampuni inawakilishwa, hasa haki yake ya kupata faida”.

Dkt. Al-Qaradhawi ameifafanua hisa kuwa: “Haki za umiliki wa sehemu kwa mtaji mkubwa wa makampuni ya hisa za pamoja au ubia na hisa, na kila hisa ni sehemu ya sehemu sawa za mtaji” ().

Hisa, basi, inawakilisha hisa zinazotolewa na washirika wakati wa kuchangia mradi wa kampuni, na mtaji huundwa kutoka kwa hisa hizi, iwe kwa pesa taslimu au mali.

Aina za Hisa:

Hisa hutofautiana kwa aina nyingi:

* Hisa zinagawanywa kulingana na hisa inayolipwa na mshirika katika hisa za bidhaa, hisa za pesa taslimu, na hisa za msingi.

Hisa za pesa taslimu ni hisa zinazomilikiwa na wamiliki wao baada ya kulipa thamani yao kwa fedha taslimu, kwa vile zinawakilisha hisa za fedha taslimu katika mtaji wa kampuni ya pamoja ya hisa, na angalau robo ya thamani yao ya kawaida lazima ilipwe kwa kuanzishwa kwa kampuni, sharti kwamba thamani ya kawaida hulipwa kikamilifu ndani ya muda usiozidi miaka kumi kutoka tarehe ya kuanzishwa kwa kampuni.

Hisa za bidhaa huwakilisha hisa za bidhaa katika mtaji wa kampuni, na hisa hizi ziko chini ya sheria zilezile zinazotumika kwa hisa za pesa taslimu.

Hisa za mwasisi ni haki katika sehemu ya faida iliyopatikana na kampuni, na hazina thamani ya kawaida, na hutolewa kwa ajili ya uvumbuzi au makubaliano kutoka kwa serikali. Hisa hizi zinauzwa kwenye soko la hisa kwa misingi ya sehemu yake halisi ya faida.

* Hisa zinagawanywa kulingana na suala la fomu katika hisa za kawaida, hisa za wamiliki, na hisa za agizo.

Hisa za kawaida ni zile zinazobeba jina la mmiliki wake, na umiliki wake unathibitishwa kwa kusajili jina la mbia kwenye rejista ya kampuni.

Hisa za wamiliki ni zile ambazo hazina jina la mmiliki wake, lakini zinasema kuwa hisa ni kwa mmiliki wake, au mbia anayechukuliwa kuwa mmiliki machoni pa kampuni, kwa hivyo umiliki wake unakuwa ushahidi wa umiliki huu.

Hisa za agizo ni hisa zinazojumuisha kifungu cha maneno (kwa agizo) na husambazwa kwa njia za uidhinishaji, kama vile dhamana zote zilizo na masharti ya agizo, nazo ni nadra, bali ni chini kuliko hisa za mhusika pamoja na uhaba wa aina ya mwisho.

* Hisa zinatofautiana kulingana na haki za wenyehisa kwa hisa za kawaida, hisa za upendeleo, na hisa zenye kura nyingi.

Hisa za kawaida ni zile ambazo ni sawa kwa thamani, na zinawapa wenyehisa haki sawa, kwani wanampa mmiliki wake haki zinazopatikana kwa mbia bila upendeleo wowote.

Hisa za upendeleo ni zile hisa zinazowapa wamiliki wake haki ya kupata kipaumbele katika kupokea faida fulani, au kipaumbele katika kurejesha kile kilicholipwa kutoka kwa mtaji baada ya kufilisiwa, au kipaumbele katika masuala yote mawili, au faida nyingine yoyote ambayo haipatikani kwa wamiliki wa hisa za kawaida.

Hisa zenye kura nyingi ni zile zinazompa mmiliki wake kura zaidi ya moja katika mikusanyiko mikuu.

* Hisa hutofautiana kulingana na mzunguko au la, kwa hisa za dhamana, na hisa za mzunguko

Hisa za dhamana ni hisa zisizoweza kuuzwa zinazowasilishwa na mjumbe wa bodi ya wakurugenzi wa kampuni ya hisa ili kuhakikisha usimamizi wake, na hisa hizo haziwezi kuuzwa hadi muda wa wakala wa mwanachama uishe, naye ndiye apitishe bajeti ya mwaka wa fedha uliopita ambao alifanya kazi yake.

Hisa za mzunguko ni zile zinazojumuisha hisa zote isipokuwa hisa za dhamana. Inaruhusiwa kuuzwa kwa hisa katika kununua na kuuza kwa mujibu wa mifumo ya biashara.

Tabia za Hisa:

Hisa za kampuni zina sifa zinazotofautiana na hisa nyingine, na zinaweza kufupishwa kama ifuatavyo:

* Thamani ya hisa ni sawa, ambapo hisa za makampuni lazima ziwe sawa kwa thamani, kwa pamoja, zinaunda mtaji wa kampuni, na baadhi ya sheria za kibiashara zimeweka kikomo cha juu na cha chini cha thamani ya hisa inayotajwa kutolewa, na lengo ni kuwezesha uendeshaji wa kampuni, kuwezesha usambazaji wa faida, kuwezesha tathmini ya wengi katika makusanyiko ya jumla ya kampuni, na kudhibiti bei ya hisa katika soko la hisa.

* Majukumu ya wabia ni sawa, yaani majukumu wa wabia hugawanywa miongoni mwao kulingana na thamani ya hisa, hivyo haihusiki na deni la kampuni isipokuwa kwa mujibu wa hisa anazomiliki, bila kujali kiasi ya madeni au hasara ya kampuni.

* Kutogawanyika kwa hisa, yaani wamiliki wa hisa wanaweza wasiwe wengi mbele ya kampuni, kwa hivyo ikiwa umiliki wa hisa utahamishiwa kwa zaidi ya mtu mmoja kwa sababu ya urithi au zawadi, basi mgawanyiko huu, hata ikiwa ni halali kati yao, haikubaliki kwa kampuni, na lazima wamchague mtu anayewawakilisha kwenye kampuni.

Labda faida ya kutogawanya hisa ni kuwezesha utekelezaji wa haki na utekelezaji wa majukumu ya pande zote kati ya mbia na kampuni.

* Hisa inaweza kuuzwa, na maana yake ni uhamishaji wa umiliki wake kutoka kwa mtu mmoja hadi kwa mwingine, na mzunguko huu unachukuliwa kuwa moja ya sifa muhimu za kampuni za pamoja. Badala yake, mzunguko ni kigezo kinachokubalika zaidi cha kutofautisha kati ya ubia na Makampuni ya mitaji, ili kwamba ikiwa imeainishwa katika vifungu vya ushirika vya kampuni au uamuzi utolewe na mkutano mkuu wa wanahisa ambao ni pamoja na kukataza kusamehewa kwa hisa, basi kampuni inapoteza hadhi yake kama kampuni ya hisa na kuwa ubia wa watu, na hisa zinasambazwa kupitia usajili wa umma.

 

Jinsi ya kulipa Zaka ya Hisa:

Fiqhi ya kisasa iligawanywa katika maoni matatu juu ya jinsi ya kulipa Zaka  ya hisa, kama ifuatavyo:

Maoni ya kwanza: Kwamba Makampuni ya hisa yatende kama yanavyowatendea watu binafsi katika Zaka, kwa maana ya kwamba kampuni hiyo inalipa Zaka ya hisa zake zilizowakilishwa katika fedha ilizonazo, kama vile mtu mmoja anavyotoa Zaka ya pesa yake, na Zaka  imewekwa juu yake kwa kuzingatia aina ya pesa, na kwa mujibu wa kiwango, na kiasi cha wajibu.

Na ikiwa kampuni haitoi Zaka katika pesa zake kwa sababu yoyote ile, basi wanahisa lazima watoe Zaka katika hisa hizo. Ikiwa mbia anajua Zaka inahusika na fungu lake, basi anatoa Zaka katika hisa zake kwa kuzingatia hivyo, na ikiwa hajui, basi ikiwa alichangia katika kampuni kwa nia ya kufaidika na mapato ya hisa, basi hakuna Zaka juu ya sehemu ya asili, lakini badala yake hutoa Zaka juu ya mapato yake, na wajibu ni robo ya kumi. Na kama alipata hisa kwa nia ya kufanya biashara, basi anatoa Zaka juu yake kama bidhaa ya biashara, yaani (2.5%), na hivi ndivyo Baraza la Kiislamu la Fiqh ilichoamua katika kikao chake cha nne cha kongamano lililofanyika Jeddah, iliamuliwa na kongamano la kwanza la Zaka  la Baitu Al-Mal, na akaona hivyo pia Prof. Al-Sadik Al-Dariir.

Inaonekana kwamba usemi huu ulitegemea kile Imamu Shafi alichosema katika kitabu cha Al-Jadid, kwamba mchanganyiko huo unaathiri fedha zote za Zaka, kinyume na wanachuoni wa umma, ilielezwa katika matini ya uamuzi wa Baraza la Fiqh: “Hii inatokana na kanuni ya mchanganyiko miongoni mwa Wanachuoni wa Fiqhi walioijumlisha katika fedha zote,” yaani, Imamu Shafi katika kitabu cha Al-Jadid.

Rai ya pili: Hisa hizi zipendekezwe kulingana na aina ya shughuli ya Kampuni iliyozitoa, kwa hivyo hisa haitolewi hukumu isipokuwa baada ya kujua Kampuni inayowakilisha sehemu ya mtaji wake, na kwa hivyo inaamuliwa kuipendekeza au la. Kuna tofauti kati ya hisa za Makampuni ya viwanda ambayo hayafanyi kazi za kibiashara, kama Makampuni ya nguo, magazeti, migahawa...na mengineyo, na kati ya Makampuni yanayofanya shughuli za kibiashara kama vile Makampuni ya kuagiza na kuuza nje, na usafirishaji wa bidhaa na abiria.

Makampuni ya viwanda hayalazimiki kutoa Zaka katika hisa zao isipokuwa faida yanayoizalisha inayoongezwa kwenye fedha nyingine za mwenyehisa, na hulipa Zaka pamoja na Zaka ya pesa baada ya kupita kwa mwaka mmoja juu yake na kiwango kimekamilika na kufikiwa.

Makampuni ya kibiashara lazima yalipe Zaka  kwenye hisa zake, kama vile Zaka  ya aina za mali za biashara, yaani robo ya kumi (2.5%) ya thamani ya soko pamoja na faida, ikiwa mali na faida zikifikia kiwango, au zimekamilishwa na kile mmiliki anacho, baada ya kutoa thamani ya majengo, mitambo na zana zinazomilikiwa na kampuni, Rai hii inawakilishwa waheshimiwa: Sheikh / Abd Al-Rahman Issa, Profesa / Wahba Al-Zuhaili, na Sheikh Abdullah Al-Bassam.

Walitoa dalili juu ya hivyo kama ifuatayo:

* Thamani ya Hisa za Makampuni ya viwanda huwekwa kwenye mitambo na zana, na inajulikana kuwa mtaji wa fedha zenye faida - yaani, zisizo za kibiashara - kwa ujumla, hakuna Zaka juu yake, wala juu ya mtaji na faida kwa pamoja kama mali ya biashara, wala juu ya mazao na mapato kama vile vilivyobakia kutoka katika ardhi ya kilimo, isipokuwa imebakia kutoka humo kitu na mwaka umepita, na huu ndio msingi wa kutofautisha kati ya hisa za Makampuni ya viwanda na hisa za Makampuni ya kibiashara.

*Faida ya kampuni si chochote ila ni matunda ya kutumia zana hizo, na mitambo ya Makampuni ya viwanda hupungua asili na thamani kwa ajili ya faida hii, na sababu ya Zaka ni za kiwango kinachokua, na zana hizi hazikui, lakini zinapungua, kwa hivyo zaka haifai kwake.

Rai ya tatu: Kuzingatia hisa za Makampuni kama aina za mali za biashara, iwe shughuli za Makampuni haya ya viwandani au ya kibiashara, kwa hivyo hisa za kila aina huchukuliwa kuwa aina za mali za biashara, Zaka  inalipwa kwa thamani ya soko lake robo ya moja ya kumi (2.5%) pamoja na faida, na hivi ndivyo watu watukufu walivyoona kama: Sheikh / Muhammad Abu Zahra, Dkt. Yusef Al-Qaradhawi, Dkt. Sami Hammoud, Sheikh Abd al-Rahman Al-Hilu, Dkt. Muhammad Omair Al-Zubair, na Sheikh Rajab Bayoud Al-Tamimi.

Walitoa dalili kama ifuatayo:

* Hisa ni pesa ambazo zimechukuliwa kwa biashara, kwa sababu alizokuwa nazo anazifanyia biashara kwa kuzinunua na kuziuza, na anapata kutokana nazo kama kila mfanyabiashara anavyopata kutokana na bidhaa yake, na thamani yake halisi inayokadiriwa sokoni inatofautiana katika kuuza na kununua kutokana na thamani yake ya kawaida, kwa kuzingatia hili, ni moja ya aina za mali za biashara, kwa hivyo ilistahiki kuwa chombo kitolewe Zaka kama mali zote za biashara, na imebainishwa ndani yake kile kinachozingatiwa katika matoleo ya biashara.

*Sababu ya Zaka katika mali ni ukuaji wake, kwa hivyo Zaka ni wajibu kwa kila kinachopatikana kwa ukuaji na utumiaji, kwa Makampuni ya viwanda - kwa mfano - mtaji wake ni mitambo na zana hizi, kwa hivyo haziwezi kulinganishwa na zana za seremala na mhunzi anayefanya kazi kwa mkono wake, kwa hivyo Zaka inatakiwa juu ya zana hizi kwani ni mali zinazoongezeka, na ukweli kwamba Wanachuoni wa Fiqhi hawakuweka Zaka kwenye zana za viwanda katika zama zao kwa sababu zilikuwa nyenzo za msingi, kwa hivyo hazikuzingatiwa kuwa ni mali zinazoongezeka na zenye tija peke yake, tofauti na zana za viwandani hivi sasa.

Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye Kuafikisha kwa Ayapendao na kuyaridhia.

Share this:

Related Fatwas