Nadharia ya dini mbadala

Egypt's Dar Al-Ifta

Nadharia ya dini mbadala

Question

Ni nini alama za mikondo ya ukufurishaji kufuata mafunzo yasiyo endana na mafunzo ya dini ya kiislamu?

Answer

Kwa hakika Uislamu ni dini inayosimamisha uhusiano mzuri kati ya mja na Mola wake, na ni elimu iliyo na vyanzo vyake na marejeleo yake, ambapo hunukuliwa na misingi yake kupitia wataalamu wake wabobezi, na miongoni mwa sifa zake kuu ni kwamba inazingatiwa na watu wake husika.

Pengine mtu kushindwa kujifunza dini kwa masharti na vidhibiti hivyo na kugeuka kwa kutumia njia mbadala akijikinaisha kuwa anajifunza, mbinu ambayo magaidi wanaifauata, ambapo makundi ya kigaidi yanajaribu kugundua njia mbadala mbali na njia sahihi ya ukati na kati ya dini inayokubaliwa na umma katika karne nyingi zilizopita kuhusu uelewa na mtindo wa kuhakikisha pamoja na wataalamu wake na namna za kuwafundisha, zaidi ya hayo kuachana na maoni makuu ya Maimamu na badala yake kufuata maoni finyu, hali inajulikana kwa dini potofu au dini ya kidhana, na hiyo ndiyo dini mbadala ambapo mtu au kundi huunda mfumo mzima wa dini ukijumuisha vyanzo, marejeleo na misingi yao mbadala, nayo ni nadharia inayokua kwa kupita kwa wakati na vizazi mpaka igeuke kuwa sababu ya kutofautiana na kuzozana mwishowe kupotea kabisa. Mfano wa hali ni kama mtu anayesimama mbele ya kioo akaona picha yake na kudhani kuwa picha ndiyo asili kutokana na dhana inayomtawala, ambapo picha inayoonekana katika kioo siyo asili kama anavyodhani, bali ni picha.

Kwa hiyo, dini mbadala au dini ya kidhana huashiria hali ya kuifanya dini ambayo ni ibada maalumu ni sawa sawa na vitendo vya nje na kumhukumu anayewajibika navyo kuwa muumini na kwamba yeye ndiye mkweli, ilhali wengine ni wapotofu, jambo ambalo huwagawanya waumini katika mafungu mawili; Waislamu wanaotekeleza ibada ipasavyo, na kwa upande mwingine, wale ambao hushikilia ibada ambazo humfanya mmoja wao ahukumiwe Uislamu kwa kushikamana nao.

Share this:

Related Fatwas