kutoa Mimba Kabla ya Siku 120
Question
Ni nini hukumu ya kisheria kuhusu kutoa mimba? Mke wangu amebeba mimba kwa siku 32, ambapo daktari ameonya kwamba ikiwa mimba itaendelea, kutakuwa na hatari kwa afya ya mama. Hapa chini kuna ripoti ya kitabibu iliyoambatanishwa:
Baada ya kufanya uchunguzi wa kitabibu kwa muhusika, na kupitia picha za uchunguzi wa mionzi ya Magnetic Resonance Imaging (MRI), ilionekana kwamba ana maumivu makali katika maeneo ya chini ya mgongo na shingo kutokana na kuwepo kwa matatizo ya diski za uti wa mgongo katika maeneo (L3-L4) na (L5-S1), na pia kuonekana kwa uvimbe kwenye uti wa mgongo. Anahitaji matibabu ya dawa na mapumziko kamili; jambo ambalo linahitaji kuzuia mimba kutokea au kuzaa wakati wa kipindi cha matibabu, kwa sababu ya hatari ya athari kwa afya yake na uwezekano wa kupata matatizo makubwa kiafya, na pia hatari ya dawa ambazo hawezi kuacha kutumia kipindi hicho kwa mtoto aliye tumboni na madhara yanayoweza kumtokea kutokana na matumizi ya dawa za kupunguza maumivu.3].
Answer
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na rehma na amani zimwendee bwana wetu Mtume wa Mwenyezi Mungu, jamaa zake, Maswahaba wake na wanaomfuata. Na baada ya hayo:
Wanazuoni wamekubaliana kwamba ikiwa umri wa mtoto tumboni umefika siku mia moja na ishirini (120) -ambapo roho huingizwa katika mwili wa mtoto- basi haiwezi kuruhusiwa kuondolewa mimba, na inaharamishwa kutoa mimba kabisa katika hali hii; kwa sababu hiyo inachukuliwa kuwa ni kuua nafsi, ambayo Mwenyezi Mungu ameiharamisha kuuawa isipokuwa kwa haki, kama anavyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu katika Qur'ani Tukufu: {Wala msiwauwe watoto wenu kwa sababu ya umasikini. Sisi tunakuruzukuni nyinyi na wao} [Al An`am151] Na pia anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu katika Qur'ani Tukufu: {Wala msiuwe nafsi ambayo Mwenyezi Mungu amekataza isipo kuwa kwa haki} [Al Israa 33].
Hata hivyo, ikiwa umri wa mtoto tumboni haujafika siku mia moja na ishirini (120), kuna tofauti ya maoni miongoni mwa Wanazuoni kuhusu hukumu ya kutoa mimba. Baadhi yao wamesema ni haramu, na hii ni kauli inayokubalika zaidi kwa Madhehebu ya Maliki, Dhahiriya na baadhi ya Shafi. Wengine wamesema ni huchukiza -isiyopendekezwa -(makruhu) kabisa, na hii ni kauli ya baadhi ya Hanafi na Maliki na maoni yanayowezekana miongoni mwa Shafii. Baadhi ya wengine wamesema ni halali kwa ajili ya udhuru tu, na hii ni kauli halisi ya Madhehebu ya Hanafi. Wengine wamesema ni halali kabisa, na hii ni kauli ya baadhi ya Hanafi na maoni miongoni mwa Hanbali na Ramli Shafi ikiwa mbegu ya mtoto imekuwa kutokana na zinaa, na pia alisema hivyo Lakhmi kutoka kwa Maliki na Abu Ishaq Al-Marozi kutoka kwa Shafi kabla ya siku arobaini.
Kauli yenye nguvu na iliyochaguliwa kwa ajili ya Fatwa ni kwamba kutoa mimba hakujuzu kabla ya kupulizwa roho isipokuwa kama mimba hiyo imetokana na uzinifu, au kwa sababu ya udhuru; kama ilivyo kweli katika Madhehebu ya Hanafi, na Ibn 'Abidin amepokea katika Hashiya yake kutoka kwa Ibn Wahban kwamba miongoni mwa udhuru ni mama kukosa maziwa baada ya mimba kuonekana na baba wa mtoto hana uwezo wa kumwajiri mnyonyeshaji — yaani mlezi — na ikahofiwa kufa kwake, akasema: basi ruhusa ya kutoa mimba inabebwa juu ya hali ya udhuru.[1]
Pia alikumbusha Imamu al-Zarkashi kuwa ikiwa mama atahitaji kunywa dawa inayoruhusiwa ambayo itasababisha kutoa mimba, basi ni haki yake kutokuwa na dhima kwa sababu hiyo.[2]
Na kwa msingi huu, katika tukio hili na kwa mujibu wa ripoti ya daktari inayosema kuwa kuendelea kwa mimba kunahatarisha afya ya mama, na kwa vile mtoto bado hajafikia siku mia moja na ishirini (120), basi inaruhusiwa kufanya utoaji wa mimba katika hali hii; kwa mujibu wa maoni/rai ya baadhi ya wanazuoni waliokubali utoaji wa mimba katika kipindi hiki kwa ajili ya udhuru. Hakuna pingamizi kwa neno la kisheria katika jambo hili.
Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ni Mjuzi Zaidi.
[1] Rad Mukhtar Ala dar Mukhtar, 3/193.
[2] Al iqna`a Bihashiyat Al bujayrimy 4/129.
Arabic
Englsh
French
Deutsch
Urdu
Pashto
Hausa
