Kuchora Tattoo
Question
Ni ipi hukumu ya kujichora tattoo[1] [2]?
[1] "Kuchora tatoo": Hujumuisha michoro na mifumo mwilini, kwa kuingiza sindano au kitu kama hicho kwenye ngozi ili kutoa damu na kuingiza rangi za rangi ili kutoa umbo fulani.
[2] "Tattoo":Inayotumiwa na baadhi ya wanawake kwa ajili ya mapambo, kama vile kubainisha jicho badala ya kutumia wanja au kuchora nyusi, au kutengeneza michoro inayoonekana kwenye ngozi kwa kutumia rangi zinazotoweka baada ya muda mfupi na hazichukui umbo la kudumu.
Answer
Miongoni mwa aina za mapambo ambayo mwanamke hujipamba kwayo ni yale yanayojulikana kama tattoo, nayo ni ya aina mbili:
Aina ya kwanza: tattoo yenye kudumu; nayo ni michoro na mapambo / nakshi inayowekwa juu ya mwili kwa kuchoma ngozi kwa sindano au mfano wake ili kutoa damu na kuingiza rangi mbalimbali zinazotoa umbo fulani. Aina hii imeharamishwa kisharia, kwa sababu ina madhara kwa binadamu, na husababisha unajisi katika sehemu iliyochorwa kutokana na damu iliyochanganyika na rangi.
Aina ya pili: tattoo ya muda; nayo ni kuchora michoro ya juu juu, juu ya ngozi kwa kutumia rangi zinazofutika baada ya muda mfupi, na hazidumu. Aina hii ya pambo inafaa, kwa kuwa inafanana na kujipaka hina ambayo inaruhusiwa kisharia.
Maelezo
Uislamu umehalalisha kujipamba na kujiremba; Mwenyezi Mungu amesema: {Sema: Ni nani aliyeharamisha pambo la Mwenyezi Mungu alilolitoa kwa waja wake} [Al-A‘raf: 32].
Na katika Hadithi, Mtume (S.A.W) amesema: “Hakika Mwenyezi Mungu ni Mzuri na anapenda uzuri.” Imepokewa na Muslim.
Miongoni mwa mapambo ambayo mwanamke hujipamba nayo ni yale yanayojulikana kama tattoo, nayo ni ya aina mbili:
Aina ya kwanza: Tattoo yenye kudumu:
Nayo ni miongoni mwa mapambo ambayo Sharia tukufu imeyaharimisha, kwa sababu yana madhara kwa binadamu. Imepokewa kutoka kwa ‘Abdullah bin Mas‘ud (R.A) amesema: (Mungu na amewalaani[1] wale wanaochora tattoo na wale wanaochorwa tattoo, wale wanaochora nyusi zao na wale wanaong'olewa nyusi zao, na wale wanaochora meno yao kwa uzuri, wale wanaobadilisha uumbaji wa Mungu. Alisema: Hii ilimfikia mwanamke kutoka kabila la Asad aitwaye Umm Ya'qub, ambaye alikuwa akisoma Qur`ani Tukufu, kwa hivyo akamwendea na kusema: Ni Hadithi gani hii niliyosikia kutoka kwako, kwamba umewalaani wale wanaochora tattoo na wale wanaochorwa tattoo, wale wanaochora nyusi zao, na wale wanaochora meno yao kwa uzuri, wale wanaobadilisha uumbaji wa Mungu? Abdullah akasema: Kwa nini nisimlaani yule ambaye Mtume wa Mwenyezi Mungu kamlaani? Hali ya kuwa imo katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu." Mwanamke akasema: "Nimesoma kilicho kati ya jalada mbili za Qur`ani Tukufu na sikukipata." Akasema: "Kama ungelisoma, ungelikipata (ugelikiona). Mwenyezi Mungu (Mwenyezi Mungu awe radhi naye) akasema: {Na chochote alichokupeni Mtume – kichukueni, na alichokukatazeni basi kiepukeni."} [Al-Hashr: 7] (Imepokewa na Muslim).”
Hadithi hii inaonesha kuwa tattoo ya kudumu kwa kuchoma kwa sindano ni haramu; kwa sababu laana haiji ila juu ya jambo lililoharamishwa kisharia.
Wanazuoni wametaja sababu za kuharamishwa kwa tattoo kwa njia hii, miongoni mwazo ni:
Kwanza: Husababisha unajisi katika sehemu iliyochorwa kutokana na damu iliyochanganyika na rangi.
Pili: Athari ya kudumu ya tattoo husababisha udanganyifu na kubadilisha maumbile ya Mwenyezi Mungu, kama ilivyokuja katika matini ya hadithi iliyotajwa: “wanaobadilisha maumbile ya Mwenyezi Mungu”, na kama ilivyokuja katika kauli ya Mwenyezi Mungu kwa ulimi wa Shetani: {Na nitawapoteza, na nitawatia matumaini ya uongo, na nitawaamuru wakate masikio ya mifugo, na nitawaamuru wabadilishe maumbile ya Mwenyezi Mungu. Na anayemchukua Shetani kuwa mlinzi badala ya Mwenyezi Mungu basi amepata hasara iliyo wazi} [An-Nisa: 119].
Tatu: tattoo huumiza mwili kwa kuchoma sindano, na kuchoma sindano ni madhara kwa binadamu pasipo dharura. Kisharia imeharamishwa kujidhuru au kumdhuru mwingine; Mwenyezi Mungu amesema: {Wala msijitie kwa mikono yenu katika maangamizi} [Al-Baqarah: 195]. Na amesema: {Wala msiuue nafsi zenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kurehemu kwenu} [An-Nisa: 29]. Aya hizi mbili zimekataza kujidhuru na kujitia katika maangamizi, na zimeamrisha kuilinda nafsi kutokana na hatari na madhara. Miongoni mwa makusudio ya Sharia ya Kiislamu ni kulinda nafsi; kwa sababu hiyo Mwenyezi Mungu ameharamisha kila kinachosababisha kuangamiza binadamu au sehemu yake[2].
Aina ya pili: Tattoo ya muda
Aina hii imejitokeza hivi karibuni na imejulikana kwa jina la “tattoo”, nayo ni miongoni mwa mapambo yanayoruhusiwa kisharia[3]. Aina hii ya tattoo hufanywa kwa moja ya njia mbili:
Njia ya kwanza: Kutumia chombo maalumu cha kuchorea ambacho hakisababishi damu kutoka.
Njia ya pili: kuweka stika juu ya mwili yenye mchoro au umbo maalumu, nayo huchapishwa juu ya ngozi kwa muda fulani, kisha hufutika kwa kupita muda na kwa kutumia maji.
Aina hii ya pambo inafaa na kujuzu wala haina madhara, kwani inafanana na kujipaka hina[4] ambayo inaruhusiwa kisharia.
Tunapata faida kutokana na yaliyotangulia:
Tattoo iliyokatazwa kisharia ni ile inayohusisha kuchoma sindano ndani ya ngozi ya binadamu na kuijaza rangi na mapambo, pamoja na kuchanganyika kwa hilo na damu inayotoka.
Inajuzu kisharia kujipamba kwa kinachojulikana hivi sasa kwa jina la “tattoo” ambayo ni ya kuchora au kupamba juu ya tabaka la nje la ngozi, haifiki kwenye damu na hufutika baada ya muda mfupi; kwa kuwa inafanana na kujipaka hina ambayo inaruhusiwa kisharia.
[1] "Laana": ni kustahili kufukuzwa kutoka kwa rehema ya Mungu Mwenyezi.
[2] Al-Jāmi‘ li-Aḥkām al-Qur’ān cha Al-Qurṭubī (juzuu 5, ukurasa 393), na Sharḥ An-Nawawī ‘alā Muslim (juzuu 14, ukurasa 106).
[3] Inayokubalika kisheria.
[4] kupaka ngozi ya mwanadamu kwa rangi ya hina.
Arabic
Englsh
French
Deutsch
Urdu
Pashto
Hausa
