Wanawake na wanaume kufanya kazi sehemu moja
Question
Je, inaruhusiwa kwangu kufanya kazi sehemu ambapo wanaume na wanawake hufanya kazi pamoja? Mume wangu ameniambia kwamba sehemu ya kazi ya mchanganyiko huchukuliwa kuwa faragha na kwa hivyo ni haramu.
Answer
Hakuna kizuizi kisharia kufanya kazi katika sehemu moja yenye wanawake na wanaume, iwapo watazingatia mipaka ya kisharia. Kwa kuwa mahali pa kazi pa wazi si katika khalwa (faragha iliyoharamishwa).
Kinachotupa faida kutokana na Hadithi hizi mbili ni: inajuzu kuzungumza na mwanamke na kumuuliza mambo yenye manufaa, iwapo kuna usalama dhidi ya fitna, pamoja na kuzingatia wajibu wa kujisitiri (stara).
Na kwamba uharamu wa kuwepo wanaume pamoja na wanawake hauko katika uwepo wao tu, bali huwa katika hali ya kijamii inapokuwa inakwenda kinyume na sharia tukufu; kama vile wanawake kuonesha yale ambayo si halali kwao kuyaonesha kisharia, au mkusanyiko kuwa juu ya maasi, au kuwepo kwa khalwa (faragha iliyoharamishwa).
Maelezo
Msimamo wa Waislamu, wa zamani na wa sasa, ni kwamba uwepo tu wa wanawake na wanaume sehemu moja si haramu, na kwamba Uharamu unakuwa tu katika mazingira ya kijamii ikiwa ni kinyume na Sharia ya Kiislamu, kama vile wanawake wanapoonesha kile wasichoruhusiwa kuonesha kulingana na Sharia ya Kiislamu, au mkusanyiko huo ni kwa lengo la maovu, au kunapokuwepo na faragha iliyoharamishwa.
Wanazuoni wamesema kwamba kile kilichoharamishwa chenyewe ni mgusano wa kimwili na ukaribu, si tu kukusanyika kwa wanaume na wanawake sehemu moja, hili limeelezwa na Hadithi Tukufu, imepokewa kutoka kwa Sahl bin Sa'd Al-Sa'idi R.A. amesema: "Wakati Abu Asid Al-Sa'idi alipofanya sherehe ya harusi, alimwalika Mtume (S.A.W.) na Masahaba zake, lakini hakuwatayarishia chakula wala hakukileta kwao isipokuwa mke wake, Umm Asid." Imepokewa na Bukhari.
Maana ya Hadithi inaashiria kwamba kutenganishwa kwa wanawake na wanaume kwa upande wa sehemu na mwingiliano wa moja kwa moja si lazima kwa wanawake, bali ni maalumu kwa wake za Mtume (S.A.W.) kwa kufuata kauli ya Mwenyezi Mungu: {Na mnapowauliza wakeze haja waulizeni nyuma ya mapazia } [Al-Ahzab: 53].
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraira (R.A) katika kisa cha Abu Talha Al-Ansari (R.A). kumlisha mgeni wake: "Basi walijifanya wanakula, lakini walienda kulala wakiwa na njaa." Imepokewa na Bukhari.
Maana dhahiri ya Hadithi ni kwamba walikusanyika katika sahani moja, na Mtume (S.A.W.) akawaambia: "Mwenyezi Mungu Amependa jinsi mlivyomtendea mgeni wenu usiku wa leo." Na Aya ifuatayo iliteremshwa kuhusu wao: {bali wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji} [Al-Hashr: 9].
Kinachoweza kueleweka kutoka katika Hadithi hii ni kwamba inaruhusiwa kuongea na wanawake na kuwauliza maswali ambayo ni kwa masilahi ya umma, mradi tu hakuna hatari ya fitina na kuzingatia kilichowajibu kusitiriwa.
Kuhusu kazi ambazo zinahitaji wanaume na wanawake kuwa sehemu moja, hakuna madhara katika hilo ikiwa hakuna hofu ya fitina na hawako peke yao, kuwepo tu kwa wanaume na wanawake sehemu moja si haramu kwa jinsi hiyo, kinachokuwa haramu ni mwanaume kuwa peke yake na mwanamke sehemu ambapo hakuna mtu mwingine anayeweza kuingia, Hivyo basi, si kila hali ya kuwa pamoja peke yao inachukuliwa kuwa faragha iliyoharamishwa.
Imepokewa kutoka kwa Anas bin Malik (R.A) amesema: "Alikuja Mwanamke mmoja katika wanawake wa Madina kwa Mtume (S.A.W) na akakaa naye faragha, kisha akasema: naapa kwa Mwenyezi Mungu, hakika nyinyi ndio watu ninaowapenda zaidi.'" Imepokelewa na Bukhary na Muslim.
Katika baadhi ya riwaya: "Akakaa naye faragha katika baadhi ya njia au katika baadhi ya vichochoro," ikimaanisha kwamba alikaa naye kando ambapo wale waliokuwa naye hawakuweza kusikia maneno yake au malalamiko yake kwake. Faragha hapa inamaanisha faragha ya sauti na mazungumzo, ikimaanisha kwamba alimuuliza swali mbele ya watu, na haikuwa kujitenga kamili kunakokatazwa.
Inaonekana kutoka katika Hadithi kwamba kuzungumza na mwanamke asiye maharamu kwa siri hakupunguzi dini na taqwa ya mtu pale ambapo hakuna hofu ya fitina. Kwa mfano, kufunga tu mlango kati ya mwanamume na mwanamke kwa njia ambayo inamruhusu yeyote kuufungua na kuingia wakati wowote hakufanyi kuwa ni faragha iliyoharamishwa.
Tunapata faida kutokana na yaliyotangulia:
Ni kwamba hakuna pingamizi kufanya kazi sehemu ambapo kuna wanawake na wanaume, mradi tu vidhibiti vya Sharia vizingatiwe, na sehemu ya kazi hakuchukuliwi kuwa sehemu ya faragha iliyoharamishwa.
Arabic
Englsh
French
Deutsch
Urdu
Pashto
Hausa
