Zulia ya Kufundisha watoto Jinsi ya...

Egypt's Dar Al-Ifta

Zulia ya Kufundisha watoto Jinsi ya Kuswali

Question

 Hukumu nini ya Kiislamu inayohusiana na mradi wa utengenezaji wa zulia la kufundisha watoto jinsi ya kuswali?

Answer

 Sifa zote njema ni za Allah pekee, na swala na salaam ziwe juu ya Bwana wetu Muhammad Mtume wa Mwenyezi Mungu, na pia juu ya jamaa zake na maswahaba zake, na juu ya wale wanaowafuata kwa wema mpaka Siku ya Malipo.
Baada ya kusoma ombi lililotajwa hapo juu na CD inayoambatana nayo, ambayo ina filamu fupi kuhusu Swala ya Adhuhuri kama mfano wa ile programu inayooneshwa kwenye skrini iliyoambatanishwa na zulia, na vile vile karatasi zilizoambatishwa na Fatwa na ambazo zenye maelezo ya Swala kulingana na kila madhehebu za Sunni, tunaripoti yafuatayo:
Kuhusu asili ya wazo la mradi iliyouliziwa, ambayo ni kuonesha vitendo vya Swala kupitia skrini iliyoambatanishwa na zulia la kuswali ili mtoto aliangalie wakati wa kuswali, kumwongoza kwa kile kinachotakiwa katika kila sehemu ya Swala, kwa hivyo anaiga kile anachokiona na anachokisikia katika filamu zilizowasilishwa kwake, ni mojawapo ya njia ambazo utaratibu wake unategemea upana wa Sheria ya Kiislamu, na imepokelewa kutoka kwa Bw. wetu Omar Ibn Al-Khatwab, R.A; kutoka kwa Ibn Saad alisimulia katika "Al-Tabaqabat" na kutoka kwa njia yake Al-Baladhuriy katika kitabu cha: [Ansab Al-Ashraf] kutoka kwa Muhammad Ibn Sirin, alisema: "Omar Ibn Al-Khatwab, R.A, ulimpata usahaulifu wakati wa kuswali, kwa hivyo alimfanya mtu nyuma yake amkumbushe, na ikiwa alimwonesha ishara ya kusujudu au kusimama, alifanya hivyo. ”Na Muhammad Ibn Sirin, ingawa hakusikia kutoka kwa Omar, R.A; lakini alikuwa mmoja wa wafuasi wakuu ambao wanavyuoni wameafikiana juu ya kukubali Hadithi zake:
Al-Hafiz Abu Omar Bin Abdul-Barr alisema katika "Al-Tamhiid" (8/301 Wizara ya Waqfu ya Moroko): [Wanavyuoni wa Hadithi wamekubaliana kwa pamoja kwamba Ibn Sirin ndiye anayesimulia Hadithi sahihi zaidi kuliko wafuasi wengine, na kwamba hakusimulia au kuchukua isipokuwa kutoka kwa mwenye dhamana, na kwamba Hadithi zinazopokelewa kutoka kwake ni sahihi; siyo kama Al-Hassan na Atwaa].
Alisema pia – kwa mujibu wa yaliyotajwa na Al-Hafiz Ibn Rajab katika Sharh Illal At-Tirmidhiy (1/556, Maktaba ya Al-Manar): [Kila anayejulikana kwa kuchukua kutoka kwa wenye udhaifu na kusamehe katika jambo hilo: basi Hadithi alizosimulia siyo hoja; akiwa ni mfuasi au aliye chini yake. Na kila anayejulikana kwamba hachukui isipokuwa kutoka kwa mwenye uaminifu, basi Hadithi alizosimulia zinakubalika. Hadithi zinazosimuliwa na Saeed Ibn Al-Musayyab, Muhammad Ibn Sirin na Ibrahim Al-Nakh’i kwao ni sahihi.]
Al-Hafiz Al-Bayhaqiy ametaja katika “Ujumbe wake kwa Sheikh Abi Muhammad Al-Juwayni”: Hadithi zilizosimuliwa na Ibn Sirin ni Hadithi zilizokubaliwa na Imamu Al-Shafi, R.A. akinukuu kutoka "An-Nukat kwa Ibn Al-Salah" na Imamu Al-Zarkashiy (1/483, Adhwaa Al-Salaf).
Kuangalia ushahidi wa sheria na misingi yake kunaonesha kuwa hakuna pingamizi la kisheria la kutengeneza zulia hili, kuliuza na kufaidika nalo, na kujifunza kuswali kupitia hilo kwa njia iliyotajwa hapo juu, kwa sharti tu kwamba kauli na vitendo vya kuswali ni sahihi kwa mujibu wa sheria na inafuatana na madhehebu iliyodaiwa kuwa Swala hiyo ni sawa na masharti yake; Kupokea vitendo vya kuswali kupitia zulia lililotajwa hapo juu ni aina ya kujifunza kitu kinachohusiana na Swala kutoka kwa mgeni; sheria imeshuhudia uhalali wa jambo hilo; hali hii inaonekana katika vitu; miongoni mwake ni:
Kwanza: yale yaliyopokelewa kutoka kwa Masheikh wawili (Al-Bukhariy na Muslim) - na maneno ya Hadithi hii ni maneno yake Imamu Muslim - kutoka kwa Hadithi ya amri ya Mtume, S.A.W. kumtengenezea mimbari, na kisha kuswali kama Imamu kwa watu; Kuwafundisha jinsi wanavyoswali, na kusema kwake - baada ya kumaliza Swala yake ya mwisho na kuwageukia watu -: “Enyi watu! Nimefanya hivi ili mnifuate, na kujifunza Swala yangu.”
Pili: Uhalali wa kumrekebishia Imamu; akikosea katika kisomo chake wakati wa kuswali, au akiacha kitu ambacho kinasomwa kwa lazima lakini hakusoma. Na hali hii imepokelewa kutoka kwa Othman Ibn Affan, Abdullah Ibn Omar, Abu Hurairah na Anas Ibn Malik miongoni mwa Masahaba, R.A, nayo ni kauli yake Ataa', Al-Hasan, na Ibn Sirin, nayo ni kauli yake Malik, Shafiy, Ahmad, na Ishaq, R.A. [Tazama: “Marifatul Sunan Wal Athaar” na Imam Al-Bayhaqi (4/366, Dar al- Wafa’), na “Sharh Al-Sunnah” na Imam Al-Baghawiy (3/159, Al-Maqtab Al-Islamiy)], na wanafiqhi wa madhehebu zinazofuatiwa, wana maelezo kadhaa katika vitabu vya fiqhi katika suala la kumrekebishia Imamu.
Na dalili ya uhalali wa kumrekebishia anayeswali ni: Hadithi iliyopokelewa kutoka kwa Abu Dawud kutoka kwa Ibn Umar, R.A., kwamba Mtume, S.A.W, aliswali Swala, na akaisoma ndani yake, na akakosea ndani yake, na alipoondoka, akamwambia baba yangu: "Je! uliswali nasi?" Akasema: Ndio. Akasema: Ni nini kimekuzuia? yaani: Ni nini kilikuzuia kunirekebishia?
Na Hadithi ile iliyopokelewa pia kutoka kwa Al-Musawar Ibn Yazid Al-Asadi, R.A., kwamba alisema: Nilimshuhudia Mtume wa Allah, S.A.W., akisoma katika Swala, na akaacha kitu ambacho hakukisoma. Mtu mmoja akamwambia Ewe Mtume wa Allah umeacha kuisoma Aya ile na ile, Mtume akasema: “Je! hunikumbushi”
Imepokelewa kutoka kwa Al-Bayhaqiy katika Sunan yake kutoka kwa Anas Ibn Malik, R.A., kwamba alisema: Maswahaba wa Mtume wa Allah, S.A.W., walikuwa wakifundishana katika Swala.
Na imepokelewa kutoka kwa Bayhaqiy, R.A., kwamba akisimama kwa ajili ya kuswali, kijana mmoja akasimama nyuma yake akishika Qur'ani, na akikosea katika chochote, humrekebisha.
Na Imamu Ibn Qudamah alisema katika kitabu cha: [Al-Mughni 1/398, Dar Al-Turath Al-Arabi]: [Imepokelewa kutoka kwa An-Najjad kutoka kwa Aamir Ibn Rabi'ah, alisema: Nilikuwa nimekaa Makka, na ikawa mtu amekaa kwenye kaburi akiomba, na mtu mwingine alikuwa amekaa nyuma yake akimfundisha, basi alikuwa Othman R.A].
Imamu Al-Bayhaqiy alisema katika kitabu cha “Ma'rifat Al-Sunan Wa'l-Athar (4/366): [Imepokelewa kutoka kwa Abu Abd Al-Rahman Al-Sulami, kutoka kwa Ali kwamba alisema: “Imamu akiomba kula, mlishe," Abu Abd Al-Rahman alisema: "Inamaanisha kwamba akikaa kimya." (Yaani akisahau chochote mkumbushe).
Tatu: Uhalali wa kumwonya Imamu juu ya kutokea kwa kusahau au makosa katika Swala; kwamba yule anayeswali nyuma yake anaweza kusema Subhana Allah akiwa yeye ni mwanamume, na anaweza kupiga makofi akiwa ni mwanamke. Kwa kupiga nyuma ya kiganja chake cha kulia kiganja chake cha kushoto au kinyume chake, na Imamu Al-Nawawi alisimulia hivyo katika kitabu cha “Al-Majmuu” (4/14, Al-Muniriyah) kutoka kwa wanavyuoni wengi.
Na dalili ya hivyo ni ile: iliyopokelewa kutoka kwa Al-Bukhari kutoka kwa Sahl Ibn Saad Al-Saadi, R.A., kwamba wakati Mtume wa Allah, S.A.W., alipotoka ili kupatanisha kati ya watu, wakati wa Swala ulifika na hakuja kuswali pamoja na watu, kwa hivyo Abu Bakr, R.A., akatangulia, kisha Mtume wa Allah, S.A.W., akaja, alikuwa akitembea kati ya safu, hadi aliposimama kwenye safu, na watu wakaanza kupiga makofi, na Abu Bakr, R.A., hakuwa akigeuka katika Swala yake, kwa hivyo wakati watu wengi walipopiga makofi akageuka, alimuona Mtume wa Allah, S.A.W., amesimama katika safu na Mtume wa Allah S.A.W., akamwamuru aswali. kwa hivyo Abu Bakr, R.A., akainua mikono yake na kumsifu Allah, na akarudi nyuma yake mpaka akasimama kwenye safu. Mtume wa Allah, S.A.W., alitangulia na akaswali Imamu kwa watu, na alipomaliza, aliwageukia watu na kusema: “Enyi watu! kwa nini mmepiga makofi wakati wa kutokea kitu katika Swala, kupiga makofi ni kwa wanawake tu, katika Swala ikitokea chochote mwenye kuswali anaweza kusema Subhana Allah. Ewe Abu Bakr! Ni nini kilichokuzuia kuswali Imamu kwa watu wakati nilikuashiria? ”Abu Bakr, R.A., alisema: Haiwezekani kwa Ibn Abi Quhafa kuswali mbele ya Mtume wa Allah, S.A.W.
Nne: Uhalali wa kusoma kutoka katika Qur’ani kwa Imamu na kwa anayeswali pekee yake, na hii ni madhehebu ya Imamu Shafi, nayo ni rai iliyochaguliwa na wanavyuoni wa madhehebu ya Imamu Ahmad Ibn Hanbali. 384), na "Al-Mughni" (1/336)].
Imepokelewa kutoka kwa Al-Hafiz Al-Bayhaqi kutoka kwa Mama wa Waumini Aisha, R.A. kwamba: “Yeye Alikuwa akiswali nyuma ya mtumishi wake Dhakwan na wakati ambapo akisoma kutoka Qur'ani.”
Imamu Al-Zuhri aliulizwa juu ya mtu anayesoma Qur'ani katika Ramadhani, akasema: “Mbora wetu alikuwa akisoma kutoka Qur’ani", “Al-Mughni” (1/335).
Ukariri ambao unatokana na zulia linalozungumziwa ni sawa na maswala hayo manne katika kujifunza na kuonya yote yaliyo halali katika maombi ambayo kutokana nayo wageni wanajifunza, na inaonekana katika kila picha iliyotajwa hapo juu, na kutajwa sawa juu ya mamlaka ya Omar Ibn Al-Khattab, Mungu awe radhi naye, kama ilivyotajwa..
Kwa kuongezea yaliyotajwa hapo juu: miongoni mwa masuala yaliyowekwa katika misingi ya Sheria ambayo ni kwamba hukumu ya njia ni sawa na hukumu ya makusudi; basi kufundisha watoto wadogo hukumu za Swala kulingana na kile kinachohitajika kwa aliyetunga Sheria, na kile kinachohitajika kwa sheria ni ya aina mbili: moja: ambayo ni miongoni mwa makusudi, na ya pili: ambayo ni miongoni mwa njia zilizohakikishwa na makusudi hayo, na sheria huthibitishwa njia za utii kama ambavyo huthibitishwa kwa makusudi [Rejea: "Qawaid Al-Ahkaam” na Imamu Al-Izz Ibn Abd As-Salam (1/54,Dar Al-Kutub Al-Ilmiyyah)]. Kutokana na hivyo, utengenezaji na matumizi ya zulia lililotajwa kwa kusudi ambalo limeulizwa linaingia katika ombi ambalo ni halali kwa upande wa umma. Kwa sababu ni njia moja kwa makusudi mengine, ambayo ni kufundisha na kujifunza hukumu za Swala.
Na hali ile ile - kutoka kwa ile inayothibitisha hivyo – ni iliyopokelewa kutoka kwa baadhi ya Masahaba kuhusu kutafuta msaada wa mashine za kuhesabu rakaa na kadhalika zinazohusiana na Swala. Al-Hafiz Ibn Rajab Al-Hanbali alisema katika kitabu chake: “Ahkam Al-Khawatim na yanayohusiana nayo" (uk. 109, Dar Al-Kutub Al-Ilmiyyah): [Imepokelewa kutoka kwa Al-Fadhl Ibn Shadhan Al-Razi Al-Maqri katika kitabu chake: “Ad Al-Ay” kupitia kwa Abd Al-Rahman Ibn Al-Qasim kutoka kwa baba yake kutoka kwa Aisha, R.A.: kwamba akiswali Swala ya lazima, alihesabu Swala yake kwa pete yake, akiigeuza pete katika vidole vyake hadi kumaliza Swala zake.
Imepokelewa kutoka kwa Abu Ma’shar, kutoka kwa Ibrahim, alisema: “Hakuna ubaya kwa mtu ambaye anahifadhi Swala yake kwa pete yake.”]
Mwanachuoni Al-Kharshi Al-Maliki alisema katika “Sharh Al-Mukhtasar” (1/294, Dar Al-Fikr): [Sio ujinga kugeuza pete kutoka kidole hadi kingine kwa ajili ya kuhesabu idadi ya rakaa ili asisahau; Kwani kufanya hivyo ni kwa ajili ya kurekebisha Swala tu].
Kuhusu CD iliyotumwa kwetu, baada ya kutazama yaliyomo ndani yake; nayo ni mfano wa Swala ya Adhuhuri itakayowasilishwa mbele ya mtoto anayeswali; Tunaonya yafuatayo:
Kwanza: ni jambo la lazima kubadilishwa kwa picha iliyooneshwa ili kufaa na hukumu za madhehebu ambayo Swala zinafuatwa hukumu zake.
Pili: Inahitajika kupitia tena lugha ya maneno yanayotamkwa na yanayosikika.
Tatu: Dua ya kufungua Swala ilionekana kwamba ilisomwa kabla ya takbiir ya ufunguzi wa Swala, na maoni sahihi - kulingana na wale wanaosema - ni kwamba dua hii inasomwa baada takbiir ya ufunguzi wa Swala na kabla ya kusoma Al-Fatihah.
Nne: Al-Fatihah ilisomwa wakati wa kusimama bila kusoma chochote katika Qur'ani baada yake, au kwa kuonya kwamba kuna kitu kilisomwa kutoka hapo baada yake.
Tano: Tunashauri kwamba usomaji ufanywe kwa njia ya Qur’ani inayofundisha. Ambapo msomaji anasoma kisha anaacha nafasi kwa anayeswali ili asome baada yake.
Sita: Ni jambo la lazima kuzingatia nafasi za kusoma kwa sauti na kusoma kwa siri. Ambapo haikuonekana kumuonya mtoto anayeswali kwamba usomaji anaosikia unarudiwa kwa sauti au kwa siri.
Saba: Hakuna usomaji wowote kwa Adhkar za kusujudu, na kukaa kati ya sijda hizo mbili.
Nane: Ni sawa pia kuchukua faida ya yaliyomo baada ya kurekebisha kwake na kuibadilisha kwake kwa kuionesha kwenye simu mahiri.
Kuhusiana na tafiti zilizoambatanishwa ambazo zinaonesha maelezo ya Swala kulingana na madhehebu manne, baada ya kuzipitia, tunasema kwamba: Njia yetu ya kuzipitia ni kuthibitisha madhehebu iliyochaguliwa, au ambayo inafuatwa na wanafiqhi wengi.
Tafiti hizi zote zinahitaji kupitiwa kwa lugha, na kwa sababu ya wingi wa makosa katika lugha hatukuzithibitisha, zinahitajika pia kurekebishwa upya.Inahitajika pia kutaja kusoma kwa siri katika mahali pake, na pia kusoma kwa sauti katika mahala pake katika Swala zote. Tumeambatanisha na Fatwa hii makosa yaliyotajwa katika tafiti hizo, na usahihi wa makosa haya moja kwa moja.
Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ni Mjuzi Zaidi

Share this:

Related Fatwas