Kumpa Mtoto Jina la Kwanza la Mfadh...

Egypt's Dar Al-Ifta

Kumpa Mtoto Jina la Kwanza la Mfadhili Wake

Question

 Hapo awali mmetoa Fatwa inayoruhusu utoaji wa jina la familia la mfadhili kumpa mtoto anayefadhiliwa asiyejulikana wazazi wake. Hii ni kwa namna ya kuitwa mtoto kwa jina maalumu, kisha majina kadhaa ya kupewa yanatajwa katika ukoo wake, kisha jina la ukoo la familia ya mfadhili linatajwa mwishoni.
Swali hapa: Je, inajuzu kutaja baada ya jina la mtoto jina la mfadhili wake pamoja na ukoo wa familia ya mfadhili, ilimradi tu majina ya kupewa ambayo ni tofauti na ukoo wa mfadhili halisi yatatajwa kati kati yake?
Je, nini hukumu ikiwa jina la mfadhili lina mchanganyiko wa Majina? Je, inajuzu kumpa mtoto aliyefadhiliwa jina hilo? Kuweka katika nyaraka rasmi sehemu ya kwanza ya jina lenye mchanganyiko katika nafasi iliyowekwa kwa ajili ya kuweka jina la baba ndani yake, na jina la pili katika nafasi ya jina la babu, kisha linatajwa jina la kupewa, kisha jina la ukoo la familia ya mfadhili mwishoni?
Kuhusu kesi yangu: Nimemfadhili mtoto wa kike ambaye jina lake ni: Aisha, na jina langu ni: Ahmed Yahya - ambalo ni jina lenye mchanganyiko wa majina mawili - na jina la baba yangu ni: Muhammad Jamal Al-Din - ambalo pia ni jina lenye mchanganyiko wa majina mawili - na jina la babu yangu ni: Abdul Rahman, na ukoo wa familia ni: Rashid, mimi ni: Ahmed Yahya Bin Mohammed Jamal Al-Din Bin Abdul Rahman Bin Rashid.
Je, inajuzu kwangu kutaja jina la mtoto wa kike aliyetajwa: Aisha Ahmed Yahya, kisha nitaje jina moja au mawili ya kupewa, kisha jina la ukoo wa Rashid; Kwa sharti kwamba jina (Ahmed) litajwe kwenye nyaraka rasmi katika nafasi iliyopangwa kwa ajili ya kutaja jina la baba, kisha jina: (Yahya) linatajwa katika nafasi ya jina la babu, halafu jina la kupewa linatajwa, kisha jina la ukoo wa familia yangu: (Rashid)?
Je, inajuzu kutajwa jina kamili la mke wangu katika nafasi ya jina la mama, au inatosha kutajwa jina lake la kwanza tu kisha likafuatiwa na majina ya kupewa, kisha jina la ukoo wa familia yake?
Kwa taarifa kusudio la haya yote ni kuhifadhi Afya ya kisaikolojia ya binti huyo ambaye sasa ana miaka minne, na nia yetu ni kumjulisha kuwa sisi sio wazazi wake wa kweli, lakini katika wakati sahihi na kwa njia sahihi; na hivyo ndivyo wataalamu wa saikolojia wanavyotuambia?

Answer

 Sifa zote njema ni za Allah pekee, na swala na salaam ziwe juu ya Bwana wetu Muhammad Mtume wa Mwenyezi Mungu, na pia juu ya jamaa zake na maswahaba zake, na juu ya wale wanaowafuata kwa wema mpaka Siku ya Malipo.
Sharia ya Kiislamu ililisimamia suala la nasaba, ikalilinda na kulihifadhi kama mojawapo ya malengo muhimu ya kisheria, na zikawekwa kanuni na mipaka ya kuilinda kuiepusha fujo na uwongo; Kwa hiyo, kanuni za ndoa zilitungwa, uharamu wa zinaa, kusingizia wanawake, na kutotunza heshima za Waislamu, na kanuni na hukumu nyingine.
Mwenyezi Mungu hakuwaachia viumbe wake nafasi ya kuchagua nasaba zao, bali aliwawekea uthibitisho wa ukoo kwa njia maalumu; Kama vile ndoa sahihi, kukiri, ushahidi, ndoa inayoshukiwa, na kila ndoa iliyobatilishwa baada ya kuingia kwa sababu ya ufisadi wake.
Kwa hiyo Sheria ilikataza kuasili; Nako kule ambako mwanamume anamnasibisha mtoto wa mtu mwingine kwake, na kilichofuatwa katika zama za kabla ya Uislamu ni kwamba kulea kunamthibitishia mtoto anayedai juu ya mwenye kuasili haki zote ambazo zinawekwa kwa ajili ya mtoto halisi juu ya baba yake; Al-Nasafiy alisema katika tafsiri yake [3/17, Dar Al-Kalim Al-Tayyib]: “Ikasemwa: “katika zama za kabla ya Uislamu ilikuwa Mtu anapompenda mtoto wa mtu mwingine, humshirikisha kwake, na humtengea fungu la kurithi la mtoto wa kiume na kuwa katika watoto wake, na hujinasibisha naye; na husemwa: Fulani ni mtoto wa fulani.
Basi Uislamu ukaufuta mfumo huu, ukaamrisha asinasibishwe mtoto yeyote isipokuwa kwa baba yake tu, na kwamba mtoto anayedaiwa asinasibishwe kwa yule aliyemfadhili. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {Wala hakuwafanya watoto wenu wa kupanga kuwa ni wana wenu khasa. Hayo ni maneno ya vinywa vyenu tu. Na Mwenyezi Mungu ndiye anayesema kweli, naye ndiye anayeongoa Njia.(5) Waiteni kwa baba zao, maana huo ndio uadilifu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu. Na ikiwa hamuwajui baba zao, basi ni ndugu zenu katika Dini, na rafiki zenu.} [AL AHZAAB: 4,5]; Mwanachuoni Al-Taher Ibn Ashour amesema katika kitabu cha: [Al-Tahrir na Al-Tanweer 21/261, Al-Dur Al-Tunisiah]: “Jambo hili ni uthibitisho, ambao kwalo madai ya mwenye kuasili yanabatilika kuwa mwanawe. Maana ya kuwaita kwa baba zao: nasaba. Na maana ya kuwaitia kwa baba zao: matokeo ya hilo; Nayo ni kwamba wao ni watoto wa baba zao, sio watoto wa wale waliowafadhili. Inajulikana kuwa sahaba mkubwa Zaid Ibn Haritha aliitwa (Zayd Ibn Muhammad) wakati Mtume wa Mwenyezi Mungu S.A.W. alipomfadhili. Katazo liliposhuka, jina lake lilirudishwa kama lilivyokuwa (Zayd Ibn Haritha).
Imepokelewa kutoka kwa Al-Bukhariy kutoka kwa Wathila Ibn Al-Asqaa, R.A. kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu S.A.W. amesema: “Mojawapo ya uwongo mkubwa zaidi ni kwamba mtu anajinasibisha na baba asiyekuwa wake”
Imepokelewa kutoka kwa Muslim kutoka kwa Ali Ibn Abi Talib R.A. kwamba Mtume S.A.W. amesema: “Mwenye kujinasibisha na baba asiyekuwa wake, au kujihusisha Mtumwa na Bwana si wake, basi laana ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Malaika, na watu wote itakuwa juu yake, na Allah haikubali toba yake au fidia siku ya Kiyama”.
Imamu Al-Nawawi amesema katika kitabu cha [Sharhu Muslim 9/144, Dar Ihyaa At-Turathi Al-Arabiy] wakati wa kutoa maoni yake juu ya Hadithi hii: “Hili liko wazi katika ukali wa uharamu wa mtu kujihusisha na mtu asiyekuwa baba yake, au Mtumwa kujihusisha na Mtu asiyekuwa Bwana wake, Kwa sababu ya kukufuru neema, na kupoteza haki za urithi, uaminifu, akili na mengineyo, pamoja na kukatwa ukoo na kuasi”. Kuna mambo kadhaa muhimu yanayohusiana kwa karibu na suala la ukoo; ambapo matokeo yake ni kuruhusiwa na kutoruhusiwa:
Mojawapo ni: ndoa; Ukoo ni moja ya sababu ya kuharamisha wanawake. Kwani Mwenyezi Mungu Mtukufu Anasema: {Mmeharimishiwa mama zenu, na binti zenu, na dada zenu, na shangazi zenu, na khaalati zenu, na binti wa ndugu mume, na binti wa dada} [AN NISAA: 23], Kujua ni nani anayeruhusiwa kuoa na ni nani anayeharamishwa kunategemea uthibitishwaji wa nasaba au kutokuwepo kwake.
Ikiwemo: Urithi; nao urithi ulikuwa mwanzoni mwa kutunga Sheria ya udugu uliyofanyika Madina, kisha Sheria ikakataza hilo, na kufanya urithi uwe baina ya jamaa; Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema: {Na jamaa wa nasaba wanastahikiana wenyewe kwa wenyewe zaidi katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua kila kitu.} [AL ANFAAL: 75], Ibn Abbas amesema: “Mtume (S.A.W) alifanya udugu baina ya maswahaba zake, na wakaurithi udugu huo mpaka ilipoteremka Aya hii, wakarithishwa kwa nasaba. [Zad Al-Misir fi 'ilm Al-Tafsir, kitabu cha Ibn Al-Jawzi 2/229, uk. Dar Al-Kitab Al-Arabiy].
Ikiwemo: kuunganishwa kwa jamaa, na ilipokelewa katika matini nyingi za kisheria amri ya kuunganisha undugu, na kitisho cha kuwatenga; zikiwemo Aya hii ya Qur`ani: Mwenyezi Mungu anasema: {Basi yanayo tarajiwa kwenu mkitawala ndio mfisidi katika nchi na mwatupe jamaa zenu?} [MUHAMMAD: 22].
Imepokelewa kutoka kwa Imamu Muslim kutoka kwa Mama wa Waumini Aisha, R.A., kwamba Mtume, S.A.W amesema: “Tumbo la uzazi limeshikamana na arshi, linasema. “Yeyote atakayejiunga nami, basi Mwenyezi Mungu atamuunganisha, na yeyote anayenitenga, basi Mwenyezi Mungu atamkatilia mbali.” Ni lazima kwa kila mtu kuunganisha tumbo hilo la uzazi ambalo limewekwa kwa Sheria, sio lile analozua.
Ikiwemo: katika umiliki, imethibiti katika fiqhi kwamba umiliki haukuwa baina ya asili na tawi, hivyo mtu hammiliki baba yake, hata akiwa ni juu katika nasaba, wala mwanawe, hata akishuka chini katika nasaba. Baadhi ya wanavyuoni wameitanua hali hiyo, wakisema kuwa mwenye tumbo la uzazi kutoka kwa maharimu basi ameachiliwa huru. Ushahidi wa yale yaliyopokelewa na wale maimamu wanne ambao ni Ahmad katika Musnad yake kutoka kwa Samra Ibn Jundub, R.A, kwamba Mtume, S.A.W amesema: “Mwenye kumiliki tumbo la uzazi kutoka kwa maharimu basi anaachiliwa huru.”
Kwa maana hii, Imamu Ibn Hazm anasema katika kitabu cha: {Jamharat Ansaab Al-Arab 1/2, 3 juz. Dar Al-Kutub Al-Elmiyya]: “Ni wajibu katika nasaba kumjua baba yake na mama yake, na kila atakayekutana naye kwa nasaba katika tumbo la uzazi linaloharamishwa, ili kuepukana na wale aliyoharamishiwa kuoana nao. Na kumjua kila mtu ambaye ana uhusiano naye kwa tumbo ambao unalazimu urithi, au unahitaji kuunganishwa naye, au kutumia pesa, au mkataba au hukumu; Yeyote asiyejua haya amekosa wajibu wa dini yake”.
Kwa hiyo, kuchezea nasaba kwa kuingiza isiyokuwa ndani yake; kumhusisha mtu kwa asiyekuwa baba yake ili amshirikishe jina lake lote, hali hii ni ufisadi mkubwa; Kwa sababu ya kuchanganya nasaba, kuvurugika kwa undugu na mafungamano asilia ya kifamilia, uvunjaji wa mirathi na mengine yanayofanana na hayo, na kuenea kwa uadui na chuki baina ya watoto na jamaa halisi na baina ya mtu wa kuasili; Kwa msongamano wake nao katika gharama na urithi na kadhalika. Mbali na uwongo ulioharamishwa unaopelekea kuvuruga mafungamano ya jamaa.
Lakini kuna maana nyingine ya kuhusiana na wengine ambayo haijakatazwa, wala haijumuishi maovu yoyote yaliyotajwa. Ni kwa mtu anayehusiana na familia fulani kwa njia inayoonesha kuwa ni wa familia hii kabisa, bila ya udanganyifu kwamba yeye ni mtoto wa mmoja wa wanachama wake halisi, kwamba sifa ya familia iko mwishoni mwa jina lake, na hii ni sawa na uhusiano uliokuwa kati ya makabila ya Kiarabu hapo awali, na hali hii haiingii ndani ya upeo wa kuasili ambao umekatazwa na sheria; Kwa sababu kuasili ni kumuongezea mtoto mwingine na kumfahamu kuwa kama mwanawe katika hali ya mirathi na nasaba, na kukaa peke yake pamoja na wanawake wa familia kama maharimu wake, na mambo mengine yaliyokuwa ya kawaida katika zama za kabla ya Uislamu na katika zama za Uislamu wa mwanzo. Kisha Uislamu ukakataza hali ile kuhakikisha kwamba nasaba haichanganyiki - kama ilivyotajwa hapo awali -.
Mwanachuoni Al-Alusiy amesema katika kitabu cha: [Rouh Al-Ma’ani 21/149, uk. Al-Muneriyah] katika tafsiri ya Aya hii: {Waiteni kwa baba zao, maana huo ndio uadilifu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu. Na ikiwa hamwajui baba zao, basi ni ndugu zenu katika Dini, na rafiki zenu.} [AL AHZAAB: 5]: “Maana ya dhahiri ya Aya hii ni kukataza kumhusisha mtu kwa asiyekuwa baba yake kwa makusudi, na labda hali hiyo kama ilivyokuwa katika zama za Ujinga (kabla ya Uislamu), lakini ikiwa si hivyo, kama mzee anavyosema kwa mdogo kwa huruma: (Ewe mwanangu) - na mara nyingi usemi huu husemwa - basi inaonekana kwamba hakuna ukatazo. Katika maelezo ya chini ya Al-Khafaji juu ya tafsiri ya Al-Baydawi: kuasili, na ikiwa tafsiri yake ni sahihi ni kama udugu, lakini imeharamishwa kwa kufanana na makafiri. Labda hakuna ushahidi wa uharamu huu katika Aya iliyotajwa. Ni nini kinachoashiriwa na uharamu wa kulingania kwa namna ilivyokuwa katika zama za kabla ya Uislamu”.
Imepokelewa kutoka kwa Mashekhe wawili kutoka kwa Anas, R.A., amesema: Mtume S.A.W. aliwaita Al-Ansar akisema: “Je, kuna yeyote asiyekuwa miongoni mwenu?” Wakasema: Hapana isipokuwa mtoto wa dada yetu, Mtume wa Mwenyezi Mungu S.A.W. amesema: “Mtoto wa dada wa watu ni miongoni mwao”. Katika Hadithi hii, Mtume S.A.W., amebainisha kuwa mtoto ni wa kabila la mama yake na si miongoni mwao kwa kweli.
Al-Manaawiy amesema katika kitabu cha [Faydh Al-Qadiir 1/87, 88, Dar Al-Maarifa]: Kauli yake: “Mtoto wa dada wa watu ni miongoni mwao”; kwa sababu amenasibishwa kwa baadhi yao, naye ni mama yake, kwa hiyo ana uhusiano na jamaa zake katika yote anayopaswa kuhusiana nayo, kama vile msaada, ushauri, mapenzi, kufichua siri, usaidizi, uchamungu, huruma na ukarimu. Na kadhalika”.
Na katika Sahih Al-Bukhariy: Kwamba Hatib Ibn Balta’ah R.A., alimwambia Mtume S.A.W: “Nilikuwa mmoja wa Makureshi, lakini sikuwa miongoni mwao.” Katika Hadith hii, Hatib, R.A., ametaja kwamba yeye ni mmoja wa kabila la Makureshi lakini si kweli.
Al-Hafidh Ibn Hajar amesema katika kitabu cha: [Fath Al-Bari 8/634, Dar Al-Marifa]: “Kauli yake: (Nilikuwa mmoja wa Makureshi), maana yake ni: si kwa kweli, kwa sababu alisema baada ya hapo: (Nami sikuwa miongoni mwao) Kauli yake: (Nilikuwa mmoja wa Makureshi, lakini sikuwa miongoni mwao) Huu sio mgongano, bali alimaanisha kuwa yeye ni miongoni mwao kwa maana ya kuwa yeye ni mshirika wao, na imethibitishwa Hadithi ya Mtume S.A.W. isemayo: “Mshirika wa watu ni miongoni mwao”.
Kazi ya watu wema waliotangulia na watu wa Hadithi ilifanywa bila lawama kwa uwiano usio na kawaida, na kama jambo hilo likiharamishwa au kulazimu kwa kuasili ambako kumekatazwa, walikuwa wakilikanusha.
Al-Hafiz Al-Sakhawiy amesema katika kitabu cha: [Fath Al-Mughith Bi-sharh Alfiyat Al-Hadith 3/297, Dar Al-Kutub Al-Elmiyyah], akielezea maneno ya Al-Iraqi: “(Na wakanasibisha) baadhi ya wapokezi kwa mahali palipotokea tukio, au katika nchi, au kabila, au ufundi, au sifa, au mambo mengine ambayo hayaonekani mbele ya ufahamu unaokusudiwa.
Al-Hafiz Al-Suyutiy anasema katika kitabu cha [Tadreeb Al-Rawi 2/ 340, Maktaba Ar-Riyadh Al-Hadithah]: “Msimulizi anaweza kunasibishwa na nasaba: kutoka mahali, au kabila, au ufundi, siyo hali iliyodhahiri ambayo inatangulia uelewa wa nasaba hii haikukusudiwa, bali kwa sababu ya mahali moja, au kabila hilo, na kadhalika.
Na nasaba, ikiwa imetoka katika asili ya mtu, inaweza kuwa kwa ajili ya uhuru, ambao ndio unaowezekana zaidi, kama: Abu Al-Bakhtariy Al-Ta'i'i, na jina lake ni Said Ibn Fairouz, ambaye ndiye ni baba wa Tai, kwa sababu bwana wake alitoka Tai na alimwacha huru. Inaweza kwa ajili ya kuwa mshirika; hali ambayo ndiyo chimbuko lake ni mkataba na mapatano ya kusaidiana, na kukubaliana, kama vile: Imam Malik Ibn Anas Al-Asbahiy Al-Tayimiy, yeye ni Asbahi kwa kweli, na mshirika kwa kabila la Tayim. Hii ni kwa sababu watu wake wa "Asbah" washirika kwa Tayim wa Makureshi. Uislamu ulifuta ushirika wa utii uliokuwa katika zama za kabla ya Uislamu za ugomvi na mapigano baina ya makabila au uvamizi bila ya ushindi wa waliodhulumiwa na kuunganisha kwa jamaa. Nasaba inaweza kuwa kwa utii wa mhudumu; kukodisha au kujifunza; Kama: Miqsam, iliambiwa kuwa ni mtumwa wa Ibn Abbas kwa ajili ya usahaba wake. inaweza kuwa kwa kunyonyesha; Kama Abdullah Ibn Al-Saadi, ambaye ni mmoja wa masahaba; Baba yake aliitwa: Al-Saadi; Kwa sababu alinyonyeshwa katika Bani Saad Ibn Bakr. Inaweza kuwa kwa dini na Uislamu; Kama vile: Muhammad Ibn Ismail Al-Bukhariy Al-Jaafiy; Kwa sababu babu yake Al-Mughirah alikuwa mmoja wa majusi, basi alisilimu kwa sababu ya Al-Yaman Ibn Akhnas Al-Jufiy, na akanasibishwa kwake. Nasaba inaweza kuwa kwa cheo fulani; kwa maana kuwa jina lake lilijumuishwa katika moja ya madaraka, kwa hivyo alinasibishwa kwa wamiliki wa madaraka hayo. Huyu ni kama Imamu Al-Layth Ibn Saad Al-Fahmiy, na ilinasibishwa na Fahm; Kwa sababu jina lake lipo katika diwani ya Misri katika watumwa wa Kinana Ibn Fahm, na watu wa nyumba yake wanasema: Sisi ni Wafursi kutoka kwa watu wa Isfahan, yaani: asili yake ni kutoka Isfahan, lakini ananasibishwa na Fahm; Kwa sababu jina lake limo katika diwani ya Fahm [Rejea: Tarekh Dimishq 50/347, Dar Al-Fikr]. Nasaba kwa watu wasio wa asili katika mifano ya awali haijumuishi makatazo ya kisheria katika kuasili.
Kwa hiyo, Dar Al-Iftaa ya Misri, katika Fatwa yake Na. 310 ya mwaka wa 2010 A.D., ilisema kwamba inajuzu kumpa mtoto aliyefadhiliwa jina la familia ya mfadhili wake kama jambo la kuhusishwa, ili ushirika kamili wa familia uonekane bila ulaghai kwa kudai kuwa ni mtoto wao wa kweli.
Swali hapa lilikuwa juu ya kutaja jina la mfadhili pamoja na jina la familia yake, na majina ya bandia ambayo ni tofauti na jina la mfadhili wa kweli, pia inaruhusiwa. Vile vile, ikiwa jina la mfadhili ni la kiwanja, basi inajuzu pia kumpa mtoto aliyefadhiliwa kwa namna iliyotajwa katika swali hilo, kwamba sehemu ya kwanza ya jina la kiwanja iwekwe kwenye nyaraka rasmi katika nafasi inayohusishwa kwa jina la baba, na jina la pili linaandikwa katika nafasi ya jina la babu, kisha jina la bandia linatajwa, kisha jina la familia ambayo ni mfadhili mwishoni. Kwa sababu ukweli wa kuasili haupo kwenye hali hii na ile iliyo kabla yake. Imetajwa hapo awali kuwa kuasili ni kumuongezea mtoto wa mtu mwingine na kumfanya achukue nafasi ya mwanawe katika mirathi, nasaba, na anakaa peke yake pamoja na wanawake wa familia kwa madai ya kuwa wao ni maharimu wake, na kadhalika. Ama hapa katika hali hizi mbili, mfadhili hakudai ubaba wake kwa aliyefadhiliwa, na hakushiriki jina lake kamili naye kwa kile kinachoeleweka kutoka kwake kuwa ni mtoto wake wa kweli; na nyaraka rasmi zinaeleza nasaba hii kwa kina, na kwa njia ambayo huondoa mashaka; nyaraka hizi zinapambanua kati ya jina la kiwanja, ambalo ni ishara ya mtu mmoja maalum, na jina la baba yake, ikiwa ni jina la kiwanja au siyo la kiwanja.
Ipasavyo, na katika muktadha wa swali hilo: inaruhusiwa kwa jina la mtoto aliyefadhiliwa kuwa: (Aisha Ahmed Yahya), kisha weka jina lingine la bandia, kisha uchukue jina la familia yako: (Rashid). Kwa ingizo lililotajwa kwenye kiini cha swali, ambalo ni kuweka jina la: (Ahmed) katika nyaraka rasmi kwenye nafasi iliyohusishwa kwa ajili ya kutaja jina la baba, kisha huwekwa jina la: (Yahya) katika nafasi iliyotengwa kwa ajili ya kutaja jina la babu, kisha jina la bandia, kisha jina la familia yako: (Rashid), na katika hali hiyo kuasili hakuwa haramu. Pia inaruhusiwa kuandikwa jina la mke wako badala ya jina la mama, pamoja na jina la familia yake, ilimradi tu majina mengine ya bandia yatakuwa kati yake.
Kwa sharti la kumfahamisha mtoto ukweli wa hali yake katika wakati ufaao na kwa njia ifaayo kama ilivyoamuliwa na wataalamu wa afya ya kisaikolojia.
Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ni Mjuzi Zaidi
Ofisi ya Fatwa

 

Share this:

Related Fatwas