Mwenye kuritadi

Egypt's Dar Al-Ifta

Mwenye kuritadi

Question

 Sheikh aliyetoa hotuba ya Ijumaa katika Msikiti wa Rashdan leo hii ametaja Hadithi yenye maana ya “Mwenye kubadili dini yake, muueni” katika muktadha wa kuzungumzia baadhi ya Wamisri wanaoritadi Uislamu. Kwa hiyo, nataraji kushauriana na rai ya Dar Al-Iftaa juu ya kiwango cha usahihi au nguvu ya Hadithi hii, na kiwango cha usahihi wa rai iliyowasilishwa na Sheikh kuhusu ulazima wa kumuua anayeritadi Uislamu, na kama ni maoni yake binafsi, je, hayo yanakubaliana na rai ya Al-Azhar, au Dar Al-Iftaa, au Wizara ya Wakfu inayosimamia msikiti huo, au vipi hasa?
Ndani ya mipaka ya elimu yangu, Mtume wa Mwenyezi Mungu (S.A.W) hakuwahi kumuua mtu yeyote kwa sababu ya kuritadi Uislamu, na hakuna hata mmoja katika makhalifa wake waongofu aliyefanya hivyo. Sheikh Mahmoud Shaltout, Mwenyezi Mungu amrehemu, ana kitabu kilichochapishwa ambamo ameifafanua rai hii na akasema kwamba Hadithi hii ni Hadithi moja isiyozingatiwa katika kusimamisha adhabu, na kwamba kumuua anayeritadi haijuzu isipokuwa akitoka dhidi ya kundi la Waislamu, au kubeba silaha dhidi yao au kitu kama hicho. Ama kuritadi kwake tu, dhambi yake ni juu yake na hisabu yake kwa Mwenyezi Mungu. alitaja Aya nyingi zinazoashiria uhuru wa imani na hakuna kulazimishwa katika dini na kwamba Muhammad, S.A.W., alitumwa kama Mtume, mwalimu, mwongozo na rehema kwa walimwengu wote. Hakutumwa kama walii wala mtawala n.k.
Tafadhali tushauri kuhusu maoni sahihi kwa baruapepe yangu katika kampuni iliyooneshwa hapo juu, na Mwenyezi Mungu akulipe kheri?

Answer

 Kwa jina la Mwenyezi Mungu, sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na sala na amani zimshukie Mtume wa Mwenyezi Mungu, na baada ya hayo.
Katika habari, tunapaswa kutofautisha kati ya mambo mawili ambayo ni kuthibitishwa kwake na kuelewa kwake.
Hadithi inaweza kuthibitika kwa mtazamo wa mapokezi, lakini inapofahamika katika muktadha wa jumla ya Sheria, maana yake inakuwa wazi. Na Hadithi iliyotajwa ni sahihi imepokelewa kutoka kwa Al-Bukhari katika sahihi yake, Abu Daud katika Sunan yake, na At-Termidhi kutoka Hadithi ya Ibn Abbas R.A.
Njia za wanavyuoni zimekhitalifiana katika kuifahamu Hadithi hii iliyotangulia, kwa hivyo inasemekana kuritadi ni jinai inayohitaji adhabu kwa kila mwenye kulitenda, isipokuwa baadhi ya wanavyuoni wa Fiqhi waliosema hakuna adhabu ya kidunia kwa anayeritadi isipokuwa kwa kiwango cha mzozo wa kijamii unaotokea. Ibrahim Al-Nakha'i alichagua rai inayosema kuwa toba inaombwa kutoka kwa anayeritadi milele.
Na rai hii ndiyo iliyochaguliwa, hasa katika zama hizi, kwa sababu ushahidi kwa ujumla wake ulizungumza juu ya aliyeritadi aliyetangaza wazi kwa ukafiri wake na kuwadhuru watu kwa kitendo chake hicho, na madhara yake hayakuishia kwake yeye mwenyewe tu, bali zaidi ya hayo yalisababisha mtikisiko ambao uliongoza kwenye fitna, kwa mujibu wa kauli yake Mwenyezi Mungu: {Kama wanaafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, na waenezao fitna katika Madina hawatoacha, basi kwa yakini tutakusalitisha juu yao, kisha hawatakaa humo karibu yako ila muda mchache tu (60) Wamelaanika! Popote watakapo onekana watakamatwa na watauliwa kabisa (61)} [Al-Ahzab 60: 61] na kwa sababu Mtume S.A.W., amefanya kuritadi dini inayoruhusisha damu kwa kuondoka katika kundi hilo kwa kusema (Naapa kwa Mwenyezi Mungu Ambaye hakuna mungu isipokuwa Yeye tu hairuhusiwi kumwaga damu ya Muislamu anayeshuhudia kuwa hakuna Mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu na kuwa Muhammad (S.A.W.) ni Mtume wake isipokuwa katika [visa] vitatu: mtu anayeacha dini yake na kujitenga na jamaa). [Sahih Muslim 3/1302]. Hiki ni kikwazo kinachoonesha kwamba koleo la ubomoaji limefanywa katika mkutano, na kwa sababu ulimwengu umeahidi kuheshimu uhuru wa imani, nao ni mpango wa busara ambao tunaheshimu. Mtume S.A.W., aliishi katika Al-Madina yuko pamoja na Ibn Ubai na wengineo, na anaujua unafiki wake, na wala hakumuadhibu.
Kwa ajili ya hayo na mengineyo, Sheikh Shaltout na wengine walielekea kwenye ukweli kwamba jinai la ukafiri “kuritadi” kwa tendo lenyewe haliruhusu kumwaga damu, bali kinachoruhusisha kumwaga damu ni kupigana na Waislamu na kuwafanyia fujo na kujaribu kutia fitna katika dini yao. [Al-Islam Aqida wa Sharia uk.103]
Na hitimisho, Hadithi iliyotajwa katika swali ni sahihi, lakini pamoja na kuongezwa kwa Hadithi na Aya zilizobaki ndani yake, inaeleweka kuwa kuritadi ni kosa linalohitaji adhabu huko akhera, lakini anayeritadi hatakiwi kuadhibiwa katika dunia hii isipokuwa kama anayeritadi huyo akisababisha madhara ya kijamii

 

 

Share this:

Related Fatwas