Adamu na Shetani

Egypt's Dar Al-Ifta

Adamu na Shetani

Question

Shetani alijuaje kwamba Adamu angeshuka duniani? 

Answer

 Kwa jina la Mwenyezi Mungu, sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na rehma na amani zimwendee bwana wetu Mtume wa Mwenyezi Mungu, jamaa zake, masahaba wake na wanaomfuata, na baada ya hayo:
Qur`ani Tukufu imezungumza kuhusu majaribio ya Ibilisi kumpotosha Adam na Mke wake Hawa, kuhusu kufukuzwa Ibilisi kutoka Peponi, kuhusu maombi ya Ibilisi ya kutaka muhula, kuhusu majibu ya Mwenyezi Mungu ampe muhula mpaka Siku ya Kiyama, na kuhusu maonyo ya Ibilisi dhidi ya Adam na kizazi chake mpaka Siku ya Kiyama, hayo yote yametajwa katika aya kadhaa za Qu`rani Tukufu.
Adui wa Mwenyezi Mungu, Ibilisi, alikuwa ni mshirika wa malaika, na malaika na Ibilisi walikuwa na tabia ambazo si miongoni mwa sifa za wanadamu katika suala la kiini cha usafi na utayari wao wa kutambua na kuelewa uhalisi wa mambo kwa kuona tu. kwani maono ya Ibilisi ya kuonekana kwa Adamu na mkewe yalimfanya aelewe kwamba kiumbe huyu ndiye anayependelewa zaidi na kwamba Mwenyezi Mungu ndiye atamjaalia Mrithi wa Dini yake.
Ndio maana Sheikh At-Tahir Ibn Ashuur anasema katika Tafsir At-Tahrir wat-Tanwiir: “Ukweli tu kwamba Malaika walimtazama kiumbe huyu wa ajabu ambaye makusudio yake ni kumfanya Mrithi wa Dini katika ardhi inatosha kuwaelewesha mambo yaliyomo ndani yake ya maajabu ya sifa kwa namna ambayo ataidhihirisha kwa nje, kwa sababu mitazamo yao ni ya hali ya juu sana kutokana na usalama wao kutokana na kuharibika kwa mada.
Na kama wanadamu wanahitilafiana kati yao kuhusu maono ya mambo yenye siri, na mwelekeo wa mwangaza wa roho zao kwenye habari, na kutazamia na kuchunguza viumbe, kiasi cha tofauti yao kuhusu sifa za roho zikiwa za kimaumbile, kijitihada, au za kiufahamu, ambazo ngazi yake ya juu ni Unabii. Basi unazionaje roho halisi za kimalaika?”

 

 

 

Share this:

Related Fatwas