Kuuawa kwa Kaab Bin Al-Ashraf!

Egypt's Dar Al-Ifta

Kuuawa kwa Kaab Bin Al-Ashraf!

Question

Matini ya Tuhuma:
Mtume wa Uislamu (S.A.W.) alipoambiwa kwamba Ka’b bin Al-Ashraf alikuwa akimkashifu na kuwachochea Makuraishi dhidi yake kupitia mashairi yake, Mtume (S.A.W.) alituma watu watano akiwemo: Abu Na’ila Ndugu yake Ka’b wa kunyonya, kwa ajili ya kumuua, basi Mtume wa Uislamu (S.A.W.) akaenda nao mpaka Baqii’ Al-Gharqad, kisha akawaelekeza, na akasema: Nendeni kwa jina la Mwenyezi Mungu, Ewe Mola wasaidie, kisha akarudi nyumbani kwake usiku wa mbalamwezi, wakaenda mpaka wakafika kwenye ngome ya Kaab, ambaye alikuwa bwana harusi aliyeoa hivi karibuni, basi Abu Naila akapiga kelele, hivyo Kaab akaruka nje salama alipoijua sauti yake, wakamfanyia usaliti na wakamuuwa, na wakachukua kichwa chake, kisha wakarudi mpaka wakafika Baqii' Al-Gharqad, wakasema Allaahu Akbar (Mwenyezi Mungu Mkubwa) na Muhammad aliposikia takbira zao, akasema Allaahu Akbar na akajua kuwa wamemuua, basi wakamjia hali amesimama na anaswali, akasema: Nyuso zimefaulu?.  

Answer

Wakasema: Uso wako ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, na wakakitupa kichwa cha Kaab mbele ya Mtume (S.A.W.)!
Tunauliza: Kwa nini Mtume wa Uislamu (S.A.W.) anawafanyia wapinzani wake usaliti kwa njia hii? Je, inafaa kumuua mtu kwa sababu tu alimpinga Mtume wa Uislamu (S.A.W.) kwa mashairi yake? Je, inafaa awakilishe binadamu mtu anayeua kwa njia hii?
Jibu la Tuhuma:
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na rehma na amani zimwendee bwana wetu Mtume wa Mwenyezi Mungu, jamaa zake, masahaba wake na wanaomfuata, na baada ya hayo:
Hadithi ya kuuawa kwa Ka’ab bin Al-Ashraf ilitajwa katika vitabu vya Sunna na Sira (1), lakini hakuna yale yaliyotajwa katika swali kwamba Mtume (S.A.W.) kichwa cha mtu huyo kilitupwa mbele yake, na muktadha huu hauna matukio halisi ambayo yaliyotokea katika swala la kunyongwa kwa Ka'b, ambayo yanaelezea sababu ambazo zilipelekea kunyongwa kwake, na kwamba aliuawa; kwa sababu yeye alikuwa msaliti, si kwa sababu yeye alikuwa Myahudi, wala kwa sababu yeye alikuwa mpinzani.
Huyu ni mtu miongoni mwa Mayahudi waliokaa Madina baada ya kufanya mapatano na Mtume (S.A.W.) ambayo yanabainisha kuwa pande zake mbili zidumishe usalama wa Madina, na kwamba pande hizi mbili hazivunji ahadi hii, wala hazidhuru usalama, lakini mara tu alipoona yaliyotokea baina ya Waislamu na watu wa Makkah katika Vita vya Badr, na jinsi vita vilivyoisha kwa kurudi kwa washirikina wakiwa dhaifu, lakini alianza kuwachochea washirikina na kuwasha moto wa chuki katika nafsi zao, na akatunga mashairi yake ili kuchochea jambo hili dhidi ya Waislamu.
Imepokelewa kutoka kwa Ibn Abbas – R.A. amesema: Alipokuja Ka’b bin Al-Ashraf Makka, walimjia na kumwambia: Sisi ni watu wa kumwagilia maji na bustani, na wewe ndiye bwana wa Yathrib, sisi ni wabora au yule mtu ambaye ni dhaifu sana (wanakusudia Mtume (S.A.W)), anayedai kuwa yeye ni mbora kuliko sisi, akasema: “Nyinyi ni wabora kuliko yeye.” Basi wahyi (Ufunuo) akateremshiwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (S.A.W) kwa Aya hii: {Hakika anaye kuchukia ndiye aliye mpungufu} [AL KAWTHER: 3], na ikateremshwa Aya hii pia: {Huwaoni wale walio pewa sehemu ya Kitabu? Wanaamini masanamu na Shet'ani! Na wanawasema walio kufuru, kuwa hao wameongoka zaidi katika njia kuliko Walio amini.} [AN NISAA: 51]
Na Ka’b hakutosheka na hilo, bali alianza kujiunga na makafiri wa Makka dhidi ya Mtume (S.A.W).” Al-Qurtubi anasema: “Waislamu Waliposhindwa kwenye Siku ya Uhud, wakawa na mashaka na wakaasi, hivyo Ka’b bin Al-Ashraf akaondoka na wapanda farasi arobaini kwenda Makka, na Maquraishi wakajiunga naye kwenye Al-Kaaba.”
Imepokelewa kutoka kwa Ikrimah R.A. kwamba Ka’b bin Al-Ashraf aliwaendea washirikina wa makafiri wa Kikureshi, hivyo akawahimiza kumvamia Mtume (S.A.W.), na akasema: Sisi tupo pamoja nanyi ili tupigane naye ().
Al-Maziri amesema: “Ka’b alivunja ahadi ya Mtume (S.A.W.),na akamlaani na kumtukana waziwazi.” Hivyo, Ka’b alikuwa mhalifu anayestahiki adhabu, na adhabu ya wahalifu ni kitu ambacho kinakubalika kwa wanadamu wote.
Kwa nini njia hii?!
Ka'b alikuwa na nafasi katika watu wake kama ile ya wahalifu wakubwa waliojikinga kupitia makabila yao, na kukamatwa kwake hali ya kuwa amezuiliwa na watu wake katika hali hii ilikuwa ni sababu ya migogoro mikubwa zaidi baina ya makundi yaliyoko Madina ambapo hapakuwa na usalama wa Madina baada yake.
Na ili kusawazisha baina ya kuepusha fitna hii kubwa zaidi na kuzima moto wa fitna iliyopo kwa sababu ya makosa yake, aliyepewa jukumu hili aliona kuwa hila ya kumkamata Ka’b ndiyo njia bora zaidi, na kwa jambo hili Muhammad bin Maslamah R.A. hakumpa Ka’b ahadi, wala hakumlinda kwa neno, bali alizungumza naye kuhusu jambo la kununua na kuuza. Akamjia Ka’b na kumwambia: Tulitaka utukopeshe wasq moja au mbili (kama kipimo), basi Ka’b akasema: “Basi wanawake wenu ni dhamana kwangu.” Wakasema: Vipi tukuwekee dhamana wanawake wetu na hali wewe ni Mwarabu mzuri zaidi? Akasema: Basi watoto wenu muwaweke rehani.” Wakasema: Vipi tutawaweka watoto wetu rehani na alaaniwe mmoja wao? Imesemwa: aliwekwa rehani wasq moja au mbili, hii ni fedheha kwetu, lakini tunaweza kukuwekea silaha rehani na akamuahidi kumjia, basi wakamuua, kisha wakaja kwa Mtume (S.A.W) na wakamwambia hivyo.
Mtume (S.A.W) aliwapa Mayahudi amani:
Na hakuna dalili ya kuwa jambo hilo si kufutilia mbali au kutokomeza kabila ambalo Mtume (S.A.W.) aliwabainishia watu kwamba kuuawa kwake kulikuwa tu kwa sababu ya kuisaliti nchi yake. na Ummah wake. Mayahudi walipofadhaishwa na kuuawa kwake, walimjia Mtume (S.A.W.) na kulalamika juu ya jambo hilo. Mtume (S.A.W.) akawakumbusha hiyana yake na yale aliyokuwa akiwachochea kupigana na kuwadhuru. Kisha akawaita waandike mapatano ya amani baina yake na wao. Akasema: Na mapatano ya amani hayo yalikuwa pamoja na Ali R.A. Na ni Wayahudi wangapi walioishi Madinah humo kwa usalama, na hawakudhurika mpaka baada ya kuvunja ahadi! Na tazama msimamo wa Mayahudi juu ya mauaji yake, jinsi ambavyo hawakumtetea na hawakupigana naye.

 

Share this:

Related Fatwas