Uhusiano wa Kiwahabi na Alkhawariji...

Egypt's Dar Al-Ifta

Uhusiano wa Kiwahabi na Alkhawariji

Question

Mawahabi ni nani? Je, wao ni Alkhawariji?

Answer

Uwahabi ni madhehebu ya Kiislamu ambayo yalizuka katika eneo la Najd la Bara Arabu chini ya mwanzilishi wake, Sheikh Muhammad bin Abd Al-Wahhab (1703 BK - 1792 BK) na ambaye Uwahabi unanasibishwa kwake. Uwahabi ulilingania mambo ambayo ndani yake ulipingana na wanazuoni wa Ahlul-Sunnah wal Jama`ah na Maimamu wao, na miongoni mwa mambo mashuhuri zaidi kati ya hayo ni: Uharamu wa kujenga Misikiti juu ya makaburi ya watu wema, na kutojuzu kuswali katika Misikiti hiyo. Uharamu wa kujenga makuba juu ya makaburi, na uharamu wa kuomba msaada kwa Manabii na watu wema waliopitia, na uharamu wa kutafuta baraka kutoka kwao, na kutojuzu kuomba dua kwa kupitia Manabii kwa Mwenyezi Mungu, na kwamba mwenye kufanya hivyo ameingia kwenye ushirikina mkubwa zaidi, na jambo hili la mwisho ni upuuzi kabisa wa waliyoyasema; Ambapo walihukumu, kwa sababu ya kauli hiyo, kuwa Waislamu wengi ni makafiri, bali waliwahukumu wanazuoni wengi na watu wema vile vile, kwa sababu wao waliruhusu yote yaliyotajwa hapo juu, na miongoni mwao kulikuwa na kundi lililokwenda mbali zaidi mpaka waliwaua watu (Kundi la Kisalafi la Kijihadi), na pengine hii ni sababu mojawapo ya kuwafananisha na Alkhawariji, kwani walikuwa wanakufurisha watu wa umma kwa sababu zisizo za kufuru, hivyo husema: Mtenda dhambi kubwa ni kafiri ambaye atakuwa motoni milele.

Share this:

Related Fatwas