Msimamo wa Mtume (S.A.W.) kwa Bibi ...

Egypt's Dar Al-Ifta

Msimamo wa Mtume (S.A.W.) kwa Bibi Aisha, (R.A.), Katika Hadithi ya Al-Ifk (Uwongo ).

Question

Matini ya Tuhuma:
Imetajwa katika Qur`ani kuhusu Hadithi ya Uwongo katika Aya hii:
{Hakika wale walio leta uwongo ni kundi miongoni mwenu. Msifikiri ni shari kwenu, bali hiyo ni kheri kwenu. Kila mtu katika wao atapata aliyo yachuma katika madhambi. Na yule aliyejitwika sehemu yake kubwa miongoni mwao, atapata adhabu kubwa} [AN NUUR: 11].
Maana ya uwongo –kufuatana na waliyoyataja wafasiri- ni yale yaliyozushwa dhidi ya Bibi Aisha (R.A.) nayo ni kwamba Mtume (S.A.W.) alimchukua katika baadhi ya misafara, hivyo akatoa idhini kwa ajili yake usiku kuondoka, na wakataja Hadithi ndefu ambayo imeelezwa kuwa baadhi ya Waislamu walizusha dhidi yake, na kwamba Mtume wa Uislamu (S.A.W.) alishauriana na Maswahaba zake, na Ali bin Abi Talib alimshauri ampe talaka, na wapo wanawake wengine wengi, na kwamba Mtume wa Uislamu (S.A.W.) hakuwa na misimamo mikali kwa Aisha, bali alikuwa akimtembelea, na akauliza kuhusu hali yake. Akiwa na huzuni na husuda juu ya yale yaliyozungumzwa juu yake, kisha akamwambia mwishoni mwa jambo: “Ama baada ya hivyo, ewe Aisha, niliambiwa hivi na hivi kuhusu wewe. Ikiwa wewe huna hatia, basi Mwenyezi Mungu atakusamehe, na ikiwa umefanya dhambi, basi omba msamaha kutoka kwa Mwenyezi Mungu na utubu kwake, kwani mja akikiri kisha akatubu, Mwenyezi Mungu atamsamehe.
Tunauliza: Je, mwenye akili timamu haoni kuwa Muhammad ni Mtume wa Uislamu (S.A.W.) akajaza Qur’ani kwa mambo yake hasa na mambo ya wake zake? Je, hili halioneshi kwamba Mtume wa Uislamu (S.A.W.) aliathiriwa na matamanio yake na kusuluhishwa katika hali mbalimbali? Basi kwa nini Qur’an ilichelewesha kipindi hiki, hivyo Mtume wa Uislamu (S.A.W.) haikumsaidia? Je, hakupaswa kushuka kumuunga mkono mara tu uvumi huo ulipoenea kuhusu mkewe?
 

Answer

Jibu la Tuhuma:
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na rehma na amani zimwendee bwana wetu Mtume wa Mwenyezi Mungu, jamaa zake, masahaba wake na wanaomfuata, na baada ya hayo:
Qur’ani Tukufu imetaja katika Aya zake nyingi usuluhisho kwa ajili ya hali za nyumba ya Mtume, na hii ni kwa ajili ya kila muumini wa Qur’ani Tukufu aweze kumuiga Mtume (S.A.W.) katika hali zake zote, hata katika hali zake za nyumbani na pamoja na wake zake.
Hadithi ya Uwongo ni dalili ya kwamba Qur’ani si kitabu cha mwanadamu:
Katika mazingira ya Waarabu, mtu hudhuriwa na madhara yoyote kutokana na shutuma kidogo zinazoathiri heshima yake, hasa ikiwa anashuku kuwa tuhuma hiyo ni kwa mke wake. Huyo Mwarabu katika hali hii, ambayo kidole cha tuhuma kinamwashiria mkewe, anatetea heshima yake tuhuma hiyo, kadiri awezavyo, wala hacheleweshi katika jambo kama hili, hasa wale wanaodai heshima au uongozi miongoni mwao. au kuwa na ushawishi fulani kwa watu wake.
Yaliyomtokea Mtume (S.A.W.) katika yale yaliyovumishwa kuhusu mke wake Aisha (R.A.) ni jambo kama hilo. Natamani kujua kwanini utetezi wa tuhuma hii ulicheleweshwa kwa mwezi mzima?!
Na lau kuwa Qur’ani ilikuwa ni uzushi wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (S.A.W.) kwa nini mwandishi wake anachelewesha na hali yake ndiyo iliyodhurika kwa kuchelewa kutetea tuhuma hii muda huu mrefu? Kwanini alichelewa kuandika jambo ambalo lingemtetea yeye na mkewe?!
Ikatokea kwamba Qur’ani iliteremshwa katika jambo lisilokuwa hili mara moja na mara moja, kama ilivyotokea katika kisa cha Khawla, ambaye Mwenyezi Mungu alisikia maneno yake alipokuwa akijadiliana na nafsi yake, hivyo wahyi ukashuka mara moja.
Hapana shaka kuwa alikuwa akingojea kitu kisichokuwa katika uwezo wake kukiteremsha au kukishusha, na lau kilikuwa mkononi mwake, hakulichelewesha mpaka ndimi za wafuasi wake zikathubutu kusambaza tuhuma hiyo kwenye mji wake, na huu ulikuwa ni Wahyi wa Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu akasema: {(Nao watasema:) Wala hatuteremki ila kwa amri ya Mola wako Mlezi. Ni yake Yeye yaliyoko mbele yetu na yaliyoko nyuma yetu, na yaliyomo katikati ya hayo. Na Mola wako Mlezi si mwenye kusahau} [Maryam: 64]
Nabii mwalimu
Na katika msimamo wake – S.A.W. – kabla ya kuteremshwa wahyi juu yake ni jambo linalobainisha utukufu wa Mtume, na kuonesha ukamilifu wa nafsi hii kwa namna isiyo ya kawaida katika tukio kama hilo, na hiyo ni kama ifuatavyo:
1- Uwiano wa kipekee uliodhihirika katika nafsi ya Mtume (S.A.W.).
Ni mume aliyedhurika na Hadithi hii, ambayo kuhusu mke wake anayempenda sana zaidi kuliko watu wote, naye ni muadilifu anayemtembelea mke wake ili kujua hali yake na kumhakikishia afya yake, na hakufuta kutoka kwa hesabu yake yaliyotangulia kutoka kwa maisha yake na uhusiano wake naye.
Aisha – R.A – anasema, anapoeleza hali yake – S.A.W.– pamoja naye katika ugonjwa wake: “Jambo linalonitia shaka katika maumivu yangu ni kwamba sioni kutoka kwa Mtume – S.A.W. - wema niliokuwa nikiuona kutoka kwake nilipolalamika, anaingia na kutoa salamu, kisha husema: Hamjambo? Kisha anaondoka. Hilo ndilo linalonitia shaka naye, na sijisikii vibaya mpaka niwe safi.” Kisha anataabika pale watu wanapozungumza kuhusu mke wake kwa namna hii, na hawezi kutoa adhabu kwa mmoja wao, kwani adhabu ya kukashifu bado haijaamuliwa katika Sharia.
2- Ni matamanio au ni taarifa ya ujumbe:
Sijui jinsi ya kuelezea kile alichosema – S.A.W.- kwa Aisha: “Ama baada ya hivyo, ewe Aisha niliambiwa hivi na hivi kuhusu wewe. Ikiwa wewe huna hatia, basi Mwenyezi Mungu atakuondoleeni, na ukitenda dhambi, basi omba msamaha kwa Mwenyezi Mungu na tubu Kwake, kwani mja akikiri kisha akitubu, Mwenyezi Mungu atamsamehe.”
Je, hii inawezaje kutafsiriwa ni kama matamnio au ni zao la matamnio?! Je, ilikuwa sawa kwake kufunga mlango wa rehema ya kimungu, wakati alipotumwa kupokea toba ya wenye kutubu? Au anamshutumu kwa tuhuma, kama watu wanavyofanya bila kujali maisha au hata kungoja ushahidi? Au ni wajibu wake kumweleza, kama alivyowaeleza wengine, anafanyaje katika kukabiliana na mtihani huo?
3- Ni matamanio au ni shauku ya hali ya juu:
Na kama ukistaajabu, basi cha ajabu zaidi ni tafsiri ya yale aliyoyasema Mtume -S.A.W.- kuhusu mke wake msafi kwamba hali ilikuwa ni matamanio ya mwili. Na yale yaliyokuwa na Aisha na hayakuwa na wanawake wengine wa Madina yanayomtofautisha na wengine, isipokuwa mapenzi yake kwake? Je, hakuwa katika uwezo wake ikiwa ni matamanio - pale aliponasihiwa na Ibn Abi Talib kuoa mwanawake mwingine - kama alivyosema – wananwake wengine ni wengi? Je, hakuweza kumwacha na kuoa wanawali wengine waliojaza jiji hilo? Je, hali hii ni kutokana na ile iliyodaiwa kuwa ni matamanio, au ni mapenzi ya mume mtukufu ambaye hakutaka kumwacha mke wake wakati wa mtihani wakati ambapo hakuna ushahidi wa yale waliyodai?  
 

Share this:

Related Fatwas