Baina ya Dauwdi na Suleiman Amani I...

Egypt's Dar Al-Ifta

Baina ya Dauwdi na Suleiman Amani Iwe Juu Yao

Question

Matini ya Tuhuma:

Ilitajwa katika Qur’ani Tukufu: {Na Dauwd na Suleiman walipo kata hukumu katika kadhiya ya konde walipo lisha humo mbuzi wa watu usiku. Na Sisi tulikuwa wenye kushuhudia hukumu yao hiyo. (78) Tukamfahamisha Suleiman. Na kila mmoja wao tulimpa hukumu na ilimu. Na tuliifanya milima na ndege kuwa pamoja na Daud imnyenyekee na imtakase Mwenyezi Mungu. Na Sisi ndio tulio fanya hayo (79)} [AL ANBIYAA: 78-79]

Answer

Na ilitajwa katika tafsiri yake kwamba watu wawili waliingia kwa bwana wetu Dauwdi, mmoja akiwa na shamba na mwingine mwenye kondoo. Mwenye shamba akasema: Kondoo huyu aliingia kwenye shamba langu usiku na akaanguka ndani yake na akaharibu bila kuacha chochote. Kwa hiyo bwana wetu Dauwdi alitoa hukumu kwake achukue kondoo pamoja na kilimo. Basi wakatoka wakapita karibu na Sulemani, naye akasema: Dauwdi alifanyaje kuhusu hukumu kati yenu? Akamwambia. Suleiman akasema: Kama ningeiona amri yako, ningehukumu vinginevyo. Imepokelewa kwamba alisema: Isipokuwa haya, kwa ajili ya upole kwa makundi mawili haya, na akamjulisha Dauwdi kuhusu hilo. Basi akamwita na kumuuliza kuhusu hukumu iliyo ni nzuri kwa makundi mawili hayo? Akasema: Kondoo hupewa kwa mwenye shamba, ili kufaidika na maziwa yake, uzao wake, sufi na manufaa yake, na mwenye kondoo humlipa mwenye shamba kama shamba lake. Shamba likiwa kama lilivyokuwa siku ile lilipoliwa, hupewa kwa mwenye shamba, na mwenye kondoo akachukua kondoo wake. Dauwdi akasema: Hukumu ndiyo ni hukumu yako, na umri wa Sulemani siku ile ulikuwa miaka kumi na moja..

Inajulikana kuwa Dauwdi, (A.S), alikuwa mmoja wa manabii, wafalme na watu wenye hekima wenye msukumo, kwa hiyo hawezi kutotatua kesi kama hii, na haifikiriki kwamba Suleiman alikuwa akifuata hukumu za baba yake. Ni wazi kwamba Qur’ani Tukufu ilimchanganya Suleiman na Absalomu, naye yeye ndiye aliyekuwa akimshutumu baba yake, na Absalomu alipoamua kumwasi baba yake, alilainisha mioyo ya wana wa Israeli na kusema: Ni nani unifanye hakimu duniani ili kuwatendea haki walioonewa! Alikuwa akimbusu, kumheshimu na kumtukuza yule, hivyo akawafanya watu wanampenda, kisha akafanya mapinduzi yaliyoshindwa dhidi ya baba yake (2 Samweli 15:1-6).

 

Jibu Lake:

Kituo cha Utafiti wa Sharia kwenye Dar Al-Ifta nchini Misri.

Kwanza: Alichokihukumu Daudi, (A.S), hakikuwa kibaya wala kupinga utume wake, wala uvuvio wake, wala ufalme wake na hekima yake. Ilikuwa ni kwa jitihada tu kutoka kwake. Ama yale aliyohukumiwa na bwana wetu Sulaiman, (A.S), ni wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu.Akasema: {Tukamfahamisha Suleiman}.Hii inaashiria kuwa ufahamu wa Suleiman juu ya kesi hiyo ulikuwa wa ndani zaidi, kwa sababu ilikuwa kwa uvuvio kutoka kwa Mwenyezi Mungu, naye alikuwa mpole zaidi kwa wale wapinzani wawili. Na Mwenyezi Mungu alitaka kumwonesha kwa baba yake ujuzi wa Sulemani ili apate kupendezwa naye zaidi na kufarijiwa na wanawe waliompoteza kabla ya kuzaliwa kwa Sulemani.

Pili: Aya inaonesha kuwa kesi iliwasilishwa kwa Daudi na Sulaiman pamoja na wakaihukumu pamoja, na hukumu ya kila mmoja wao ilikuwa ya uadilifu, huu ni ufahamu ulionyooka ambao Qur'ani Tukufu inaiweka wazi mahakama na mambo yanayopaswa kuwa juu yake, na haifahamiki katika Aya ya kwamba Sulaiman, (A.S), alikuwa akifuata hukumu za baba yake kwa kauli yake Mwenyezi Mungu: {Na Daud na Suleiman walipo kata hukumu katika kadhiya ya konde...} Aya hiyo ilionesha kuwa kesi iliwasilishwa kwao wote wawili.

Hukumu ya Daudi ilikuwa kweli kweli; Kwa sababu imeegemezwa juu ya faini ya uharibifu kwa wale waliowapuuza kondoo, na kanuni ya faini ni kuwa iwe ni fidia kamili, hivyo hukumu ilikuwa ni haki, na inakutosha kuwa ni kwa mujibu wa Sunnah imeleta kuhusu uharibifu wa mifugo.

Uamuzi wa Sulemani ulikuwa wa kweli, kwa sababu ulitegemea kuwapa haki jamaa zake, huku akiambatanisha haki na malipo ya walicho nacho kwa muda, kwa kuwa ni sawa na amani, na labda wenye kondoo hawakuwa na kondoo wingine isipokuwa hawa tu, Wapinzani hao wawili walitosheka na hukumu ya Sulemani, kwa sababu wapinzani hao wawili walikuwa watu wa uadilifu, si watu wa kukata tamaa, na kama wasingeridhika, hatima ingekuwa kwenye hukumu ya Daudi, kwa kuwa huruma si wajibu.

 Tatu: Kuhusu kauli kwamba Qur’an ilimchanganya Suleiman na Absalom, hii si sahihi. Kwa sababu aya  hii haukumzungumzia Absalomu hata kidogo, na ikiwa tunakubali hadithi ya Absalomu, hii haimaanishi kwamba inapingana na aya hii, kwa sababu aya hii inahusiana na bwana wetu Sulemani na Absalomu hauna uhusiano wowote nayo. Hadithi ya Absalomu ni hadithi nyingine isipokuwa hadithi ya Sulemani, (A.S).          [1]) Ukombozi na Mwangaza 17 / 117

 

 

 

Share this:

Related Fatwas