Ugaidi na vitisho ni maneno yanayod...

Egypt's Dar Al-Ifta

Ugaidi na vitisho ni maneno yanayodhihirisha vitendo vya unyanyasaji na hujuma zinazofanywa na watu wenye misimamo mikali

Question

Tukitaka kuelezea vitendo vya unyanyasaji na hujuma zinazofanywa na watu wenye itikadi kali, ni istilahi gani kati ya hizo mbili inayokuja kwanza, “ugaidi” au “vitisho”?

Answer

"Ugaidi" una maana ya vitisho, na ni wa aina mbili: ugaidi wa kiakili, na ni kwa njia ya Kukufurisha katika masuala madogo au katika migogoro ya kupendeza, nao kwa silaha, yaani kwa kulazimisha maoni ya itikadi kali kwa vurugu na nguvu ya silaha. Ugaidi wa kiakili hufungua njia kwa ugaidi wa kutumia silaha. Ama neno la “vitisho” pia lina maana hiyo hiyo, lakini linadhihirisha zaidi uenezaji wa hali ya msukosuko na wasiwasi unaotokana na woga. Haitakiwi “vitisho” iwe ni matokeo ya vitendo vya unyanyasaji na uharibifu tu, lakini inaweza kutokea kama matokeo ya kueneza uvumi mbaya. Neno la “vitisho” ni neno sahihi na pana zaidi, kama vile sisi hatupati upande wowote chanya kwake, kwani huwa ni neno lenye maana hasi, kwa hivyo Mwenyezi Mungu alisema: “Kama wanaafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, na waenezao fitna katika Madina hawatoacha, basi kwa yakini tutakusalitisha juu yao, kisha hawatakaa humo karibu yako ila muda mchache tu. (60) Wamelaanika! Popote watakapo onekana watakamatwa na watauliwa kabisa.(61)” (Al-Ahzab: 60, 61).  Qur’ani tukufu ikahusisha adhabu kwa aliyefanya hivyo. Kwa hiyo, tunaona kwamba neno la “vitisho” lilitumiwa kwanza, lakini kutokana na kuenea na umaarufu wa neno la “ugaidi” katika jamii na vyama vya kimataifa kama tafsiri ya neno “terrorism”, tunalikubali na kulitumia.

Share this:

Related Fatwas