Udhibiti wa uzazi

Egypt's Dar Al-Ifta

Udhibiti wa uzazi

Question

Je, ni njia gani zinaruhusiwa kisharia za kudhibiti uzazi?

Answer

Jibu: Inaruhusiwa kutumia kila njia iliyoidhinishwa na madaktari kwa ajili ya udhibiti wa uzazi, mradi inakidhi viwango vya matibabu vinavyozuia madhara ya kiafya na kufikia manufaa yanayotarajiwa kutokana na njia hiyo. Hii pia ni kwa makubaliano kati ya wanandoa. Wanachuoni wa Sharia ya Kiislamu hapo awali waliruhusu kutenga / kutoa nje mbegu za uzazi kama njia ya kuzuia mimba. Kwa sababu kutenga ilikuwa njia inayojulikana katika zama zao na kabla yao katika zama za Mtume (S.A.W), na si kwa sababu jambo hilo lilikuwa pekee. Na Mwenyezi Mungu ndiye anayejua zaidi.

Share this:

Related Fatwas