Kafara ya kiapo

Egypt's Dar Al-Ifta

Kafara ya kiapo

Question

Je, ni kiasi gani cha kafara ya kiapo? Je, inajuzu kutoa thamani?

Answer

Kiapo kinachoweza kutolewa kafara yake ni kiapo cha “Ghamuws”  (Ya Uongo Ili Kudhulumu Haki Ya Mtu), Kiapo cha “Muna’qidah” (Cha kweli kweli kwa makusudi) kinachoweza kuvunjika. Lakini kafara ya kuvunja kiapo cha “Laghu” (Cha upuuzi) haiwajibika.

Kafara ya kuvunja kiapo ni kuwalisha masikini kumi, au kuwavisha nguo, basi asiyeweza kupata basi afunge siku tatu, kwa mujibu wa kauli yake Mwenyezi Mungu: “Mwenyezi Mungu hatakushikeni kwa viapo vyenu vya upuuzi, lakini atakushikeni kwa mnavyo apa kweli kweli kwa makusudio. Basi kafara yake ni kuwalisha masikini kumi kwa chakula cha wastani mnacho walisha ahali zenu, au kuwavisha, au kumkomboa mtumwa. Asiye pata hayo, basi afunge siku tatu. Hii ndiyo kafara ya viapo vyenu mnapo apa. Na hifadhini yamini zenu. Namna hivyo Mwenyezi Mungu anakubainishieni Aya zake ili mpate kushukuru” [Al-Ma 'idah: 89].

Kafara ya kuvunja kiapo inakadiriwa na uzani wa Swai’ katika chakula kikuu cha watu wengi kama ngano au mchele, kwa mfano, kwa kila masikini moja miongoni mwa masikini kumi, kama ilivyokuwa mtazamo wa wanachuoni wa madhehebu ya Hanafi. Swai' inakadiriwa na uzani wa ngano karibu (2,500) kg, na kwa mchele wa Misri karibu (2,750) kg.

Wanachuoni wa madhehebu ya Shafi’ wanashikilia kuwa ni wajibu kutoa Mud kutoka kwa watu wengi wa nchi, na Mud ni sawa na robo ya Swai', na kiasi chake ni takriban gramu (510) kwa kila masikini moja.

Ikiwa ni vigumu kwake kufanya kazi kulingana na madhehebu ya Imamu Abu Hanifa, hakuna ubaya kwake kufanya kazi kulingana na madhehebu ya Imamu Asha-Shafi.

Inajuzu kutoa mchele au ngano yenyewe, na inajuzu pia kutoa thamani ya moja kati ya hizo kwa masikini. Nacho ni kiasi cha kulisha masikini moja kwa kufungua siku moja katika kafara ya kufunga saumu, lakini kiasi hiki kinazidishwa mara kumi. Na Mwenyezi Mungu pekee ndiye Anayejua Zaidi.

Share this:

Related Fatwas