Kafara ya kiapo

Egypt's Dar Al-Ifta

Kafara ya kiapo

Question

Ni kiasi gani cha kafara ya kuapa kiapo? Je, inajuzu kulipa kwa thamani?

Answer

Tunaweza kutoa kafara kwa kiapo cha Ghamuus (yaani kiapo cha kujitokomeza Motoni haraka haraka), na kiapo kilichofungika (ni yamini ya kweli kweli inayochukuliwa kwa kukusudiwa jambo la baadae) ambacho mtu anakivunja. Ama kiapo cha upuuzi  (kiapo cha upuuzi kipitacho katika ulimini wa Muislamu/mtu bila ya kukusudia) hakitakiwi kafara.

Kafara ya kiapo ni kuwalisha masikini kumi, au kuwavisha, asiye na uwezo basi afunge siku tatu.” Mwenyezi Mungu Mtukufu akasema: “Mwenyezi Mungu hatakushikeni kwa viapo vyenu vya upuuzi, lakini atakushikeni kwa mnavyo apa kweli kweli kwa makusudio. Basi kafara yake ni kuwalisha masikini kumi kwa chakula cha wastani mnacho walisha ahali zenu, au kuwavisha, au kumkomboa mtumwa. Asiye pata hayo, basi afunge siku tatu. Hii ndiyo kafara ya viapo vyenu mnapo apa. Na hifadhini yamini zenu. Namna hivyo Mwenyezi Mungu anakubainishieni Aya zake ili mpate kushukuru. ” [Al-Maida: 89].

Kafara ya kuapa inakadiriwa kuwa kipimo katika sehemu kubwa ya chakula kikuu cha watu wa nchi, kama vile ngano au mchele, kwa mfano, kwa kila masikini kumi, kama wanavyoshikilia wanavyuoni wa madhehebu ya Hanafi, na kipimo hicho  kinakadiriwa kwa uzani wa ngano karibu (2,500) kg, na kwa mchele wa Misri takriban (2,750) kg.

Wanavyuoni wa Madhehebu ya Shafi wanashikilia kuwa ni wajibu kulipa kipimo kutoka kwa watu wengi wa chakula cha nchi, na kipimo hicho ni takriban gramu (510) kwa kila masikini.

Ikiwa ni vigumu kwake kufanya kazi kwa mujibu wa Madhehebu ya Hanafi, hakuna lawama kwake kufanya kazi kwa mujibu wa madhehebu ya Shafi.

Inajuzu kutoa mchele au ngano yenyewe, na inajuzu kuwapa masikini thamani ya chochote kati yao, ambacho ni kiasi cha kumlisha masikini kwa kifungua kinywa cha siku hiyo kwa kafara ya saumu, lakini kiasi hiki kinazidishwa na kumi. Na Mwenyezi Mungu ndiye anayejua zaidi.

Share this:

Related Fatwas