Swala ya Haja

Egypt's Dar Al-Ifta

Swala ya Haja

Question

Swala ya Haja ni nini, na nini hukumu yake, na inafanywaje?

Answer

Swala ya Haja ni imependekezwa, na inaswaliwa rakaa mbili ndani yake inasomwa Al-Fatiha na sura yoyote kutoka katika Qur’ani Tukufu, kisha anamhimidi Mwenyezi Mungu, kisha anamswalia Mtume, (S.A.W), kisha anaomba dua iliyotajwa katika Sunna.

Swala ya Haja ni ile inayoswaliwa kwa ajili ya kupata haja, na Wanachuoni wa Fiqhi walio wengi wanasema kuwa Swala hii imependekezwa, na huswaliwa rakaa mbili ambazo husomwa ndani yake surat Al-Fatiha na sura yoyote kutoka Qur’ani Tukufu baada yake, basi hiyo. inafuatiwa na kumsifu Mwenyezi Mungu Mtukufu na kumswalia Mtume, (S.A.W), kisha anamuomba Mwenyezi Mungu kwa dua hii iliyopokelewa kutoka kwa Mtume, (S.A.W), ambaye amesema ndani yake: “Hakuna Mungu mwingine anaestahiki kuabudiwa isipokuwa Wewe Mwenyezi Mungu uliye Mpole uliye Mkarimu. Ametakasika Mwenyezi Mungu Mtukufu, Mola wa Arshi Tukufu. Sifa zote Njema ni zake Bwana wa Viumbe vyote. Ninakuomba vinavyopelekea kuzipata Rehma zako  na Msamaha wako ulio na malipo ya kila jema, na kusalimika na kila kosa, usiniache na dhambi isipokuwa umenisamehe, wala usiniache na jambo zito isipokuwa umeniondoshea, wala haja yoyote uiridhiayo isipokuwa umenipatia, na kunirahisishia ewe Bwana wa Viumbe vyote, ewe Mpole wa Wapole.

 (Imepokelewa kutoka kwa Al-Tirmidhiy na Ibn Majah).

Hadithi hii inabainisha idadi ya rakaa zake, namna ya kuswaliwa kwake, na dua iliyosemwa ndani yake.

Share this:

Related Fatwas