Swala ya kutubu

Egypt's Dar Al-Ifta

Swala ya kutubu

Question

Ni ipi hukumu ya Swala ya kutubu? Na inaswaliwa wakati gani?

Answer

Imepokelewa kutoka kwa Abu Bakr, (R.A), amesema: Nimemsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (S.A.W) akisema: “Yeyote afanyaye dhambi kisha akatawadha, kisha akaswali, kisha akamwomba Allah msamaha,  humsamehe.” Kisha akasoma Aya hii: {Na ambao pindi wafanyapo uchafu au wakajidhulumu nafsi zao humkumbuka Mwenyezi Mungu na wakamwomba msamaha kwa dhambi zao} [Al-Imran : 135] Imepokelewa kutoka kwa Al-Tirmidhiy katika Sunan yake.

Hadithi hii inaashiria uhalali wa Swala ya kutubu, na imependekezwa kwa maafikiano ya madhehebu manne.Inapendekezwa kwa Muislamu, akitenda dhambi, kutawadha na kutawadha vizuri, kisha aswali rakaa mbili ambazo ndani yake anajitahidi kuuweka moyo wake katika akili na kunyenyekea kwa Mwenyezi Mungu, kisha amuombe msamaha Mwenyezi Mungu, basi Mwenyezi Mungu Mtukufu atamsamehe kwa rehema, na ni lazima pia afanye hivyo, anatimiza masharti ya toba kwa kujutia dhambi na kuazimia kutoifanya tena, hata ikiwa inahusiana na haki ya mwanadamu ni bora kuirudisha haki hii kwake. Na Mwenyezi Mungu ndiye anayejua zaidi.

Share this:

Related Fatwas