Mikopo ya Vijana kwa Maendeleo na U...

Egypt's Dar Al-Ifta

Mikopo ya Vijana kwa Maendeleo na Uwekezaji yenye Riba

Question

Tunayo heshima kubwa kukujulisha kuwa Chama kiko mbioni kuchukua nafasi ya Mfuko wa Jamii katika mchakato wa mikopo ya vijana kwa maendeleo na uwekezaji. Mikopo hii hutolewa kwa viwango vya riba vya masharti nafuu vya takriban asilimia 10, ambayo ni chini ya viwango vya riba vya benki.

Tunatumai unaweza kutufahamisha kuhusu uhalali wa mikopo hii, kwa sababu tunatafuta kufanya matendo mema kwa manufaa ya vijana, tukitafuta radhi za Mwenyezi Mungu. Tafadhali kumbuka kuwa asilimia 10 inagawanywa kama ifuatavyo:

- Asilimia tano kwa Mfuko wa Jamii.

- Asilimia nne kwa Chama, itumike kwa yatima, masikini, wagonjwa, ajira, na gharama za utawala.

- Asilimia moja kwa makampuni ya bima, ambayo kulipa kwa wale wasioweza kulipa.

Tunatumai utaipatia Jumuiya Fatwa sahihi ya kisharia ambayo kulingana na msingi wake tusonge mbele na mradi huu ikiwa inaruhusiwa, au kuufuta ikiwa ni haramu. Mwenyezi Mungu Mtukufu akujaalie kuwa ni taa, nuru, na muongozo kwetu katika njia ya haki, kwa kufuata sharia ya Mwenyezi Mungu, na kushikamana na kamba madhubuti ya Mwenyezi Mungu, tukifuata nyayo za kipenzi cha Mtume Muhammad (S.A.W).

Answer

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na rehma na amani zimwendee bwana wetu Mtume wa Mwenyezi Mungu, jamaa zake, Maswahaba wake na wanaomfuata. Na baada ya hayo:

Unachokiita mikopo kinafafanuliwa kisharia kuwa ni mikataba ya fedha kati ya chama na vyama vingine, yaani vijana wanaoendesha miradi hiyo, na mikataba ya ufadhili wa uwekezaji kati ya benki, mashirika ya umma, au vyama kwa upande mmoja, na watu binafsi au taasisi kwa upande mwingine—ambapo malipo yanaamuliwa kulingana na upembuzi yakinifu wa miradi na uwekezaji mbalimbali—kwa hakika ni mikataba mipya inayofanikisha maslahi ya vyama vyao. Fatwa ni kwamba inajuzu kuunda mikataba mipya ambayo haikutajwa katika Fiqhi ya kurithi, maadamu iko mbali na shaka na madhara na kufikia maslahi ya vyama vyao. Kama alivyoipendelea Sheikh Al-Islam Ibn Taymiyyah na wengineo pia.

Vyombo vya kisharia kama vile serikali, mashirika ya umma na vyama vina sheria ambazo ni tofauti na zile za mashirika asilia. Wanachuoni wa Fiqhi wamezingatia maeneo manne ya kubadilisha sheria, ikiwa ni pamoja na kubadili sheria kwa kuzingatia asili ya watu binafsi. Wamethibitisha, kwa mfano, kwamba zaka haitozwi kwenye wakfu, misikiti, na hazina ya umma, na kwamba inajuzu kukopa kutoka wakfu kwa faida inapobidi.

Ni muhimu kabisa kutoita mkataba huu mkopo. Kwa sababu hii inaleta mkanganyiko na kanuni kwamba "kila mkopo unaoleta faida, basi ni riba."

Kwa hiyo, mnachofanya kinaruhusiwa kwa sharia ya Kiislamu. Hakika, inachukuliwa kuwa tendo la hisani ambalo utalipwa, kama malipo ya kuwezesha maisha ya vijana na kuwasaidia kuanzisha miradi yenye tija inayosaidia maisha yao na kunufaisha jamii zao.

Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ni Mjuzi Zaidi.

Share this:

Related Fatwas