Fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Vijana kwa Miradi
Question
Tunaomba rai (ya Uislamu) kuhusu fedha zinazotolewa kwa vijana na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii na Benki kwa ajili ya miradi ya vijana, ingawa zinarudishwa na riba.
Answer
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na rehma na amani zimwendee bwana wetu Mtume wa Mwenyezi Mungu, jamaa zake, Maswahaba wake na wanaomfuata. Na baada ya hayo:
Muamala na Benki ni dhana mpya ambayo haikuwepo zama za sharia za mwanzo, wala zama za Maswahaba na waliowafuata. Hakuna maandiko kuhusu kuruhusiwa au kukatazwa kwake. Bali, ilikuwa chini ya tafsiri na ufahamu wa Wanachuoni wa Kiislamu. Kwa hiyo, maoni yao yalitofautiana kuhusiana na miamala hii ya kibinadamu, kati ya wale walioruhusu na wale waliokataza, kila mmoja kulingana na mtazamo wake wa maandiko ya sharia na tafsiri yake mwenyewe. Kinachotakiwa kwa uchunguzi makini wa kanuni za kisharia za Kiislamu na ari yake ni kwamba sharia ya Kiislamu imeegemezwa katika kulinda maslahi na mahitaji ya watu. Kwa hiyo, shughuli hii iliyoanzishwa hivi karibuni lazima iwe na hukumu na kanuni zinazowiana na sharia ya Kiislamu yenye usamehevu, inayotaka kupanuka kwa upeo mpana zaidi. Kwa mtazamo huu, ikiwa mtu anayefanya muamala na Benki anakusudia kwa muamala huo mkopo, deni, au amana, basi haijuzu kwake kuchukua kutoka Benki zaidi ya kiasi alichowapa. Benki lazima irudishe mkopo, deni, au amana bila nyongeza yeyote. Vitu hivi lazima virudishwe vyenyewe au thamani yake ikiwa ni ya thamani, au sawa na ikiwa bidhaa mfanano. Hii ni kwa sababu ongezeko lolote juu ya kiasi kilicholipwa huchukuliwa kuwa ni riba, jambo ambalo limekatazwa na sharia ya Kiislamu, kwa kuzingatia kwamba fedha zimekuwa za thamani na si za bidhaa mfanano. Hata hivyo, ikiwa mtu anayefanya muamala na Benki anakusudia Benki kuwa wakala wake kamili na akakubali kile ambacho Benki imekiainisha, au ikiwa anakusudia kupitia muamala huu Benki iweze kuwekeza fedha hizo kwa ajili yake katika yale aliyoruhusu Mwenyezi Mungu, na faida hiyo itabainishwa mapema kwa muda na kiasi, basi kubainisha faida hiyo mapema ni haramu kwa baadhi ya Wanachuoni wa Fiqhi wanaosema kuwa ni haramu.
Wengine wanaamini kuwa inajuzu kwa mujibu wa Sharia, kwa sababu muamala na nia ya kuwekeza katika hati za uwekezaji na kadhalika hauko chini ya aina yeyote ya mkataba uliotajwa. Ni muamala wa manufaa kwa watu binafsi na jamii, na haihusishi unyonyaji, ulaghai, udanganyifu au ukosefu wa haki kutoka kwa upande mmoja hadi mwingine. Au ni aina ya Mudharaba wa halali, na kubainisha faida mapema hakuzuii kuwa Mudharaba, kwa sababu ni aina ya ahadi ya kufikia jina hili wakati wa kuingia mkataba, kutegemea kuwa tukio la kawaida katika miamala kama hii kupata faida katika miamala iliyotokea kabla ya muamala huu. Ahadi ni ya lazima kwa mujibu wa baadhi ya Wanachuoni wa Fiqhi, kama ilivyo Madhehebu ya Imamu Malik na wale wanaokubaliana nayo. Kwa sababu kuweka wazi huku hakukatazwi na Qur`ani Tukufu wala Sunna ya Mtume Wake (S.A.W) na kwa kuwa ni ahadi ya kutekeleza yale yaliyoafikiwa wakati hakika yatatimizwa mwishoni mwa mwaka, bali maelezo haya yanaweza kuhitajika kutatua mizozo baina ya watu katika miamala yao, na ili kila mtu ajue haki yake. Mudharaba, kama wanavyosema baadhi ya Wanachuoni wa Fiqhi, ni kwa mujibu wa makubaliano ya washirika. Ikiwa mmiliki wa pesa hakuwa na sehemu maalumu ya faida, mshiriki wake angedhulumiwa. Maadamu mapatano haya hayapingani na maandiko kutoka katika Qur`ani Tukufu au Sunna za Mtume (S.A.W) basi hakuna pingamizi katika sharia ya Kiislamu.
Idara ya Fatwa inachagua maoni ya pili na inaamini kuwa kupitisha maoni hayo ni sahihi zaidi kulinda maslahi ya watu. Ali Ibn Abi Talib alifanya mafundi ni wadhamini katika zama zake, ingawa kanuni ya asili hawakuwa wadhamini. Kwa sababu fundi ni mwaminifu, na mwaminifu hatakuwa mdhamini. Kanuni hii ilitumika wakati wa zama za Mtume wa Mwenyezi Mungu (S.A.W), na zama za Abu Bakr, Umar, na Uthman. Kisha Ali (R.A) akawadhamini, baada ya kuwa hawakuwa wadhamini hapo awali, na baada ya kutakiwa tu kula kiapo pale walipodaiwa kuwa wamejipatia mali na kuzinyima, au kudai kuwa wanadeni la bidhaa kwa wamiliki wao na kuwapinga au walidai kuwa wamezikabidhi kwa watu wake. Hili linatokana na kauli ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (S.A.W): “Ushahidi ni wa mwenye kudai na kiapo ni cha mwenye kupinga.” Ali aliwadhamini mafundi katika zama zake, kinyume na kanuni iliyotumika katika zama za Mtume wa Mwenyezi Mungu (S.A.W) na masahaba zake. Hii ilikuwa ni kwa sababu Ali alizingatia mabadiliko ya mazingira ya zama, na kile alichokiona cha udhaifu wa uadilifu wa baadhi ya watu na upotevu wa mali ya wamiliki wao. Ili kupata uadilifu miongoni mwa watu, Ali aliwadhamini mafundi katika zama zake. Idara ya Fatwa nchini Misri ilishikilia kwamba ikiwa riba iliyoainishwa inakusudiwa kuwa faida na kurudi kwa fedha zilizowekezwa katika kile ambacho Mwenyezi Mungu ameruhusu, basi hakuna pingamizi juu yake katika sharia ya Kiislamu.
Kuhusiana na swali hilo, madamu Mfuko wa Jamii unatoa pesa kwa vijana, na benki pia kutoa miradi ya vijana, basi hii inaruhusiwa kwa mujibu wa sharia za Kiislamu, na hakuna ubaya wowote. Hii ni kwa sababu inahama kutoka katika nyanja ya riba, iliyoharamishwa na sharia ya Kiislamu, kwenda kwenye nyanja ya uwekezaji, maendeleo, na biashara, ambayo inaruhusiwa na hakuna ubaya katika hili. Inachukuliwa kuwa ni aina ya ushirikiano katika uadilifu na uchamungu, kama alivyoamrisha Mwenyezi Mungu katika kauli yake isemayo: {Na saidianeni katika wema na uchamngu. Wala msisaidiane katika dhambi na uadui}, maadamu miradi hii kwa kawaida hutoa faida, ambayo Benki inachukua sehemu yake.
Kutokana na hilo, jibu la swali linakuwa wazi.
Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ni Mjuzi zaidi.
Arabic
Englsh
French
Deutsch
Urdu
Pashto
Hausa
