Hukumu ya kusafiri kwa mwanamke kwa...

Egypt's Dar Al-Ifta

Hukumu ya kusafiri kwa mwanamke kwa ajili ya kuhudhuria mikutano ya kitaaluma bila ya kuwa na maharimu

Question

Ni nini hukumu ya kusafiri kuhudhuria mikutano kwa ajili ya dada yangu ambaye ni profesa katika Chuo cha Tiba, na atasafiri bila maharimu? Je, ni hukumu gani na masharti gani yanayohitajika kwa safari yake ili aepukane kuangukia dhambi? Jua pia kuwa ana umri wa zaidi ya miaka arobaini na tano.

Answer

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na rehma na amani zimwendee bwana wetu Mtume wa Mwenyezi Mungu, jamaa zake, Maswahaba wake na wanaomfuata. Na baada ya hayo:

Asili ya kusafiri kwa mwanamke ni kusafiri akiwa na maharimu wake; kama ilivyo katika Hadithi ya Ibn Abbas R.A.: "Mwanamke asisafiri isipokuwa akiwa na maharimu, na mtu asiingie kwake isipokuwa akiwa na maharimu."

Hata hivyo, baadhi ya wataalamu wa Fiqhi wa Madhehebu ya Maliki na wengine wamekubaliana kuwa mwanamke anaweza kusafiri peke yake ikiwa njia ni salama, na maeneo anayoenda ni salama pia; hii ni kwa mujibu wa Hadithi ya Uday bin Hatim (R.A.) ambapo Mtume (S.A.W.) alisema: "Ikiwa maisha yako yatadumu mpaka uone mnyama wa Dhua’ina akitoka Hira hadi atakaposafiri na kuzunguka Kaaba, hutaogopa mtu yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu."

Katika riwaya ya Imamu Ahmad alisema: "Naapa kwa yule ambaye nafsi yangu iko mikononi mwake, ningetaka Mwenyezi Mungu afanikishe hili hadi Dhua’ina atoke Hira akizunguka Kaaba bila ya kuogopa mtu yeyote."

Hukumu ya kusafiri bila maharimu imesababishwa na hali ya kutokuwa na usalama wa njia, na inaweza kuzingatiwa kwa sababu ya urahisi na upana wa dini, lakini masharti ni kuwa kusafiri kunakubaliwa kwa idhini ya mume ikiwa mwanamke ana mume, au kwa idhini ya wali wake ikiwa hana mume.

Kwa hivyo, katika suala lako, dada yako anaweza kusafiri bila maharimu wake ikiwa kuna usalama, kwa mujibu wa mtazamo wa wataalamu wa Fiqhi waliokubali hilo.

Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ni Mjuzi Zaidi

Share this:

Related Fatwas