Je, kuswali katika Misikiti yenye m...

Egypt's Dar Al-Ifta

Je, kuswali katika Misikiti yenye makaburi ni halali au haramu?

Question

Je, kuswali katika Misikiti yenye makaburi ni haramu?

Answer

Kuswali katika Misikiti yenye makaburi ya mawalii na watu wema kunajuzu kisharia, na ni jambo linalopendekezwa.

Na wala isifahamike kuwa kauli ya Mtume (S.A.W): “Mwenyezi Mungu amewalaani Mayahudi na Manasara; waliyafanya makaburi ya Manabii wao kuwa Misikiti” kuwa kuswali katika Misikiti yenye makaburi ni haramu. Hiyo ni kwa sababu maana ya kuyafanya makaburi kuwa Misikiti iliyotajwa katika Hadithi ni kumsujudia aliyezikwa kaburini kwa nia ya kumtukuza na kumuabudu, kama wanavyofanya washirikina kwa masanamu na miungu yao. Kwa hiyo, hakuna kosa kwa Muislamu kuswali katika Misikiti yenye makaburi ya baadhi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu na watu wema.

Maelezo

Kumekuwa na khitilafu nyingi kuhusu suala la kuswali katika Misikiti yenye makaburi au madhabahu[1], na sababu ya hilo ni kutoelewa ipasavyo baadhi ya Hadithi za Sunna ya Mtume (S.A.W)  miongoni mwazo ni kauli ya Mtume (S.A.W):“Mwenyezi Mungu amewalaani Mayahudi na Manasara; waliwafanya makaburi ya Manabii wao kuwa Misikiti” (Imepokelewa na Al-Bukhari).

Wale waliodai kuwa ni haramu kuswali katika Misikiti yenye makaburi walitumia Hadithi hii kama hoja, wakasema kuwa maana ya “kuyafanya makaburi kuwa Misikiti” ni kumsujudia aliyezikwa kaburini kwa nia ya kumtukuza na kumuabudu, kama wanavyofanya washirikina kwa masanamu na miungu yao.

Ufahamu huu sio sahihi; kwa sababu maana ya “kulifanya kaburi kuwa Msikiti” ni kulifanya kaburi lenyewe kuwa mahali pa kusujudia, na mtu akamsujudia maiti aliyomo kaburini kwa nia ya kumuabudu, kama wafanyavyo wasiokuwa Waislamu. Mwenyezi Mungu anasema: “Waliwafanya wanazuoni wao na watawa wao kuwa miungu badala ya Mwenyezi Mungu, na pia Masihi mwana wa Maryam, ilhali hawakuamrishwa ila wamuabudu Mungu Mmoja tu. Hapana mungu isipokuwa Yeye. Ametakasika na wanachomshirikisha” [At-Tawbah: 31].

Hiyo ndiyo maana ya kusujudia iliyosababisha laana.

Au maana ya “kulifanya kaburi kuwa Msikiti” inaweza kuwa ni kulifanya kaburi liwe Qibla katika Swala badala ya Qibla halali, nayo ni Al-Ka‘bah.

Hayo ndiyo namna ambayo iliyofahamika na Wanazuoni wa Kiislamu kuhusu katazo la kuyafanya makaburi kuwa Misikiti. Kwa sababu hiyo, Wanazuoni wamesema kuwa kuswali katika Misikiti yenye makaburi au madhabahu kunajuzu, na wametolea hoja zifuatazo:

1- Kauli ya Mwenyezi Mungu: “Wakasema: Wajengeeni juu yao jengo. Mola wao ndiye anayewajua zaidi. Wakasema wale waliokuwa na mamlaka juu ya jambo lao: Bila shaka tutawajengea juu yao msikiti” [Al-Kahf: 21].

Katika Aya hii kuna maelezo ya mambo mawili.

Kwanza: Inajuzu kujenga Misikiti juu ya makaburi ya watu wema.

Pili: Uhalali wa kuswali katika Misikiti hiyo, kwani Aya imekuja katika muktadha wa kuisifu amali hiyo. Hili ndilo walilolielewa Wanazuoni kutoka katika kauli ya Mwenyezi Mungu: “Bila shaka tutawajengea juu yao msikiti.”

2- Kauli ya Mtume (S.A.W):“Katika Msikiti wa Al-Khayf kuna kaburi la Manabii sabini[2].” Na vilevile kitendo cha Abu Jandal bin Suhail bin ‘Amr, aliyemzika Abu Basir (R.A) alipofariki, na akajenga juu ya kaburi lake Msikiti katika (Seif Al-Bahr). Hilo lilifanyika katika zama za Mtume ((S.A.W)  na mbele ya Maswahaba mia tatu[3].

Kitendo hicho cha Abu Jandal hakikuwa kimefichika kwa (S.A.W), hata hivyo vitabu vya Sunna havikutuhadithia kwamba Mtume (S.A.W) aliagiza makaburi hayo yafukuliwe na kuondolewa kutoka Msikiti wa Al-Khayf au Msikiti Mtakatifu.

3- Hadithi ya Mtume (S.A.W)“Hakuna Nabii aliyewahi kuzikwa isipokuwa mahali alipofariki[4].” Mtume (S.A.W) alizikwa katika chumba ambacho Bi. Aisha (R.A) alikuwa akiishi humo na akiswali humo Swala zake za faradhi na sunna.

Ama kauli ya baadhi ya watu: “Hadithi hii ni mahsusi kwa Mtume (S.A.W)   peke yake”, si sahihi; kwa kuwa hakuna dalili inayoonesha kuwa kuzikwa kwa namna hiyo ni maalumu kwa Mtume (S.A.W) peke yake. Hakika Sayyiduna Abu Bakr na Sayyiduna ‘Umar (R.A) walizikwa pia katika chumba hicho. Hilo ikawa ni hoja wa Wanazuoni (Ijmaa) ya Maswahaba (R.A) juu ya uhalali wake.

4- Hoja wa Wanazuoni wa Kiislamu juu ya usahihi wa kuswali katika Msikiti wa Mtume (S.A.W), na Misikiti mingine yenye makaburi, bila ya yeyote kulikataa jambo hilo.

Tunapata faida kutokana na yaliyotangulia:

Kuswali katika Misikiti yenye makaburi na madhabahu ni sahihi, na kauli ya kuharamisha kuswali humo au kudai ubatilifu wa Swala ni kauli batili isiyo na dalili.

 

[1] Adh riha ’: ni wingi wa ‘Zarih’, ambalo ni jengo lenye umbo maalum lililojengwa juu ya kaburi la mtu fulani ili kumtambulisha; na zarīh inaweza kuwa imeunganishwa na msikiti au isiyo imeunganishwa.

[2] “Imepokewa na At-Tabarani katika Al-Mu‘jam Al-Kabir (12/414).”

[3] “Imepokewa na ‘Abdur-Razzaq katika Musannaf wake.”

[4] “Imepokewa na Imam Malik katika Al-Muwatta.

Share this:

Related Fatwas