Hukumu ya kugushi cheti cha daktari ili kupata likizo kazini
Question
Ni ipi hukumu ya kugushi cheti cha daktari ili kupata likizo kazini?
Answer
Mfanyakazi anayeghushi vyeti vya daktari ili kupata likizo kazini anatenda dhambi kulingana na Sharia ya Kiislamu. Vilevile, daktari anayepuuzia na kuandika ripoti za uongo kama hizo, akijua kuwa si za kweli na haziendani na usahihi wa ugonjwa wa mtu, anakuwa na hatia ya kuvunja amana, jambo ambalo ni dhambi kulingana na Sharia ya Kiislamu na pia ni kosa la jinai.
Maelezo
Si halali kwa mfanyakazi kugushi vyeti vya daktari ili kupata likizo kazini kwa sababu zifuatazo:
Inapingana na amri ya Mwenyezi Mungu ya kuwa mkweli kwa maneno na matendo. Mwenyezi Mungu Anasema: { Enyi mlio amini! Mcheni Mwenyezi Mungu, na kuweni pamoja na wakweli} [At-Tawbah: 119].
Mtume (S.A.W) amesema: "Shikamaneni na Ukweli, kwani ukweli huongoza kwenye wema, na wema huongoza Peponi. Mtu ataendelea kuwa mkweli na kutafuta ukweli hadi aandikwe kwa Mwenyezi Mungu kama mkweli. Jihadharini na uongo, kwani uongo huongoza kwenye maovu, na maovu huongoza Motoni. Mtu ataendelea kudanganya na kutafuta uongo hadi aandikwe kwa Mwenyezi Mungu kama mwongo." Imepoklewa na Bukhary na Muslim.
Kutafuta ukweli kunamaanisha kufanya uchunguzi sahihi wa kimatibabu unaoonesha waziwazi hali ya kiafya ya mtu, hasa ikiwa hii inaathiri haki za wengine. Kitu chochote kinachokinzana na hili kinachukuliwa kuwa ni uongo, ambao umeharamishwa katika Uislamu.
2- Kutoa vyeti vya matibabu vya uongo ambavyo havioneshi hali halisi ya kiafya ya mgonjwa ni aina ya ushahidi wa uongo, ambayo ni kuwasilisha uongo kama ukweli. Hiki ndicho hasa daktari anachofanya anapofanya udanganyifu kwenye cheti cha matibabu cha mgonjwa. Mtume (S.A.W) amelifanya uzito kosa la ushahidi wa uongo, Abu Bakrah (R.A) amesema: "Tulikuwa kwa Mtume (S.A.W) akasema: 'Je, nikuambieni dhambi tatu kubwa zaidi? Ni: kumshirikisha Mwenyezi Mungu, kuwatendea wazazi wako uovu, na ushahidi wa uongo.'" Au uongo. Mtume (S.A.W) alikuwa ameegemea, akakaa na kuendelea kuurudia hadi tukasema, "Tulitamani anyamaze."
3- Kazi iliyokabidhiwa kwa mtu ni amana ambayo anawajibika kuifanya; na dai lake la ugonjwa kwa kuwasilisha ushahidi wa uongo ni usaliti wa amana hiyo kwa kushindwa kutekeleza kazi aliyokuwa amekabidhiwa. Hii ni kwa sababu uhusiano kati ya mfanyakazi na mwajiri wake, iwe wa serikali au binafsi, ni uhusiano wa ajira; yaani mfanyakazi ameajiriwa na mwajiri.
Daktari anayetoa cheti cha ugonjwa ni mshauri kuhusu nani anayestahili kupata likizo kazini; katika Hadithi: (Mshauri amewekewa amana); lazima awe mwaminifu katika ushahidi wake na mwaminifu katika ripoti yake.
Tunapata faida kutokana na yaliyotangulia:
kwamba ni haramu kwa mfanyakazi kufanya udanganyifu katika vyeti vya matibabu kwa sababu ni kwenda kinyume na Sharia, na anayefanya hivyo, na yule anayemsaidia katika kitendo hiki anapata dhambi kulingana na Sharia ya Kiislamu.
Arabic
Englsh
French
Deutsch
Urdu
Pashto
Hausa
