Zaka ya mashirika (makampuni) ya watu binafsi na namna ya kuitoa
Question
Mimi ni mshirika katika mashirika ya watu binafsi, na shughuli yake ni biashara. Asilimia yangu katika mtaji wake ni 25%. Je, zaka inahesabiwa kwa mali yote ya shirika, au kwa sehemu yangu tu? Na ikiwa Zaka itahesabiwa kwa mali ya shirika/kampuni, je, hiyo inanitosheleza mimi pia?
Answer
Zaka katika mashirika/kampuni ya watu binafsi, kwa aina zake zote, ni wajibu kwa washirika wenyewe kwa mujibu wa maagizo ya kisharia, kila mmoja kwa sehemu yake na kwa kadiri ya umiliki wake, iwapo atakuwa anamiliki kiasi cha Zaka kwa umiliki kamili, kilicho zaidi ya mahitaji ya msingi na kisicho na deni.
Maelezo
Zaka ni ibada ya lazima na nguzo miongoni mwa nguzo za Uislamu. Na miongoni mwa malengo yake na hekima ya kuwekewa kwake ni kuziba mahitaji ya masikini, kutakasa nafsi ya mtoaji kutoka kwenye tamaa na uchoyo, na kuzuia kujilimbikizia mali. Mwenyezi Mungu anasema: “Chukua kutoka kwa mali zao sadaka ambayo itawatakasa na kuwasafisha kwayo.” [Tawba: 103] Mashirika/makampuni ya watu binafsi ni chombo cha kisharia kinachoidhinisha ushirikiano wa watu kadhaa kwa nafasi zao binafsi kwa lengo la kufanya shughuli ya kibiashara, na kugawana faida au hasara kati yao kwa mujibu wa hisa zao, kama ilivyoelezwa katika vifungu vya 505 na 506 vya Sheria ya Kiraia ya Misri.
Shirika hapa hukusudia kuwa ni chombo chenye hadhi ya kisheria na dhamana ya kifedha inayojitegemea, inayoiwajibisha kwa haki na majukumu kwa taasisi na watu wengine, bado haikusudiwi moja kwa moja na agizo la kisharia la utoaji wa zaka. Bali linaloelekezewa agizo hilo ni mtu binafsi anayemiliki mali kwa uhalisia wake, kama walivyoelezea wanazuoni katika mjadala kuhusu athari ya “ushirika” katika mali, waliouita “zaka ya kuchanga” Wanazuoni walitofautiana kuhusu athari ya ushirika huu kwa kauli mbili; Madhehebu ya Imamu Shafi yalizingatia kuwa ushirika katika mtaji unaathiri hukumu ya Zaka, kiasi cha Zaka na kiwango cha utoaji, na kiwango cha lazima cha kutoa, na hiyo ni kutokana na maekelezo kati yao katika aina ya mali ambayo wamechanga.
Wanazuoni wa Imamu Hanafi walisema kuwa ushirika hauathiri kabisa utoaji wa Zaka. Kila mmoja kati ya washirika anahesabiwa binafsi, iwapo yatatimia masharti ya zaka kwake na kuondoka kwa vikwazo vyake.
Wafuasi wa Imamu Maliki, Imamu Shafi katika kauli yake ya zamani, na Madhehebu ya Hanbali (kwa maoni ya kutegemewa) walikubaliana na maoni haya — kwamba ushirika hauna athari katika Zaka ya mali isiyo mifugo[1].
Na maoni ya Wanazuoni ndiyo yanayochaguliwa kwa Fatwa katika suala hili. Na kwa mujibu wa maoni hayo, Zaka katika kampuni ya watu binafsi ni wajibu kwa washirika wenyewe kwa mujibu wa agizo la kisharia kwa nafasi zao binafsi kama wamiliki wa mali, kila mmoja kwa sehemu yake ya umiliki. Hii ni kwa kuwa mshirika huyo anapata sifa ya mfanyabiashara, kama ilivyoelezwa katika kifungu cha 10 cha Sheria ya Biashara Na. 17 ya mwaka 1999[2].
Kama ambavyo, Zaka ni ibada inayohitaji nia ili iwe sahihi, kama walivyosema Wanazuoni wa Imamu Hanafi, Maliki, Shafi na Hanbali.
Vile vile, sharti la ulazima wa Zaka ni kumiliki kiwango kwa umiliki kamili, mali hiyo iwe zaidi ya mahitaji ya msingi, na isiwe na deni. Haiwezekani kuondoa uwezekano wa kuwa miongoni mwa washirika kuna mtu ambaye hana masharti haya, na hivyo kumlazimisha kutoa Zaka ya sehemu yake kunaweza kumletea taabu au dhiki.
Tunafpata faida kutokana na yaliyotangulia;
Zaka katika mashirika/kampuni ya watu binafsi ni wajibu kwa kila mshirika mmoja mmoja (binafsi), baada ya kuhesabu kiasi halisi anachostahiki katika mali ya kampuni, kisha kujumlisha na mali zake binafsi (ikiwa zipo), kwa sharti la kutimia masharti ya Zaka zaka.
Hakuna kizuizi iwapo washirika wote watakubaliana kuipa mamlaka Bodi ya Wakurugenzi ya kampuni kutoa Zaka ya mali ya kampuni kama mtu mmoja. Katika hali hii, kampuni itahesabiwa kama muungano mmoja kwa ajili ya kukadiria kiwango-nisabu ya mtaji wa kazi, kuzingatia madeni, na kukadiria kiasi kinachopaswa kutolewa, kisha mzigo huo wa Zaka ugawanywe kwa kila mshirika kwa mujibu wa sehemu yake. Kwa kutanabahisha, zaka hii ya kampuni haitoshelezi Zaka ya mali ya mtu binafsi ya kila mshirika, iwapo anamiliki mali nyingine nje ya kampuni hiyo. Zaka hiyo ya pamoja inahesabiwa tu kwa ajili ya sehemu ya mshirika katika kampuni hiyo.
[1] “Al-Tajrid” (3/1200, chapa ya Dar Al-Salam), “Al-Mukhtasar Al-Fiqhi” (2/5, Khalaf Ahmed Al-Habtoor Foundation chapa), “Rawdat Al-Talibin” (2/172, chapa ya Al-Maktab Al-Islami), “Al-Mughdini” (Maktaba ya Al-Mughdi) 2/462.
[2] "Bada'i' al-Sana'i'" cha Imam al-Kasani al-Hanafi (2/40, chapa ya Dar al-Kutub al-'Ilmiyya), "al-Ishraf" cha Jaji 'Abd al-Wahhab al-Maliki (1/389, chapa ya Dar Ibn Hazm), "al-Ishraf" na Imam al-Majmu' (6/180, chapa ya Dar al-Fikr), na “al-Mughni” cha Imam Ibn Qudama al-Hanbali (2/476).
Arabic
Englsh
French
Deutsch
Urdu
Pashto
Hausa
