Zaka ya Mimea ya Mapambo

Egypt's Dar Al-Ifta

Zaka ya Mimea ya Mapambo

Question

Mtu anapanda ua la zambarau nalo huuzwa kwa bei ya juu. Je, analazimika kutoa Zaka juu yake? Au anatoa Zaka ya biashara kwa kile anachouza? Na kwa hali yeyote ile, kiwango cha Zaka ataamuaje?

Answer

 Zaka inayowajibika katika mazao na matunda — na hilo linajumuisha ua la zambarau kama ilivyo katika suala letu — ni sehemu ya kumi (¹⁄₁₀) ikiwa linatoka kwenye ardhi inayonyweshewa kwa mvua au kwa njia inayoitwa kwa kimazoea “Al raha” na mfano wake. Na hutolewa nusu ya sehemu ya kumi (¹⁄₂₀) ikiwa linatoka kwenye ardhi inayonyweshewa kwa vifaa kama mashine za kisasa au mvuke na mfano wake, iwe kilichotoka ardhini ni kidogo au kingi. Zaka inawajibika kwa kile chote kilichotoka ardhini wakati wa mavuno bila ya masharti ya kufikia nisabu wala kupita kwa mwaka.

Maelezo

Miongoni mwa mali ambazo sheria imewajibisha Zaka juu yake ni "mazao na matunda". Mwenyezi Mungu anasema: "Enyi mlioamini! Toeni katika vilivyo vizuri mnavyovipata, na katika tulivyokutoleeni kutoka katika ardhi." [Al-Baqarah: 267]

Na anasema tena: "Kuleni katika matunda yake yanapozaa, na toeni haki yake siku ya mavuno yake." [Al-An'am: 141]

Imepokewa kutoka kwa Ibn Umar (RA) kwamba Mtume (S.A.W) alisema: "Kilichonyweshwa kwa mvua au chemchemi au kilichochota maji ardhini chenyewe, Zaka yake ni sehemu ya kumi, na kilichonyweshwa kwa kumwagilia kwa juhudi, zaka yake ni nusu ya sehemu ya kumi." (Ameipokea Al-Bukhari katika Sahih yake, na Abu Dawud, Al-Tirmidhi na Ibn Majah katika Sunan zao)

Na ua la zambarau ni miongoni mwa mimea inayochanua maua, nalo ni “mmea wenye harufu nzuri, una maua mekundu yenye kuelekea kwenye weusi.” Na kwa kuwa muulizaji hulipanda na kisha kuuza ua hilo, basi mtazamo wa kisheria kuhusu uhalali wa Zaka juu yake unarejea kwenye yale yaliyowekwa na wanazuoni kuhusu Zaka ya mazao na matunda, kwa tofauti na tafsiri zao kuhusu yale yanayojumuishwa humo au la — na si Zaka ya bidhaa za biashara. Tofauti kati ya hizi mbili ni kwamba biashara ni kununua ili kuuza kwa faida, Bila kujumuisha kipengele chochote cha kilimo, viwanda, uzalishaji, au unyonyaji.

Imamu Abu Hanifa na waliokubaliana naye miongoni mwa Wanazuoni waliona kuwa Zaka ni wajibu katika kila kitu kinachotoka ardhini ambacho kinalengwa kupandwa, miongoni mwa mazao yanayofaidika nayo binadamu, iwe ni kwa chakula kisichoepukika au ni kwa matunda na maua yanayotumiwa kwa ajili ya starehe na burudani. Hii ni kwa sababu yote hayo yanakusudiwa kukuza ardhi. Hivyo, kwa mujibu wake, kilichoondolewa katika zaka ni yale yasiyolengwa kwa kawaida kwa uzalishaji — kama kuni, majani, mabua ya nafaka, na miti ya pamba na mfano wake. Hii pia ni kauli aliyoiunga mkono Imamu Al-Razi[1].

Na rai hii ndiyo yanayochaguliwa kwa ajili ya Fatwa, kwa kuwa yana nguvu katika hoja zake, yanaendana na ujumla wa dalili, na yanaafikiana na hekima ya kuwekewa zaka, kuzingatia maslahi ya masikini na kumshukuru Mola Mtukufu.

Tunapata faida kutokana na yaliyotangulia;

Zaka inayowajibika katika ua la benafseji ni Zaka ya mazao na matunda, na si Zaka ya biashara.

Kiasi cha zaka kinachotakiwa ni sehemu ya kumi ya uzalishaji wake ikiwa halikumwagiliwa kwa kutumia vifaa, na ni nusu ya sehemu ya kumi ikiwa limenyweshwa kwa kutumia vifaa.

Inajuzu kutoa Zaka hiyo kwa thamani ya pesa kulingana na bei ya soko siku ya mavuno. na si sharti kwa hili kufikia kiwango cha chini.

 

[1] “Al-Asl” (2/162, kilichochapishwa na Idara ya Qur’ani na Sayansi za Kiislamu - Karachi), “Sharh Mukhtasar al-Tahawi” (2/288, kilichochapishwa na Dar al-Bashair al-Islamiyya), “Al-Mabsut” (3/2, kilichochapishwa na Dar al-Ma’rifa), “G316, Mafatib al-4” Ihya’ al-Turath al-Arabi).

Share this:

Related Fatwas