Alifungua Siku kadhaa za Ramadhani na Hakumbuki Idadi Yake
Question
Mzee mmoja anakumbuka kwamba alipooa katika ujana wake, alifungua Ramadhani mwaka wa kwanza wa ndoa yake siku kadhaa na hakumbuki idadi yake. Je, afanye nini sasa?
Answer
Mwenye kufungua siku za Ramadhani katika ujana wake, ni wajibu kwake kulipa (qadhaa) alichokifungua. Na akisahau idadi ya siku alizozifungua, basi afunge (alazimike kulipa) mpaka apate yakini kwamba amemaliza deni lake. Ikiwa atakuwa hawezi kufunga (kulipa), atatoa fidia. Pia, inalazimika kwake kutoa kafara ikiwa kuharibika kwa saumu yake kulisababishwa na kujamii wakati wa mchana wa Ramadhani, na wajibu ni kutoa kafara moja tu, hata kama itakuwa katika siku nyingi tofauti za mwezi.
Maelezo
Ni wajibu kisharia kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kila Muislamu anaye wajibika; kwa kauli ya Mwenyezi Mungu: {... Basi atayekuwa mjini katika mwezi huu naafunge.} (Al-Baqarah: 185).
Kufungua Saumu kwa makusudi mchana wa Ramadhani ni dhambi kubwa, kwa sababu inavunja utakatifu wa mwezi. Imepokewa kutoka kwa Mtume (S.A.W.) kwamba alisema: “Mwenye kufungua siku moja ya Ramadhani bila ya ruhusa wala maradhi, kufunga kwake saumu ya maisha yote hakumlipi (kwa siku hiyo) hata kama atafunga.”
Miongoni mwa mambo yanayobatilisha saumu kwa makubaliano ya wanazuoni ni: Kula, kunywa, na kujamii wakati wa mchana wa Ramadhani.
Ndoa wakati wa Ramadhani inaruhusiwa kwa mujibu wa sharia ya Kiislamu. Hata hivyo, imekuwa ni desturi miongoni mwa watu kuahirisha ndoa hadi Eid, ikiwa ni tahadhari dhidi ya kuharibu saumu kwa kujamiiana wakati wa mchana wa Ramadhani. Ushahidi wa hilo ni Hadithi iliyopokelewa na Mashekhe wawili (Bukhari na Muslim) kutoka kwa Aisha (R.A) ambaye amesema: “Mtume (S.A.W) alikuwa akibusu akiwa amefunga, lakini yeye ndiye aliyekuwa na uwezo mkubwa wa kudhibiti matamanio yake.”
Ushahidi unaonesha kuwa kumkataza mfungaji kumbusu mke wake mchana wa Ramadhani kunatokana na kanuni ya kuzuia njia za maovu.
Mtu anayeanza maisha yake ya ndoa katika mwezi wa Ramadhani anahofia kwamba anaweza kutumbukia katika dhambi na kuvunja utakatifu wa mwezi huo. Kwa hiyo, kujiepusha kufanya hivyo ni vyema, kwani kunaendana na hekima iliyo nyuma ya kuruhusiwa kufunga.
Iwapo mtu atafuturu katika mwezi wa Ramadhani, akiwa hajakusudia kufunga, kisha akajamiiana, ni lazima azitimize siku alizofungua. Halazimiki kutoa kafara kutokana na kutojua hukumu za saumu ikiwemo hukumu ya kujamiiana mchana wa Ramadhani. Hii inapimiwa na mfano wa Muislamu mpya.
Ikiwa mtu huyo alikuwa anafahamu uharamu wa kujamiiana mchana wa Ramadhani, akakusudia kufunga, kisha akajamiiana na mke wake, funga ya wanandoa wote wawili ni batili. Wanapaswa kufidia siku hiyo na kutubu kwa Mwenyezi Mungu. Mume pia ana wajibu—pamoja na kufidia siku hiyo —kutoa kafara, ambayo ni saumu ya miezi miwili mfululizo. Ikiwa hawezi kufanya hivyo, lazima alishe masikini sitini.
Ushahidi wa hilo ni ule uliopokewa na Al-Bukhari katika Sahihi yake kutoka kwa Abu Hurairah, (R.A), ambaye amesema: “Mtu mmoja alikuja kwa Mtume, (S.A.W), akasema: ‘Mimi nimehukumiwa.’ Akasema: ‘Una nini?’ Akasema: ‘Nilimwingilia mke wangu wakati wa Ramadhani. unafunga miezi miwili mfululizo?’ Akasema: ‘Hapana.’ Akasema: ‘Je, unaweza kuwalisha masikini sitini?’ Akasema: ‘Hapana.’ Akasema: ‘Kaa chini.’ Akakaa, na kikapu kikubwa cha tende kikaletwa kwa Mtume (S.A.W). Akasema: Chukua hiki na utoe sadaka. Akasema: Kwa masikini kuliko sisi? Mtume (S.A.W) alicheka. Akasema: Lisha ahali zako kwa hayo.”
Ikiwa mtu atafungua saumu yake bila ya kujamiiana—kwa mfano, ikiwa anakula au anakunywa, akisahau saumu yake, na akafikiri kwamba ameivunja kwa sababu ya kutoijua hukumu hiyo, kisha akajamiiana kwa makusudi na mke wake—lazima aifidie siku hiyo, lakini hakuna kafara inayotakikana kwa mujibu wa makubaliano. Iwapo atatambua kuwa hakufungua saumu yake, kisha akajamiiana wakati wa mchana, ni lazima alipe kwa mujibu wa makubaliano. Wanachuoni wengine pia wanakubali kwamba kafara inahitajika. [1]
Iwapo mtu atafuturu kwa makusudi bila ya kujamiiana, ni lazima ajizuie kwa siku nzima, kutokana na utakatifu wa wakati huo, na aifidie siku hiyo tu—kulingana na Fatwa iliyopendekezwa. Iwapo atakuwa amejamiiana katika siku ambayo alifungua kwa kukusudia, basi ni lazima afidie tu, kwa mujibu wa wanazuoni walio wengi, wakiwemo Madhehebu ya Imamu Hanafi, Maliki, na Shafii, tofauti na Madhehebu ya Hanbali [2].
Hukumu ya kufidia siku aliyofungua ni iwapo alikuwa na uwezo wa kufunga. Ikiwa hawezi kufidia saumu, ni lazima atoe fidia kwa kumlisha masikini kwa kila siku. Fidia inakubaliwa tu kwa mtu ambaye hawezi kabisa kufunga na hawezi tena kutekeleza funga ya faradhi ya Ramadhani, katika hali ambayo kufunga kunaondolewa. Hata hivyo, ikiwa ana uwezo, basi kufunga tu ndio ni halali kutoka kwake.
Wanachuoni wameafikiana kwamba ikiwa mtu atajamiiana na mkewe mara nyingi katika siku moja, basi kafara haizidishiwi kwa vitendo vingi; badala yake, kafara moja tu inahitajika.
Mafakihi walieleza ulazima wa kafara moja ikiwa akijamii mara mbili au zaidi kwa kusema kuwa tendo hili la pili la jimai halikutokea mahali pazuri, kwani funga hiyo ilibatilishwa na jimai ya kwanza.
Wametofautiana kuhusu mtu aliyefungua saumu kwa kujamiiana mara nyingi katika siku tofauti za Ramadhani. Imamu Malik, Shaafi, na kundi la Wanachuoni walishikilia kwamba kafara moja inahitajika kwa kila siku, wakati Wanachuoni wa Madhehebu ya Imamu Hanafi walisema kwamba ni lazima alipe kafara moja isipokuwa atoe kafara kwa kujamiiana kwa mara ya kwanza..
Fatwa inayopendelewa ni kwamba kafara moja inahitajika; kwa sababu ya kuingiliana kafara kila inapowezekana, na kwa sababu kigezo cha usahihi wa kafara ni kuvuka mipaka dhidi ya saumu kwa kuvunja utukufu wa mwezi. Kwa hiyo, kafara hairudiwi tena, kwa sababu utakatifu ni sawa katika kila jambo, na kwa sababu kafara ni adhabu, na adhabu huzuiliwa kwa mambo yenye shaka kwa kulinganisha na adhabu zilizowekwa.
Hata hivyo, muingiliano huu ni wa masharti ya kutojamiiana tena baada ya kutoa kafara ya kwanza. Vinginevyo, kafara moja haitatosha, kwani kizuizi kilichokusudiwa hakitapatikana kwa kurudia.
Iwapo mtu huyo ni wajibu kufidia siku ambazo idadi yake haijulikani, basi afunge mpaka ahakikishe kuwa ametekeleza wajibu wake. Hii ni kwa sababu, baada ya kuwa na yakini ya kuacha, anashughulikiwa na siku zote, na kanuni ya msingi ni kwamba hajazitimiza. Kwa hiyo, ni lazima afidie siku ambazo hana hakika kuhusu kuzitimiza.
Tunapata faida kutokana na yaliyotangulia;
Kufunga mwezi wa Ramadhani ni wajibu kisaeria kwa kila Muislamu aliyelazimishwa.
Miongoni mwa mambo yanayobatilisha funga kwa mujibu wa makubaliano ya Wanachuoni ni kula, kunywa na kujamiiana mchana wa Ramadhani.
Iwapo mwenye kufuturu atasahau idadi ya siku alizofungua katika mwezi wa Ramadhani, ni lazima azifidie mpaka ahakikishe kuwa ametekeleza faradhi yake na kwamba ametimiza siku alizokuwa akidaiwa. Ikiwa hatoweza kufunga, ni lazima atoe fidia.
[1] “Al-Iqna’” cha Ibn al-Qattan, 1/234, na “Al-Majmu’” cha al-Nawawi, 6/338, chapa ya Dar al-Fikr.
[2] "Al-Mughni" (3/144, toleo la Maktaba ya Kairo).
Arabic
Englsh
French
Deutsch
Urdu
Pashto
Hausa
