Ulimwengu katika Uislamu

Egypt's Dar Al-Ifta

Ulimwengu katika Uislamu

Question

Ikiwa sayansi hii ya kisasa imesaidia, na matokeo yake, kuunda picha maalumu ya Ulimwengu huu, vile vile imethibitisha uwezo wa mwanadamu kutumia nguvu zake za asili na maliasili kwa faida yake mwenyewe, basi ni kwa kiwango gani picha hii inafanana na ile inayoweza kutolewa katika chanzo cha kwanza cha Uislamu, ambacho ni Qur'ani Tukufu kuhusu ulimwengu? 

Answer

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na rehma na amani zimwendee bwana wetu Mtume wa Mwenyezi Mungu, jamaa zake, masahaba wake na wanaomfuata, na baada ya hayo:
1) Tukiangalia Qurani Tukufu - kama ilivyotajwa na Marehemu Profesa Dk Abu Al-Wafa Al-Ghunaimi Al-Taftazaniy, mmoja wa wataalamu wakubwa katika Falsafa ya Kiisilamu ya kisasa - kwa uangalifu, tutagundua kuwa inaelekeza akili ya mwanadamu itumie mbinu iliyojumuishwa ya kuutafiti Ulimwengu, na mbinu hii ina hatua mbili: Ya kwanza: Ndani yake, mtu huyo huweka kando maoni yake ya zamani juu ya Ulimwengu, au ukitaka utasema: huweka uigaji ili kutolewa mawazo yake kutoka kwa vizuizi vyake, na kuwa tayari zaidi kwa utafiti wa kimaudhui. Hatua ya pili: kutengeneza mbinu mbili; Mbinu sanifu na ya kufata ili kuunda picha ya Ulimwengu na uhusiano wake nayo na jukumu lake ndani yake.
2) Kuhusu hatua ya kwanza: Qur'ani Tukufu inawaita watu, kwanza kabisa, kupendekeza uigaji, na kukomboa fikira na maoni na mafundisho ya zamani yaliyorithiwa. {Na wanapo ambiwa: Fuateni aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu; wao husema: Bali tutafuata tuliyo wakuta nayo baba zetu. Je, hata ikiwa baba zao walikuwa hawaelewi kitu, wala hawakuongoka} [AL BAQARAH: 170], na Qur'ani Tukukfu inakanushia wale ambao walizuia viungo vya mwili wao na akili zao na wakategemea kuiga kwa njia ya kipofu kwamba wao ni kama ng'ombe, Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {Na tumeiumbia Jahannamu majini wengi na watu. Wana nyoyo, lakini hawafahamu kwazo. Na wana macho, lakini hawaoni kwayo. Na wana masikio, lakini hawasikii kwayo. Hao ni kama nyama howa, bali wao ni wapotofu zaidi. Hao ndio walio ghafilika} [AL A'ARAF: 179].
3) Na Qur'ani Tukufu ilifanya sayansi peke yake, sio uigaji, ni mbinu pekee inayoongoza kwa kile mtu anachoamini na kutembea kulingana nacho, kama inavyoashiria kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Wala usiyafuate usiyo na ujuzi nayo. Hakika masikio, na macho, na moyo - hivyo vyote vitasailiwa} [AL ISRAA:36] Na Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema pia: {Sema: Je, nyinyi mnayo ilimu mtutolee? Nyinyi hamfuati ila dhana. Wala hamsemi ila uwongo tu} [AL ANA'AM: 148].
4) Qur'ani Tukufu inaelekea hoja ya kiakili na kuzingatia Ulimwengu ili kuthibitisha mafundisho yake, na kwa kujibu wavunja imani na kukanusha madai yao, miongoni mwa hayo ni Aya hizi: {Na kadhaalika tulimwonyesha Ibrahim ufalme wa mbingu na ardhi, na ili awe miongoni mwa wenye yakini. (75) Na ulipo muingilia usiku akiona nyota, akasema: Huyu ni Mola Mlezi wangu. Ilipo tua akasema: Siwapendi wanao tua. (76) Alipo uona mwezi unachomoza alisema: Huyu ndiye Mola Mlezi wangu. Ulipotua akasema: Kama Mola Mlezi wangu hakuniongoa, nitakuwa katika kaumu walio potea. (77) Na alipo liona jua linachomoza akasema: Huyu ndiye Mola Mlezi wangu. Huyu mkubwa kuliko wote. Lilipo tua, alisema: Enyi watu wangu! Mimi simo katika hayo mnayo fanyia ushirikina. (78) Hakika mimi nimeuelekeza uso wangu sawa sawa kwa aliye ziumba mbingu na ardhi, wala mimi si miongoni mwa washirikina. (79)} [AL ANA'AM 75: 79], Qur'ani Tukufu inataka akili ya mtu kufikiria na kuudhani utaratibu wa Ulimwengu na umoja wa Muumba wake.
5) Kuhusu hatua ya pili: kubuni mbinu sanifu na ya kufata, ingawa Qu’rani Tukufu sio kitabu katika mantiki, lakini ina kanuni za jumla za ushahidi wa busara, na kwa maelezo yake, sio kazi ya Qu’rani Tukufu kufunuliwa kwake, na msomaji wa Qur'ani Tukufu hugundua kuwa mazungumzo ndani yake yanaelekezwa haswa kwa Akili timamu kwa maoni wazi na rahisi, na kwa mioyo safi kwa ufasaha na ufupi zaidi. Na kuhusu jambo hilo hakuna chochote kinachozidi juu ya Qur`ani Tukufu miongoni mwa yaliyoandikwa na wanafalsafa na wanafikra kufuatana na tofauti ya mazingira yao na nyakati zao, kwa dalili inavyothibitishwa na athari kubwa ya kiakili ambayo imekuwa nayo kwa maisha ya wanadamu tangu kuteremshwa kwa ufunuo (wahyi) hadi leo. Wataalamu wakuu wa falsafa na busara kati ya Waislamu walielewa hilo, na wakataja kwamba ilikuwa na aina anuwai za hoja na uthibitisho, ili kwamba hakuna chochote kinachoweza kuongezwa kwa jambo hili, kwa sababu hakuna taarifa baada ya kauli ya Mwenyezi Mungu kama Imam Al-Ghazali anavyosema katika kitabu chake cha Al-Ihya (1/93), na kama anavyosema Imamu Al-Fakhr Al-Raziy katika kitabu chake Al-Arubaini: "Wote walikiri kwamba haiwezi kuongezwa katika uamuzi wa ushahidi wa busara kwa kile kilichoelezwa katika Qu’rani Tukufu".
6) Kwa kweli, tukitazama Qur'ani kwa uangalifu, tutagundua kuwa inatahadharisha akili juu ya utumiaji wa aina tofauti za mawazo ya kiakili, iwe ya moja kwa moja au siyo ya moja kwa moja. Pia inawaita watu kufahamu matokeo ya utangulizi ambao umethibitishwa kuwa sahihi katika kutoa dalili ya imani, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Kwani mwanaadamu haoni ya kwamba Sisi tumemuumba yeye kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndio amekuwa ndiye mgomvi wa dhaahiri! (77) Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: Ni nani huyo atakaye ihuisha mifupa nayo imekwisha mung'unyika? (78) Sema: Ataihuisha huyo huyo aliye iumba hapo mara ya mwanzo. Na Yeye ni Mjuzi wa kila kuumba (79) Aliye kujaalieni kupata moto kutokana na mti wa kijani nanyi mkawa kwa huo mnawasha. (80) Kwani aliye ziumba mbingu na ardhi hawezi kuwaumba mfano wao? Kwani! Naye ndiye Muumba Mkuu, Mjuzi. (81)} [YASIN 77:81]. Qur'ani Tukufu inatualika tutumie uchunguzi na ufafanuzi wa sehemu kutoka kwa ulimwengu wa asili kutuletea ufahamu wa sheria za jumla zinazoendesha ulimwengu huu kulingana na hali yake.
7) Wanazuoni wa Kiislamu walitoa dalili ya kuruhusiwa Kipimo cha akili na cha Kifiqhi kwa kauli yake Mwenyezi Mungu: {Basi Mtukufu zingatieni enyi wenye macho!} [AL HASHR: 2]. Aya hiyo adhimu inatuelekeza kutumia kipimo kwa aina zake zote mbili. Kwa sababu kuzingatia, kama Al-Jarjani anavyosema katika ufafanuzi wake: "Ni kuzingatia uamuzi wa kudumu kwa maana yoyote iliyothibitishwa, Na kuambatanishwa mfano wake nayo", na huu ni mfano sawa wa kupima. Miongoni mwa Aya zinazotoa dalili ya utumiaji wa kufuata kitu mpaka kufikia matokeo maalum na utumiaji wa mtazamo wa kisayansi juu ya vitu na jinsi vilivyotunga, Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: {Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa? (17) Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa? (18) Na milima jinsi ilivyo thibitishwa? (19) Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa? (20)} [AL GHAASIYAH 17:20]. Uangalie neno la jinsi” katika Aya hizi ili kuona kwamba inaelezea roho nzima ya sayansi ya kisasa na mbinu yake, kwa sababu sayansi - kwa dhana ya wataalamu wa mbinu za utafiti wa kisasa - ni jibu la swali ((jinsi)), na sio jibu la swali la ((kwanini)), kwa hivyo sayansi ya kisasa inajali kuelezea jinsi hali hiyo ilivyoundwa, na haijali kuitafutia kusudi lake.
8) Qu’rani Tukufu, inapotuita tuchunguze jinsi wanyama, sayari na dunia vilivyoumbwa, hutupatia njia sahihi ya utafiti wa kufata katika sayansi anuwai, kama sayansi ya maisha, falaki, jiolojia, jiografia, n.k., bila ya Qu’rani Tukufu yenyewe kuwa kitabu kinachojadili mada za sayansi hizi.
9) Miongoni mwa aya ambazo ni muhimu sana katika suala hili pia ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Hakika katika kuumbwa kwa mbingu na ardhi, na kukhitalifiana usiku na mchana, na marikebu ambazo hupita baharini kwa viwafaavyo watu, na maji anayo yateremsha Mwenyezi Mungu kutoka mbinguni, na kwa hayo akaihuisha ardhi baada ya kufa kwake, na akaeneza humo kila aina ya wanyama; na katika mabadiliko ya pepo, na mawingu yanayo amrishwa kupita baina ya mbingu na ardhi, bila shaka zimo Ishara kwa watu wanao zingatia.} [AL-BAQARAH 164]. Aya karimu hizi zinatuelekeza kuwa wanadamu wanaozingatia - yaani, hutumia akili zao vizuri - ndio wanaoangalia uumbaji wa mbingu na ardhi, na katika hali ya ulimwengu kwa tofauti zao zote, na wao ndio ni wale ambao wanaunganisha kwa maoni yao kati ya sababu na vinavyosababisha, kwa hivyo wanajua jinsi mbingu na ardhi viliumbwa, na jinsi usiku unavyofuatiliwa na mchana, jinsi meli husafiri baharini, mvua hunyesha vipi, na wanyama wanaishi vipi kwa nchi kavu.
10) Qur'ani Tukufu inatuonya kwamba mfumo wa ulimwengu ni thabiti na una sheria ambazo hazibadiliki. Hizi ndizo tunazofikia kwa kuzingatia kwa kisayansi kulingana na uchunguzi wa hisia. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: {Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia zao} [YASIN 40].
11) Vivyo hivyo, mkutano wa kibinadamu una sheria ambazo zina uthabiti ule ule, na kwa rejeleo hilo na mfano wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu alivyosema: {Hakika Mwenyezi Mungu habadili yaliyoko kwa watu mpaka wabadili wao yaliyomo nafsini mwao. Na Mwenyezi Mungu anapo watakia watu adhabu hakuna cha kuzuia wala hawana mlinzi yeyote badala yake.} [AR RAAD: 11]. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema pia: {Ndilo umbile la Mwenyezi Mungu alilo waumbia watu Hapana mabadiliko katika uumbaji wa Mwenyezi Mungu Hiyo ndiyo Dini iliyo nyooka sawa lakini watu wengi hawajui} [AR RUUM: 30].
12) Mtu huyo hawezi kufikia kutoka kwa kutafakari juu ya ulimwengu hadi ufahamu wa mfumo na sheria zake isipokuwa kwanza ajiamini mwenyewe na anaamini kuwa ulimwengu unaonekana uko chini ya mtazamo na utafiti wake, na kwamba matukio ya ulimwengu sio jambo lisiloeleweka na la kushangaza ambalo haliwezi kuelezewa, na kwamba anaweza kufaidika na ulimwengu na kutumia mali zake kwa kiwango kikubwa zaidi kupata usalama wa maisha yake, Qur'ani Tukufu ilisema kwa uwazi wakati ilipothibitisha kuwa ulimwengu umedhalilishwa kwa mwanadamu Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: {Na amefanya vikutumikieni vilivyomo mbinguni na vilivyomo katika ardhi, vyote vimetoka kwake. Hakika katika hayo zimo Ishara kwa watu wanao fikiri.} [AJ JATHIYAH: 13].
13) Uthibitisho wa Qur'ani kwamba Ulimwengu wote umedhalilishwa kwa wanadamu wakati huo huo ni uthibitisho wa roho ya njia sahihi ya kisayansi ambayo kila wakati inajaribu kuchunguza kile kisichojulikana juu ya ulimwengu huu na matukio yake kwa msingi wa kujiamini nguvu ya mwanadamu.
14) Hapa kuna maoni ambayo yana umuhimu mkubwa, nayo ni kwamba wakati motisha ya kufaidika kutoka kwa Ulimwengu kupitia njia ya sayansi ni imani ya kidini ya mwanadamu, hamu yake ya kukaribia Mwenyezi Mungu, na kushinda thawabu zake katika maisha mengine, basi kuna motisha kubwa sana, na kutoka kwa aya za Qur'ani zenye umuhimu mkubwa katika suala hili, ni Aya hii: {Je, hawatazami ufalme wa mbingu na ardhi, na vitu alivyo viumba Mwenyezi Mungu, na pengine ajali yao imekwisha karibia? Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?} [AL A'ARAF: 185], aya hiyo ilizingatia kuwa kufahamu kwa viumbe kwa anuwai yake ni miongoni mwa kazi muhimu zaidi za wema, ambayo lazima Muislamu afanye hesabu yake kwa usawa wa matendo yake katika maisha mengine, kwa hivyo lazima ajitahidi kadiri ya uwezo wake katika usawa wa matendo yake katika maisha mengine, na ndio kwa sababu hiyo baadhi ya wanazuoni wa imani katika Uislamu walifika hadi kusema kwamba mantiki ya busara ni moja ya kanuni zilizowekwa katika Uislamu, kwa hivyo mbali na Mu'tazila ambao walilazimisha kumjua Mwenyezi Mungu kwa akili, tunaona Wasunni kati ya Waash'ari pia walilazimisha kila mkalifishwa kutoa dalili ya uwepo wa Mwenyezi Mungu akilini mwake.
15) Tunaweza kusema kutoka kwa yote yaliyotajwa hapo juu kuwa Qu’rani Tukufu ilimhimiza mwanadamu atengeneze njia ya maarifa ambayo imetiwa muhtasari katika kutazama ulimwengu kwa kupima na kuzingatia au zote mbili, ili kupata ufahamu wa sheria zake za jumla. Kisha kuendelea kwa kutembea baada ya hapo hadi kumjua Mwenyezi Mungu. Kwa kweli, wakati Qur'ani Tukufu inapozungumzia matukio ya ulimwengu, inaashira matukio hayo ili kuamsha akili kutoka kwenye usingizi wake, ili mambo haya yaweze kueleweka na kufasiriwa na tafsiri sahihi ya kisayansi.
16) Akili ya mwanadamu huibua kwa maumbile yake maswali mengi juu ya ulimwengu: Je! ulimwengu ni mpya au ni ya zamani? Na ikiwa ulikuwa mpya, ungekuwaje? Je! unaisha kumaliza kwanza? Ulimwengu mwingine upo au la? Je! Ni nini sababu ya utaratibu na vifungu katika ulimwengu huu? Je, una lengo gani?
17) Qur`ani Tukufu imeanzisha ukweli mwingi kuhusiana na ulimwengu, ambyo ni muhimu zaidi ni kwamba ulimwengu ni mpya na umeumbwa, na viumbe vyote vilivyomo ndani ya umimwengu vina mwanzo na mwisho, na hakuna uhai milele isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu tu: {Yeye ndiye Muumba wa mbingu na ardhi} [AL BAQARAH: 117], Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema pia {Yeye ndiye wa Mwanzo na ndiye wa Mwisho, naye ndiye wa Dhaahiri na wa Siri, naye ndiye Mjuzi wa kila kitu} [AL HADID : 3].
18) Msomaji wa Qu’rani Tukufu anaona kwamba inasema kwa uwazi uwili kati ya Mwenyezi Mungu na ulimwengu, na moja ya ukweli juu ya ulimwengu ni kwamba hauonyeshwi katika maoni yetu, kama vile Qu’rani Takatifu inavyoonyesha kwamba kuna walimwengu wengine na viumbe ambao hatujui chochote juu yake {Na ataumba msivyo vijua} [AN NAHL: 8].
19) Ukweli ni kwamba kutazama Ulimwengu au upeo ambao ni mbali sana au kwa wanadamu na viumbe vidogo sana, hutupeleka kwenye mafunuo mengi ya Muumba ambayo yatafunuliwa kwa mwanadamu kila wakati na milele. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {Tutawaonyesha Ishara zetu katika upeo wa mbali na katika nafsi zao wenyewe mpaka iwabainikie kwamba haya ni kweli. Je! Haikutoshi kwamba Mola wako Mlezi kuwa Yeye ni Shahidi wa kila kitu?}[FUSSILAT: 53].
20) Na ikiwa bado hatujajua juu ya Ulimwengu unaoonekana au juu ya sisi wenyewe, basi tunawezaje kudai kudai kumtambua yeye ni nani Muumba, na nini maana ya ndani kabisa kwa kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu akisema: {Macho hayamfikilii bali Yeye anayafikilia macho. Naye ni Mjuzi, Mwenye khabari.} [AL ANA'AM: 103]
21) Ikiwa Ulimwengu, kulingana na kile kilichotajwa katika Qu’rani Tukufu, ni mpya, na ina Muumba ambaye ni Mwenyezi Mungu, basi ni kawaida kwamba msemo kwamba Ulimwengu uliumbwa kwa makubaliano au kwa bahati haupatani. na Qur'ani Tukufu, lakini badala yake inapingana na sayansi hiyo hiyo, John Buhler anasema: [Rejea: Allah yatajalla fi Asiri Al-Elmi, uk. 102-103]: "Mtu anapotumia sheria za bahati ili kuona kiwango cha uwezekano wa kutokea kwa tukio la matukio ya asili kama vile kuunda sehemu moja ya molekuli za protini kutoka kwa vitu vinavyoingia katika muundo wake, basi tunapata umri wa Dunia, ambayo inakadiriwa kuwa karibu miaka bilioni tatu au zaidi hauzingatiwi muda wa kutosha wa kutokea kwa jambo hili, na uundaji wa sehemu hii kwa bahati kwamba hii inaweza kutokea tu ikiwa kuna nguvu iliyoelekezwa inayolenga lengo dogo na inatusaidia kutambua jinsi mfumo huo unatoka kwenye machafuko".
22) Na kutokana na kile Qur'ani Tukufu inatuonyesha baada ya hii ni kwamba Ulimwengu mwingi ambao Ulimwengu unajumuisha haukuumbwa katika wakati mmoja, miongoni mwao ni wa zamani, na mwingine ni wa baadaye, Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {Na Yeye ndiye aliye ziumba mbingu na ardhi katika siku sita. Na Kiti chake cha Enzi kilikuwa juu ya maji} [HUD: 7], na hii inamaanisha kwamba Ulimwengu haukuwa jinsi ulivyo sasa, na haukuumbwa kabisa mara moja, badala yake kulikuwa na mpangilio wa wakati katika uumbaji wa viumbe, na hata mageuzi katika mchakato wa uumbaji wenyewe, na hii ni sawa kabisa na sayansi ya kisasa ambayo huamua miili ya mfumo wa jua na dunia kwa miaka kwa kuhesabu mionzi na kuainisha nyakati zao ambazo miili hii ya mfumo wa jua ilipoanzishwa kwa utaratibu wa kuhitimu, na kinachothibitisha upangaji huu ni kauli yake Mwenyezi Mungu: {Sifa njema zote ni za Mwenyeezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote} [AL FATIHA: 2]. Elimu ni kuwasilisha kitu kwa ukamilifu wake na kwa utaratibu, Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {Huzidisha katika kuumba apendavyo} [FATER: 1].
23) Ama juu ya data ambayo miili ya mbinguni ilitengenezwa kutoka kwake, inaelezewa katika Qu’rani kama moshi, Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: {Kisha akazielekea mbingu, na zilikuwa moshi, akaziambia hizo na ardhi: Njooni, kwa khiari au kwa nguvu! Vyote viwili vikasema: Tumekuja nasi ni wat'iifu.} [FUSSILAT: 11]. Ama data ya viumbe hai ambavyo viliibuka na kubadilika, ni kutoka kwa maji, kulingana na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na tukajaalia kwa maji kila kilicho hai? Basi je, hawaamini?} [AL ANBIYAA ': 30].
24) Kinachogusa akili ya mwanadamu ni ukweli kwamba Qur'ani Tukufu inaonyesha kwamba asili ya viumbe vyote ni moja, nayo inajumuisha wenzi wawili. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: {Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie} [ADH DHARIAAT: 36], na tunaweza kuelewa aya hizi kulingana na ile iliyogunduliwa kwa sayansi ya kisasa kwamba muundo wa atomiki iko katika viumbe tofauti, na kwamba atomi moja ina elektroni na protoni.
25) Ulimwengu, basi, hauna ukweli wowote isipokuwa kwa kile ambacho Mwenyezi Mungu amethibitisha kwake kutoka uwepo wa kukusanya vitu vyake kwa njia ambayo sayansi ya kisasa imetuonyesha, navyo ni vitu vinavyoanza na protoni ambavyo vina uwepo maalum na nguvu ya kuvutia hiyo inavifanya vijiunge pamoja, na uwepo wa ulimwengu huu unaonekana kuwa thabiti na katika mtazamo wetu, basi kwa kweli, sio chochote isipokuwa ni atomi zilizofungwa katika taa ambazo ni chanya na hasi, ambazo kwa hiyo zinarudi kwa miale. Ndio fizikia ya kisasa imebainisha kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu anaposema: {Na unaiona milima unaidhunia imetulia; nayo inakwenda kama mwendo wa mawingu. Huo ndio ufundi wa Mwenyezi Mungu aliye tengeneza vilivyo kila kitu. Hakika Yeye anazo khabari za yote myatendayo} [AN NAML: 88], na kwa hivyo Bertrand Russell anasema: "Hakuna ushahidi katika taaluma ya fizikia kwamba sifa za kiasili za Ulimwengu wa kawaida zinatofautiana na sifa za Ulimwengu wa kidhahania". Hakuna ukweli isipokuwa uwepo Muumba wa ulimwengu, na viumbe wengine wote ni kama udanganyifu wa kawaida kama wanavyosema wasufi.
26) Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ndiye anayeshikilia Ulimwengu na kuhifadhi uwepo wake juu yake, na kama sivyo, ingekuwa umetoweka {Hakika Mwenyezi Mungu ndiye anaye zuilia mbingu na ardhi zisiondoke. Na zikiondoka hapana yeyote wa kuzizuia isipo kuwa Yeye. Hakika Yeye ni Mpole Mwenye kusamehe} [FATER: 41], Ibn Hazm katika kitabu chake [Al-Fasl anasema: (5/55)]: "Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ndiye Muumba wa kila kiumbe wakati wote. Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: {Kisha tukamfanya kiumbe mwengine.} [AL MUMINUUN: 14]. Na Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema pia: {umbo baada ya umbo} [AZ ZARIAT: 6] Ni sahihi kwamba Mwenyezi Mungu anarejelea hali za viumbe vyake, kwa kuwa ni kiumbe kipya, na Mwenyezi Mungu anaumba katika wakati wote ulimwengu wote upya bila kuangamiza." Al-Kindi anasema [Al-Rasa'il, uk. 162]: "Mwenyezi Mungu ndiye Muumba ambaye anashikilia kila kitu alichokiumba, basi hakuna chochote ila kinashikiliwa kwake na nguvu zake au kikaangamia." Na Ibn Ataa Allah Al-Sakandari anasema katika uamuzi wake: "Neema mbili ambazo hazipatikani kutoka kwao, na kila sehemu yao lazima iwe: Neema ya kuishi na neema ya ugavi". Ikumbukwe kwamba kile waliotajwa hapo juu na Wanazuoni wa Uislamu walisema katika suala hili ni sawa na vile wanavyosema wanafalsafa wa kisasa huko Uropa juu ya uumbaji endelevu.
27) Na Mwenyezi Mungu aliumba kila kitu katika ulimwengu huu kwa kipimo, yaani, kwa kukadiria kiasi na muda kulingana na ilivyotangulia, na ikiwa ungependa umesema: Akafanua na akapa maelezo yake na ameupa cheo fulani cha kuwepo, Mwenyezi Mungu Mtukufu akasema: {Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.} [AL QAMAR: 49] Na Mwenyezi Mungu amesema pia: {na akaumba kila kitu na akakikadiria kwa kipimo.} [AL FURQAAN: 2], na aya ambazo zinataja makadirio ya idadi ya viumbe chini ya kipimo au hesabu ni aya nyingi katika Qu’rani Tukufu.
28) Kuhusu kiini cha kila kitu kilichopo au asili yake, Qur'ani Tukufu ilikionyesha katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Akasema: Mola wetu Mlezi ni yule aliye kipa kila kitu umbo lake, kisha akakiongoa} [TWAHA: 50]. Kwa hivyo, kulingana na Uislamu, inaweza kusemwa kuwa Mwenyezi Mungu aliumba kila kiumbe kulingana na kiini kabla ya uumbaji wake, na hii ni kinyume na vile wanavyosemwa na wanafalsafa katika enzi ya sasa kusema kuwa uwepo unatangulia kiini..
29) Na Qur'ani Tukufu inaonya, baada ya yote haya, kwamba Ulimwengu wote umetawaliwa na mpangilio mkali bila tofauti au upungufu. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: {Aliye umba mbingu saba kwa matabaka. Huoni tafauti yoyote katika uumbaji wa Mwingi wa Rehema. Hebu rudisha nadhari! Unaona kosa lolote?} [AL MULK: 3] Na hekima inahitaji kwamba viumbe katika ulimwengu vinaishi kulingana na sheria ambazo hazibadiliki.
30) Kwa muhtasari, kutoka hapo juu, sifa za picha ya Ulimwengu katika Uislamu zinaainishwa kama ifuatavyo: Ulimwengu wote ni kiumbe kipya, na viumbe vyote vilivyomo vina mwanzo na mwisho, na Mwenyezi Mungu ni yule aliyeuumba na ulimwengu na viumbe vyake vingi tunajua kila mmoja na hatujui chochote juu ya wengine. Na kwamba ukuu wa Ulimwengu hauishii kwenye maoni yetu tu, na kwa hivyo hatuwezi kusisitiza kuwa ulimwengu una mwisho au hauna mwisho. Mwenyezi Mungu hakuumba Ulimwengu wa Ulimwengu mara moja, lakini badala yake aliuumba kwa njia ya polepole au maendeleo, na kwamba misingi yote katika Ulimwengu ni ya asili moja, na Mwenyezi Mungu ndiye anayeushikilia ulimwengu huu na kuhifadhi uwepo wake, vinginevyo ingekuwa umetoweka, na kwamba uumbaji wake wa viumbe unaendelea, na wakati Mwenyezi Mungu alipoumba viumbe vyake, aliwaumba kwa kipimo, yaani, kwa kadirio la kadiri na la muda kulingana na sifa zilizopita, na Ulimwengu wote unatawaliwa na usahihi na mfumo thabiti, kwani vitu vyote ndani yake viko chini ya sheria thabiti na zisizobadilika ambazo hazibadiliki, na hiyo ni maana ya kuipata na ukweli, ambayo ni, kulingana na hekima fulani.
Na Mwenyezi Mungu Mtukfu ni Mjuzi Zaidi.
Chanzo: Profesa Dkt. Abu Al-Wafa Al-Ghunaimi Al-Taftazani, Al-Insan Wal Kawn Fil Islaam, Kairo: Dar Al-Thaqafa Lilnashr wattawzii, 1995 BK, (uk. 25-64) kwa kifupi.

 

 

Share this:

Related Fatwas