Ahmadiyya kwenye Mizani ya Sharia...

Egypt's Dar Al-Ifta

Ahmadiyya kwenye Mizani ya Sharia

Question

 Tumesikia mara nyingi kuhusu kundi la Ahmadiyya pamoja na kuwa nguvu yao ni ndogo lakini hata hivyo ni kundi lenye athari kubwa hasa baada ya matumizi ya njia za kisasa, wamekuwa na kituo cha runinga, tovuti za kiitroniki wakilingania kupitia kituo chao kuwa Mirza Ghulam Ahmad ndiye Al-Mahdy anayesubiriwa na Masihi aliyeahidiwa, wakitoa masomo hewani kwa khalifa wao wa tano kwa mitazamo yao, na wamekuwa ndani ya tovuti yao maelezo ya ajabu juu ya Hadithi inayosema “Hakuna Mtume baada yangu …”, basi upi msimamo wa Uislamu kwa kundi hili na ipi tofauti kati yao na kundi la Kadiyani?

Answer

 Shukrani zote ni za Mwenyezi Mungu peke yake, rehema na amani zimwendee Mtume wa mwisho naye ni Mtume Muhammad S.A.W pamoja na watu wa nyumbani kwake na Masahaba zake na mwenye kumfuata kwa wema mpaka Siku ya Malipo.
Ahmadiyya ni lile lile kundi la Kadiyani, nalo ni kundi lililo nje ya Uislamu na kundi hili linashikamana na imani batili ikiwa ni pamoja na unabii wa huyu mtu ambaye anaitwa Ghulam Ahmad Al-Kadiyani na kuwa yeye ndiyo Mahdi anayesubiriwa, na kuwa ametumwa kwa kupewa ujumbe baada ya Mtume Muhammad S.A.W. na anateremshiwa Ufunuo kama vile Qur`ani na Injili na Taurati, na kuwa roho ya Masihi imechukua nafasi kwake, na kuwa ibada ya Hija ni lazima kwa Waislamu kwenda Kadiyani ambao ni mji mtakatifu kama Makka na Madina, na kuwa ndio mji ulioitwa ndani ya Qur`ani kuwa ni Msikiti wa Al-Aqsa, na Ghulam Ahmad Al-Kadiyani alikuwa ameanza ulinganiaji wake 1888 ambapo ameamzisha shule ya Kadiyani ili kutoa mafunzo kwa watu wake, akaanzisha jarida la kueneza madhehebu yake linaloitwa “Al-Adyan” na kupangilia ulinganiaji wake hatua mbalimbali, na mwisho wake ilikuwa ni kudai kwake utume na yeye ndiyo Masihi anayesubiriwa.
Ghulam Ahmad anasema mwisho wa kitabu chake "Ushahidi wa Qur`ani": Hakika imani yangu ambayo nairudia mara kwa mara ni kuwa Uislamu una sehemu mbili: Sehemu ya kwanza ni kumtii Mwenyezi Mungu, na sehemu ya pili kuitii serikali ambayo imeeneza usalama na ulinzi dhidi ya madhalimu, mfano wa imani hizi batili wafuasi wake hukufuru.
Jambo la pili: Ama kuhusu gazeti la sauti ya Al-Azhar na kutangaza maneno ya Mustafa Thabiti, mimi sifahamu jambo hili ni kweli au si kweli, kwani sijasoma chochote kuhusu Mustafa Thabiti katika gazeti la sauti ya Al-Azhar.
Kwa kuchukulia usahihi wa maneno haya yaliyoandikwa katika gazeti la sauti ya Al-Azhar, hii haina maana ya kutokufuru kwake ikiwa anafuata dini kama hii ya Kadiyani, na Mtume S.A.W. anasema: “Hekima ni shabaha ya Muumini akiwa ataipata basi ni katika watu wenye haki nayo zaidi” kwa maana ikiwa itapatikana kwa ulimi wa kafiri au asiyekuwa kafiri basi sisi tunafaidika kutokana na mfumo mzima wa kibinadamu, lakini tunabainisha tukiamini kutangaza gazeti la sauti ya Al-Azhar maana hii, na hivi ni viunganisho kuhusu mtazamo wa Uislamu katika ukadiani ili kuwafikishia hawa watu, na usia wangu ni kujitenga nao ili wasikufitinishe na dini yako na jitahidi kusoma hukumu za dini yako.

 

 

 

 

Share this:

Related Fatwas