Ahadi ya utii kwa kiongozi wa shiri...

Egypt's Dar Al-Ifta

Ahadi ya utii kwa kiongozi wa shirika la kigaidi la Daishi

Question

Je, ahadi ya utii kwa kiongozi wa Daishi ni halali na kinafunga kisheria?

Answer

Ahadi ya utii kwa kiongozi wa Daishi ni haramu na hailazimiki, na si sahihi kuiita utii hata kidogo. Kwa sababu ahadi ya utii katika maana yake ya Kiislamu lazima iwe na masharti ya kutimizwa kwa Imamu, na miongoni mwa yaliyo muhimu zaidi: uadilifu pamoja na masharti yake kwa jumla (yaani awe na uadilifu katika maisha yake). Hapa hali hii haijulikani kabisa, kwa hivyo wasifu wa kiongozi wa Daishi haujulikani, badala yake haijulikani jina lake halisi ni nani, kwa hivyo anawezaje kuwa Imamu wa Waislamu? Pia, moja ya makusudio ya ahadi ya utii kwa mtawala ni kuwa na ujuzi wa sayansi na elimu ambayo humsaidia kutekeleza jukumu hili kubwa na kufikia maslahi ya watu, na kwamba jambo hilo lijulikane kwa wote, na mtu ambaye hajulikani namana gani watu wanajua hali yake, ujuzi na uwezo wake, na hii inathibitisha kwamba ahadi hii ni batili katika Sharia.

Share this:

Related Fatwas