Ukiukaji wa uelewa wa ukweli kwa uf...

Egypt's Dar Al-Ifta

Ukiukaji wa uelewa wa ukweli kwa ufahamu sahihi ni moja ya matatizo makubwa ambayo yalitesa ulimwengu wetu wa kisasa

Question

Je! Kwa nini ukiukaji wa uelewa wa ukweli ndio ni ufahamu sahihi ni moja ya matatizo makubwa ambayo yalitesa ulimwengu wetu wa kisasa wa Waislamu?

Answer

Wanazuoni walisema kwamba Fatwa hubadilika na mabadiliko ya wakati, mahali, hali na watu, na neno la ukweli huleta pamoja hali hizi nne, na neno la ukweli linajumuisha kila kitu ambacho ni kweli tofauti na sura za kiakili, na kuna mifano mingi katika  Sunnah Juu ya kuathirika kwa Fatwa ya kisheria na ukweli. Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurairah kwamba mtu alimuuliza Mtume (S.A.W) kuhusu kuchanganyika na mke kwa mtu anayefunga. Basi Mtume (S.A.W) aliruhusu, na mwingine akamjia, akamwuliza, Mtume (S.A.W) akamkataza. Hivyo, aliyeruhusiwa ni mzee, na aliyekatazwa ni kijana [Imepokelewa kutoka kwa Abu Daud] Hii ni kwa sababu mzee ana uwezo wa kudhibiti tamaa yake kinyume na kijana huyo, na imekusudiwa kwa kuchanganyika na mke ni kugusana. Mabadiliko haya katika Fatwa ya Mtume (S.A.W) yanarudia mabadiliko ya ukweli, na ukosefu wa ufahamu wa Mufti kwa ukweli kwa ufahamu sahihi ambao lazima hufanya kuwa na makosa katika Fatwa yake. Moja ya sifa za mawazo ya msimamo mkali kwa anayetoa Fatwa ni kwamba hafahamu ukweli vizuri lakini badala yake anaukataa; Kwa sababu – kufuatana na madai yake - ukweli ni kinyume na sheria! Basi anatafuta kubadilisha ukweli kwa hukumu za kisheria, na hii ni kinyume na mfumo wa Mtume, kwani hukumu ya  kisheria ilibadilishwa kwa mujibu wa mabadiliko ya ukweli, sio kinyume na hivyo.

Share this:

Related Fatwas