Athari za uvumi kwenye jamii mbalim...

Egypt's Dar Al-Ifta

Athari za uvumi kwenye jamii mbalimbali

Question

Ni nini wajibu wa Muislamu kuhusiana na uvumi unaoenezwa pale alipo?

Answer

Kusambaza habari za uwongo, au zenye madhara kupitia mitandao ya kijamii na njia nyinginezo ni haramu kwa mujibu wa sharia za Kiislamu.

Mwenyezi Mungu Mtukufu amewawajibisha Waislamu kuhakiki habari kabla ya kuzitolea hukumu, na akaamrisha mambo yarejeshwe kwa wenye elimu kabla ya kuyatangaza na kuyazungumzia. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema: {Enyi mlio amini! Akikujieni mpotovu na khabari yoyote, ichunguzeni, msije mkawasibu watu kwa kuto jua, na mkawa tena wenye kujuta kwa mliyo yatenda.} [Al-Hujurat: 6]

Mwenyezi Mungu Mtukufu amekataza kusikia na kueneza uvumi, na Yeye, Utukufu ni Wake, Aliwalaani wale wanaosikiliza wale wanaotetemeka na kueneza uvumi na vishawishi. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Lau wangeli toka nanyi wasingeli kuzidishieni ila mchafuko, na wange tanga tanga kati yenu kukutilieni fitna. Na miongoni mwenu wapo wanao wasikiliza. Na Mwenyezi Mungu anawajua madhaalimu.} [Al-Tawbah: 47].

Hii ni kwa sababu jambo hili lina athari mbaya sana kwa dini za watu, heshima, mali, na hata maisha yao pia.

Wanaoshiriki dhambi na makatazo ni wale wanaozua uvumi, wanaoeneza, na wanaotaka kuamini bila ya uthibitisho.

Share this:

Related Fatwas