Hukumu uchafu wa uke kwa wanawake
Question
Je, uchafu wa uke – unyevu unaotoka kwenye sehemu za siri za mwanamke mbali na hedhi na damu ya nifasi – ni safi au ni najisi? Mtu anawezaje kujisafisha kutokana nacho? Je, uchafu wake huharibu Udhu?
Answer
Uchafu wa uke – unyevu unaotoka kwenye uke – ni majimaji meupe ambayo yako kati ya madhii na jasho. Hukumu iliyotolewa ili mambo kuwa rahisi kwa wanawake na kuondoa uzito kwao ni kwamba ni safi, kwa kufuata rai za Wanazuoni wa Fiqhi waliosema hivyo, sio lazima kuoosha, lakini inapendekezwa kuosha sehemu ambayo imegusana nayo kwenye nguo au mwili. Ingawa inachukuliwa kuwa safi, isipokuwa hubatilisha udhu.
Maelezo
Imethibitishwa katika Sharia ya Kiislamu kwamba usafi wa mwili hupatikana kwa kuondoa uchafu na najisi; usafi unahitajika wakati wa kufanya baadhi ya ibada kama vile Swala na kadhalika; Mwenyezi Mungu Anasema: {Enyi mlio amini! Mnapo simama kwa ajili ya Sala basi osheni nyuso zenu, na mikono yenu mpaka vifundoni, na mpake vichwa vyenu, na osheni miguu yenu mpaka vifundoni. Na mkiwa na janaba basi ogeni } [Al-Ma'idah: 6]. Abu Huraira R.A. amepokea kwamba Mtume (S.A.W) amesema: "Swala ya mwenye hadathi haitokubaliwa hadi atie udhu." Imepokewa na Bukhari.
Miongoni mwa Hadathi ni majimaji yatokayo kwenye uke wa mwanamke, ambayo huitwa "unyevunyevu wa uke". Wanazuoni wa Fiqhi wametoa maoni tofauti kuhusu hukumu ya maji ya uke kama ifuatavyo:
Rai ya kwanza: Huchukulia kila unyevunyevu unaotoka ukeni kuwa safi, iwe umetoka ndani au nje ya uke, lakini hutengua Udhu, na inapendekezwa kuoshwa.
Rai ya pili: Inaona kwamba kila unyevunyevu unaotoka ukeni kuwa najisi, iwe umetoka ndani au nje ya uke, na huharibu Udhu inapotoka, na ni lazima uoshwe.
Rai ya tatu: unagawanyika unyevunyevu wa uke katika makundi mawili:
La kwanza: Unyevunyevu safi, ambao una aina mbili:
Unyevunyevu unaotokea kwa mwanamke anapokaa, yaani eneo linalopaswa kuoshwa wakati wa kujisadia na kuoga.
Unyevu unaotoka katika sehemu ambayo uume wa mwanaume hufiki wakati wa kujamiiana.
Ya pili: unyevu usio najisi, ambao ni ule unaotoka ndani ya uke, yaani, kutoka sehemu iliyo nyuma ya ile ambayo uume wa mwanaume hufikia wakati wa kujamiiana.
Baada ya kutaja maoni haya, maoni sahihi zaidi na yalitolewa Fatwa ni kwamba majimaji haya ya uke – unyevu wa uke – ni safi, kama wanavyoamini wafuasi wa maoni ya kwanza, ili kuondoa ugumu wowote kwa mwanamke. Hata hivyo, majimaji haya ya uke yanabatilisha udhu, na inapendekezwa kuosha sehemu ambayo yameugusa mavazi au mwili.
Tunapata faida kutokana na yaliyotangulia:
1. Majimaji ya uke yanayotoka sehemu za siri za mwanamke ni safi.
2. Ingawa majimaji haya ni safi, isipokuwa yanatengua Udhu.
3. Sio lazima kuosha sehemu za siri kutokana na majimaji haya, lakini inapendekezwa kuosha eneo la nguo au mwili lililogusa.
Arabic
Englsh
French
Deutsch
Urdu
Pashto
Hausa
